figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,492
- 54,895
Habari wakuu,
Leo ni siku ya furaha sana baada ya tukio la kufunga ndoa. Kweli nmeamini haya mambo ya ndoa sisi binadamu ndo tunafanya yawe Magumu.
Leo Alhamis tumeamkia bomani kufunga ndoa.. Nmependa sana mfumo na utaratibu wao. Yaani raha kwenda mbele.
Tulikuwa watu wanne tu. Bwana harusi na msimamizi wake, na bibi harusi na msimamizi wake, wasimamizi ndo wameweka sahihi kama shahidi.
Baada ya ndoa tumeambiwa kama tukipeana talaka tusirudi bomani bali mambo ya talaka ni mahakamani. Ila mfungisha ndoa kasema haombei ifike huko kwenye talaka.
Iko hivi. Just unaingia, unaapa kama kawaida mbele ya watu na mbele ya Sheria kumpenda, kumlinda na kumvumilia mpenzi wako. Yaani utampenda hadi kifo kiwatenganishe, halafu unapewa karatasi unaanguka sahihi pale, mnapeana mkono kupongezana halafu mnapewa cheti chenu cha ndoa na mnaruhusiwa kuondoka kama mke na mme.
Jana nlipigiwa simu kwamba leo twende temeke kwenye ndoa. Ni rafiki yangu alitaka nimsimamie. Akanipa tips kidogo basi ikabidi nijiandae.
Asubuhi nimepanda daladala ya Mbagala nikashuka taifa kwenye saa moja kamili asubuhi. Nmefika nikakuta washafika.. Tukakaa nje kwa stori za kawaida kama watu wanaosubiri interview.
Mara bibi harusi na bwana harusi wakaitwa ndani, ilikuwa kwenye saa mbili asubuhi. Mara nasisi wasimamizi tukaitwa.
Tukapewa tips kidogo kwamba hawa wamekubaliana kufunga ndoa. Na sisi ndo mashahidi wao. Tukakubali.. Tukaambiwa ndani tusipige kelele wala kuongea ongea bali tumsikilize mfungisha ndoa, sababu akikasirika anaweza akaondoka au kutupangia siku nyingine.
Basi utaratibu ukaanza kufuatwa wa kiapo huku wakisoma kilichoandikwa. Baada ya hapo shughuli ikaisha. Tumetumia kama dakika 40 tukatoka nje na tukasanzuka.
Mimi ikabidi niwahi kibaruani na mwenzangu akawahi kibaruani. Japo nmekutana na Foleni ya Veta, Karume na Kigogo. Ila haina tabu. Nimefurahi sana katika hili tukio la leo. Nampongeza rafiki yangu kwa kutimiza ndoto na kuifikia siku hii kubwa katika maisha. Na sasa si wawili bali mwili mmoja.
Tutaonana keshokutwa jumamosi kujipongeza kwa hili tukio kubwa. Itakuwa poa tu..
Mimi na bwana harusi tunakunywa Kilimanjaro na bibi harusi na mwenzio watajua wenyewe huwa naona wanakunywa savana wine au Juice.
Tutawaongeza marafiki zetu wawili na bibi harusi Wawili. So wanywa Kilimanjaro tutakuwa wanne na tumepanga Kreti mbili zinatutosha.
Kati ya hawa marafiki wawili mmoja anatokea Dodoma atafika leo au kesho, atakuja na beberu tushatuma hela. So asubuhi tutaanza na supu kwa pamoja wote tukiwa 10. Cake order ilitolewa juzi na tulishalipa. Mchomaji nyama kashalipwa.
Mahari tushatoa japo bado twadaiwa kidogo.. Kikubwa ni kuunganisha hawa wapendanao.
Vijana. Msiogope kuoa.. Ni raha kwenda mbele.. Rafiki yangu sasa hivi anaanza kupikiwa vitu vitamu vitamu, ataanza kulala bila nguo na ataanza kuwahi nyumbani. Hakika kapata mwenza na mshauri wa maisha. Mungu awabariki.
