tikatika
JF-Expert Member
- May 6, 2011
- 2,330
- 4,123
yaan kila nikijiuliza maswali nakosa majibu. hivi wakati nchi inaingia kwenye uchaguzi mkuu nani anasimamia misingi ya nchi!! je ni wanasiasa au watumishi wa umma ikiwemo taasisi nyeti ya TISS??
kama na usalama wanahusika inakuaje wanakaa pembeni katika kipindi kigumu cha kumpata kiongozi wa nchi??
hivi kweli 2015 usalama wa Taifa mlikuwepo waheshimiwa wangu??
nauliza tu msinitafute ila nina maswali mengi sana siwez kuyaweka bayana hapa. maana naweza leta taharuki.
ninavyojua nyie ni washauri wakuu mnaweza ingia chama chochote na mkakaa nao mezani kuwaambia huyu hafai kupewa cheo kikuu cha nchi huyu anafaa huku mmeenda na vielelezo rukuki huko vyumbani. nani atawapinga mkienda na historia ya mgombea ?? jua nyie ndio mmepewa mamlaka ya kutuchunguza. mafaili yetu mnayo nyie mjue!!
hivi mnajua nyie ndio injini ya nchi??
wapuuzeni wanaodhani kazi yenu ni kutafuta watu wabaya katika nchi na kuwanyooshea kidole tu, hako ni kasehemu kadogo katka majukumu yenu. kazi yenu kubwa ni kusimamia uchumi wa nchi. uchumi ukiyumba inchi inakua haina usalama tena!!
kauli ya rais inaweza vuruga uchumi wa nchi hata kwa miaka 20. ina uwezo wa kuleta hasara ya miaka hata 100!! anaweza leta hasara ya roho za watu maelfu. sitak niende kiundani mnajua kinachoendelea!! kiukweli mimi nawalaumu nyie.
jipeni muda mjitafakari mnavyolitia taifa hasara. kauli ilitamkwa kwenye tv tu ila tunadaiwa ng’ombe nne na mbuzi kadhaa!! mlikua wap!! haka ni ka mfano tu yapo mengi nyie ndio nawalaumu siku hadi siku. na miaka ijayo kitengo chenu ndio kitabeba lawama zote. maana nina uhakika kama taifa tutavunja record kwa mambo kadhaa wa kadha yatakayo litia taifa hasara na madoa kibao.
tafadhari wazee wa kazi huko mbele msirudie makosa yanaligharimu taifa.
kama na usalama wanahusika inakuaje wanakaa pembeni katika kipindi kigumu cha kumpata kiongozi wa nchi??
hivi kweli 2015 usalama wa Taifa mlikuwepo waheshimiwa wangu??
nauliza tu msinitafute ila nina maswali mengi sana siwez kuyaweka bayana hapa. maana naweza leta taharuki.
ninavyojua nyie ni washauri wakuu mnaweza ingia chama chochote na mkakaa nao mezani kuwaambia huyu hafai kupewa cheo kikuu cha nchi huyu anafaa huku mmeenda na vielelezo rukuki huko vyumbani. nani atawapinga mkienda na historia ya mgombea ?? jua nyie ndio mmepewa mamlaka ya kutuchunguza. mafaili yetu mnayo nyie mjue!!
hivi mnajua nyie ndio injini ya nchi??
wapuuzeni wanaodhani kazi yenu ni kutafuta watu wabaya katika nchi na kuwanyooshea kidole tu, hako ni kasehemu kadogo katka majukumu yenu. kazi yenu kubwa ni kusimamia uchumi wa nchi. uchumi ukiyumba inchi inakua haina usalama tena!!
kauli ya rais inaweza vuruga uchumi wa nchi hata kwa miaka 20. ina uwezo wa kuleta hasara ya miaka hata 100!! anaweza leta hasara ya roho za watu maelfu. sitak niende kiundani mnajua kinachoendelea!! kiukweli mimi nawalaumu nyie.
jipeni muda mjitafakari mnavyolitia taifa hasara. kauli ilitamkwa kwenye tv tu ila tunadaiwa ng’ombe nne na mbuzi kadhaa!! mlikua wap!! haka ni ka mfano tu yapo mengi nyie ndio nawalaumu siku hadi siku. na miaka ijayo kitengo chenu ndio kitabeba lawama zote. maana nina uhakika kama taifa tutavunja record kwa mambo kadhaa wa kadha yatakayo litia taifa hasara na madoa kibao.
tafadhari wazee wa kazi huko mbele msirudie makosa yanaligharimu taifa.