Tumemwagana lakini amegeuka kero

Tumemwagana lakini amegeuka kero

INSONSILE

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2012
Posts
1,872
Reaction score
2,742
Kuna dada mmoja nilikuwa na mahusiano naye siku za nyuma,
Kadiri siku zilivyokuwa zinaenda nikaona mwenzangu tabia inabadilika,
Nikimuhoji anakuwa mkali kuliko kawaida, yaani kama mwanaume mpole unaweza kufyata.
Nikaona isiwe tabu, nikawa mpole tuu na hamsini zangu, sitaki kuzama kwenye penzi ambalo litakuja kunitesa.
Sasa ikafika hatua ya kuvunja rasmi uhusiano wetu, daah alikuwa ananirushia mipasho isiyo ya kawaida.
Sikutaka majibizano, katika kumi naweza kujibu moja tu, tena kwa maneno mefupi yenye hekima.

Sasa kila baada ya muda fulani lazima atupie sms au kwenye whatsapp mipasho kama ya pwani aisee,
Maneno ya mafumbo, ya kejeli mpaka basi. Sasa hebu nishaurini nifanyeje ili asinisumbue tena?
Au bado hajaridhika kuachana na mimi? Au anatafuta gia ya kurudi? Bahati mbaya sijafundishwa kudeka kwa mwanamke.
 
Kuna dada mmoja nilikuwa na mahusiano naye siku za nyuma,
Kadiri siku zilivyokuwa zinaenda nikaona mwenzangu tabia inabadilika,
Nikimuhoji anakuwa mkali kuliko kawaida, yaani kama mwanaume mpole unaweza kufyata.
Nikaona isiwe tabu, nikawa mpole tuu na hamsini zangu, sitaki kuzama kwenye penzi ambalo litakuja kunitesa.
Sasa ikafika hatua ya kuvunja rasmi uhusiano wetu, daah alikuwa ananirushia mipasho isiyo ya kawaida.
Sikutaka majibizano, katika kumi naweza kujibu moja tu, tena kwa maneno mefupi yenye hekima.

Sasa kila baada ya muda fulani lazima atupie sms au kwenye whatsapp mipasho kama ya pwani aisee,
Maneno ya mafumbo, ya kejeli mpaka basi. Sasa hebu nishaurini nifanyeje ili asinisumbue tena?
Au bado hajaridhika kuachana na mimi? Au anatafuta gia ya kurudi? Bahati mbaya sijafundishwa kudeka kwa mwanamke.

Mimi hiyo hali ndiyo ninayo sasa ila nimenyamaza kimyaaaaaa
 
wazoee hao viumbe wanaokwenda chooni kwa kuchuchumaa

Stay calm yana mwisho hayo

Mblock kila mahala kuanzia kwenye simu hadi akilini
 
Usije ukajaribu kujibizana na mwanamke kuwa mkimya tu
 
Hahahaha tatizo unapoteza muda kusoma ujumbe ambao kiukweli unajua utakuwa na dhima zipi..!
 
Nipe namba yake nikuonyeshe jinsi ninavyoweza kuyatuliza magumegume yasikusumbue tena.
 
Mkuu Crashwise, watu wa Arusha mna akili sana. Ndo maana mko mbali kimaendeleo
 
Last edited by a moderator:
Mkuu SIPIYU30, binadamu tunatofautiana kitabia. Kuna watu ambao wakiachana na wapenzi wao hupenda kutoa mipasho, wengine kejeli, wengine matusi wengine hudiriki hata kulipiza kisasi na kudiriki kuwadhuru wale ambao walikuwa wanawapenda.

Mimi nakushauri wewe ukae kimya jifanye kama huoni wala husikii atendayo, atahangaika weeeee... atakuchamba weeee... atakusema weeee... lakini kama hutojibu chochote mwisho wa siku atachoka kwa sababu atajiona mjinga na anajisumbua bure lakini ukijaribu kumjibu na utaanzisha vita ambayo hutaweza kuizima ambayo itakugharimu sehemu kubwa ya maisha yako na kukuchafulia jina lako maana mtu anapokuwa na hasira haoni shida hata kutoa siri za ndani ambazo hakupaswa kuzitoa kwa namna yoyote ile na bila shaka unafahamu kuwa mwanaume hawezi kubishana na mwanamke kwa sbabau mwanamke ana uwezo wa kuongea zaidi kuliko mwanaume. So kuwa makini mkuu, dont let your anger take control of your judgement.
 
Last edited by a moderator:
Bado anakupenda so Roho inamuuma!!!

Solution we piga kimya na kama inawezekana m-block.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom