Tumewekwa njia panda

Tumewekwa njia panda

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,103
Reaction score
828,988
Kesho tarehe 10.01.2018 inaweza kuwa siku nyingine mbaya kwa wale wapenda wabadiliko. Kesho kuna kulia ama kucheka kama ni kweli kutakuwa na mkutano Serena hotel.

Mchana wote wa leo mpaka mida hii huku mitandaoni hakufai ni mitifuano na speculations za kila aina kuhusu siku ya kesho na kile kitachasemwa. Kila upande umejiandaa vilivyo na madongo ama vilio ama shangwe za kutosha.

Kama ilivyo kwa mechi ngumu za Simba na Yanga kila upande Unahitaji ushindi. Chochote kitakachotokea kesho kitakuwa na hasara kubwa kwa upande mmojawapo.

Kama hahami furaha shangwe nderemo na vifijo vitakuwa vingi mno... Nchi italipuka kwa kushangilia. Na wale wa upande wa pili watakuwa wamepigwa mweleka mkubwa.

LAKINI ikitokea akasema anahama au hata kusema anastaafu harakati upande wa pili patakuwa hapatoshi japo si kwa kushangilia sana bali vijembe na dhihaka kwa wingi wake.

Huku kwingine kutakuwa ni simanzi kubwa na nchi itakuwa kama iko msibani
Kuna viashiria vya kutisha kidogo.

-Kwanini kaenda peke yake? Pengine ni haki yake
-Kwanini hakushirikisha viongozi wenzake? Kizungumkuti kiko hapa
-Alichoongea mbona kinapingana na uhalisia? Ngoja tutaona...

Itoshe tu kuamini kwamba hatatonesha makovu ya vidonda vinavyopona.. Hatasahau fadhila. Hatawageuka wale wote waliompenda na kumwamini sana.

Hatawavunja moyo na kuwaumiza kihisia wale wote walioumia na kuumizwa kwa ajili yake.

Inawezekana kabisa ukawa ni mwanzo mpya wa kutufanya tusonge mbele pale tulipokwamishwa.
 
Siasa mchezzo mchafu hata tunao waamini wanaenda kutugeuka ila ngoja tusubil hiyo kesho
IMG_20180109_223921_731.jpg
 
Kesho tarehe 10.01.2018 inaweza kuwa siku nyingine mbaya kwa wale wapenda wabadiliko. Kesho kuna kulia ama kucheka kama ni kweli kutakuwa na mkutano Serena hotel.
...
Kama hahami furaha shangwe nderemo na vifijo vitakuwa vingi mno... Nchi italipuka kwa kushangilia. Na wale wa upande wa pili watakuwa wamepigwa mweleka mkubwa.
...
Inawezekana kabisa ukawa ni mwanzo mpya wa kutufanya tusonge mbele pale tulipokwamishwa.
mshana jr, Hoja ya pili, niliyonukuu hapo, juu ni dhaifu kwa kuwa dhana yake ni kwamba Lowassa ndiye mwamuzi wa mwisho wa siasa za nchi hii

mshana jr kumbuka kuwa jina la Lowassa lilipokatwa CCM, ikafiatutiwa na sekeseke mkutano wa NEC wengi, nadhani na wewe, uliamini CCM ndiyo mwisho, mbendembende kifo cha mende. Matokeo unayajua.

mshana jr, hoja ya mwisho, nukuu hapo juu, nakubaliana na wewe ila nakukumbusha kuwa, nje ya ndani ya uongozi wa CCM (kwa maana ya vikao vyake), kila mwanachama ana nguvu. Lakini ndani ya chama, nguvu ya mwanachama mmoja mmoja haipo. Mwanachama anakihitaji chama kuwa na nguvu na chama hakimhitaji mtu mmoja mmoja kuwa na nguvu.

Hitimisho ni kwamba kurejea au kutokurejea kwa Lowassa CCM kuna tija/hasara kwa Lowassa kama Lowassa, BASI. Rejea hotuba zake zote ndani na nje ya CCM. Ila nina uhakika CHADEMA itaathirika sana akirejea CCM na sababu ziko nyingi km amewezesha kupata wabunge wengi - na Team Lowassa. Lakini CCM mpya, kama Lowassa hakujipanga vizuri jinsi ya kurejea, Team Lowassa itasambaratIka.

NI MAONI YANGU TU
 
mshana jr, Hoja ya pili, niliyonukuu hapo, juu ni dhaifu kwa kuwa dhana yake ni kwamba Lowassa ndiye mwamuzi wa mwisho wa siasa za nchi hii

mshana jr kumbuka kuwa jina la Lowassa lilipokatwa CCM, ikafiatutiwa na sekeseke mkutano wa NEC wengi, nadhani na wewe, uliamini CCM ndiyo mwisho, mbendembende kifo cha mende. Matokeo unayajua.

mshana jr, hoja ya mwisho, nukuu hapo juu, nakubaliana na wewe ila nakukumbusha kuwa, nje ya ndani ya uongozi wa CCM (kwa maana ya vikao vyake), kila mwanachama ana nguvu. Lakini ndani ya chama, nguvu ya mwanachama mmoja mmoja haipo. Mwanachama anakihitaji chama kuwa na nguvu na chama hakimhitaji mtu mmoja mmoja kuwa na nguvu.

Hitimisho ni kwamba kurejea au kutokurejea kwa Lowassa CCM kuna tija/hasara kwa Lowassa kama Lowassa, BASI. Rejea hotuba zake zote ndani na nje ya CCM. Ila nina uhakika CHADEMA itaathirika sana akirejea CCM na sababu ziko nyingi km amewezesha kupata wabunge wengi - na Team Lowassa. Lakini CCM mpya, kama Lowassa hakujipanga vizuri jinsi ya kurejea, Team Lowassa itasambaratIka.

NI MAONI YANGU TU
Umepangilia hoja zako vizuri.... Je nikisema tena wakati utaamua kutakuwa na ubaya wowote? I mean nimeandika nawe umeandika! Ni haki yetu sote so long hatuvunji sheria na taratibu za JF na tunabishana kwa hoja.. Ni wakati sasa wa kusubiri kuona muda utatuletea nini
 
Back
Top Bottom