Tumejiandaaje na majanga ya dharura?

Tumejiandaaje na majanga ya dharura?

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,938
Reaction score
831,432
Huenda ikawa taifa limepata msiba mwingine mkubwa baada ya ndege ya Precion Air kupata ajali Ziwa Victoria ikikaribia kutua Bukoba Airport.

Ndege hii ni ileile ya jana iliyopata hitilafu ya engine kuzimika na kutua kwa dharura Kilimanjaro Airport.

Kabla ya ajali hii kuna mwanajamii Forums kwa jina la maharage ya ukweni alitabiri kutokea kwa ajali ya ndege! Pengine kwa mataifa yanayozingatia mambo ya kiroho hili lingetosha kuwa kwenye alert! Lakini hili si mukatadha wa mada hii.

Kuna mambo yanafikirisha sana kwenye hii ajali..! Kuna mambo sio kipaumbele kwetu hasa matukio ya dharura.

Tutawapoteza watanzania wenzetu kwa kukosa vifaa sahihi na muhimu kwenye uokoaji. Hapakuwa na helikopta yoyote ya kutoa msaada kwenye uokoaji.

Hapakuwa na hata tag boat ya kuivuta ndege nchi kavu! Imevutwa kwa kamba na watu.

Tuna bajeti nono kwa ajili ya Ma V8 ya viongozi lakini si kwenye dharura na uokozi.. Unapoipa siasa thamani kubwa kuliko taaluma haya ndio madhara yake.

Sililaumu sana jeshi la zimamoto na uokoaji, kuna wakati likiwa limeona sasa kuwepo na umuhimu mkubwa wa kuwa na vifaa vya uokoaji zikiwepo drone za uokoaji watoa maamuzi waliishia kutumbuliwa na mwanakwenda! Kama tatizo lilikuwa mkataba wa kifisadi si ungetafutwa mwingine bora lakini si kuacha kabisa kuagiza vifaa hivyo muhimu sana.

Tuna majengo marefu sana kwa sasa hapa nchini na madaraka makubwa lakini sina hakika kama kitengo chetu cha Zimamoto na uokoaji kina uwezo wa kuyahudumia pindi litakapotokea majanga.

Maisha ya wananchi wengi yanaangaamia kwa kuipa siasa thamani kubwa kuliko weledi.

Kuna wale watoto wa Mtwara walipata ajali na gari ya shule! Huwezi kuamini walibwebwa na magari ya wagonjwa mpaka dar wakati ingetumika helicopter wangefikishwa kwa haraka Muhimbili na wangesaidiwa kwa haraka.

20221106_135727.jpg
20221106_135606.jpg
 
Huenda Mama Hamia Sahani Sururu akalifanyia kazi ila sina uhakika na utendaji kazi wake na chawa wake.
Kwenye ile mikopo hakuna aliyejitolea kutusaidia tundege tuwili tutatu twa uokozi na vifaa vyakwe? Ama ajali ni kudra?
 
Nimeongea na Nurse hapo hosptali ya Government Bukoba kanambia wameshapokea maiti 10 Hadi Muda huu na baadhi ya waliofariki tunawajua..

Inasikitisha Sana
Poleni sana sana! Inanikumbusha ajali ya MV Bukoba wengi walipoteza maisha kwakuwa serikali haikuwa na vifaa sahihi vya uokozi
 
Huwa Hatujiandai Kwa Lolote Mpaka Litokee, Pictures Zote Ulizoweka Zinajieleza Bayana Kwanza Hazina Siasa Bali Ukweli Mtupu
Tunachimba Visima Sasa Wakati Tete

BUKOBA Ndege Hadi Sasa Haijaweza Kuondolewa Ziwani
Inaburutwa Na Magari Tu
 
Kuna Jamaa alibashiri hii ajali itatokea humu JF, watu wakamchukulia poa tu

 
Huwa Hatujiandai Kwa Lolote Mpaka Litokee, Pictures Zote Ulizoweka Zinajieleza Bayana Kwanza Hazina Siasa Bali Ukweli Mtupu
Tunachimba Visima Sasa Wakati Tete

BUKOBA Ndege Hadi Sasa Haijaweza Kuondolewa Ziwani
Inaburutwa Na Magari Tu
Fikiria serikali wanaweza kutumia Helicopter kuzindua matokeo ya Sensa lakini serikali hiyohiyo ikashindwa kutumia Helicopter kuokoa watu. Yani wanaweza kutumia Helicopter kwenye mambo yasiyo ya muhimu halafu kwenye mambo muhimu kama hili la ajali ya ndege Bukoba wakashindwa.
 
Fikiria serikali wanaweza kutumia Helicopter kuzindua matokeo ya Sensa lakini serikali hiyohiyo ikashindwa kutumia Helicopter kuokoa watu. Yani wanaweza kutumia Helicopter kwenye mambo yasiyo ya muhimu halafu kwenye mambo muhimu kama hili la ajali ya ndege Bukoba wakashindwa.
Inasikitisha sana mkuu, au helicopter zipo kwa ajili ya watu maalum na shughili maalum ila sio shughuli za uokoaji?
 
Kwa eneo ilipo tugboat isingefanya kazi.
Tugboat hutumia kusukuma au kuvuta, isingeweza vuta kwenda nchi kazi sababu ya kina kifupi

Hii ndege ukifuatilia flight history haijaenda sehemu tofauti na Mwanza, BK, Dsm kwa hizi siku 3
 
Back
Top Bottom