Leo ni siku ya furaha sana baada ya tukio la kufunga ndoa. Kweli nmeamini haya mambo ya ndoa sisi binadamu ndo tunafanya yawe Magumu.
Leo Alhamis tumeamkia bomani kufunga ndoa.. Nmependa sana mfumo na utaratibu wao. Yaani raha kwenda mbele.
Tulikuwa watu wanne tu. Bwana harusi na msimamizi wake, na bibi harusi na msimamizi wake, wasimamizi ndo wameweka sahihi kama shahidi.
Baada ya ndoa tumeambiwa kama tukipeana talaka tusirudi bomani bali mambo ya talaka ni mahakamani. Ila mfungisha ndoa kasema haombei ifike huko kwenye talaka.
Iko hivi. Just unaingia, unaapa kama kawaida mbele ya watu na mbele ya Sheria kumpenda, kumlinda na kumvumilia mpenzi wako. Yaani utampenda hadi kifo kiwatenganishe, halafu unapewa karatasi unaanguka sahihi pale, mnapeana mkono kupongezana halafu mnapewa cheti chenu cha ndoa na mnaruhusiwa kuondoka kama mke na mme.
Jana nlipigiwa simu kwamba leo twende temeke kwenye ndoa. Ni rafiki yangu alitaka nimsimamie. Akanipa tips kidogo basi ikabidi nijiandae.
Asubuhi nimepanda daladala ya Mbagala nikashuka taifa kwenye saa moja kamili asubuhi. Nmefika nikakuta washafika.. Tukakaa nje kwa stori za kawaida kama watu wanaosubiri interview.
Mara bibi harusi na bwana harusi wakaitwa ndani, ilikuwa kwenye saa mbili asubuhi. Mara nasisi wasimamizi tukaitwa.
Tukapewa tips kidogo kwamba hawa wamekubaliana kufunga ndoa. Na sisi ndo mashahidi wao. Tukakubali.. Tukaambiwa ndani tusipige kelele wala kuongea ongea bali tumsikilize mfungisha ndoa, sababu akikasirika anaweza akaondoka au kutupangia siku nyingine.
Basi utaratibu ukaanza kufuatwa wa kiapo huku wakisoma kilichoandikwa. Baada ya hapo shughuli ikaisha. Tumetumia kama dakika 40 tukatoka nje na tukasanzuka.
Mimi ikabidi niwahi kibaruani na mwenzangu akawahi kibaruani. Japo nmekutana na Foleni ya Veta, Karume na Kigogo. Ila haina tabu. Nimefurahi sana katika hili tukio la leo. Nampongeza rafiki yangu kwa kutimiza ndoto na kuifikia siku hii kubwa katika maisha. Na sasa si wawili bali mwili mmoja.
Tutaonana keshokutwa jumamosi kujipongeza kwa hili tukio kubwa. Itakuwa poa tu..
Mimi na bwana harusi tunakunywa Kilimanjaro na bibi harusi na mwenzio watajua wenyewe huwa naona wanakunywa savana wine au Juice.
Tutawaongeza marafiki zetu wawili na bibi harusi Wawili. So wanywa Kilimanjaro tutakuwa wanne na tumepanga Kreti mbili zinatutosha.
Kati ya hawa marafiki wawili mmoja anatokea Dodoma atafika leo au kesho, atakuja na beberu tushatuma hela. So asubuhi tutaanza na supu kwa pamoja wote tukiwa 10. Cake order ilitolewa juzi na tulishalipa. Mchomaji nyama kashalipwa.
Mahari tushatoa japo bado twadaiwa kidogo.. Kikubwa ni kuunganisha hawa wapendanao.
Vijana. Msiogope kuoa.. Ni raha kwenda mbele.. Rafiki yangu sasa hivi anaanza kupikiwa vitu vitamu vitamu, ataanza kulala bila nguo na ataanza kuwahi nyumbani. Hakika kapata mwenza na mshauri wa maisha. Mungu awabariki.