Tumefikaje hapa tulipo?

Hiyo ni dhana yako wewe, waulize watu wa zamani hapa kijiweni hususa Mwanajiji na Rev.Kishoka hata hao viongoI wa Chadema kina Mnyika walikuwa hapa enzi zile za kina Zitto, Maria Sarungi (Woman of substance) Kitila n.k watakwambia mimi ni mtu wa aina gani na ipi misimamo yangu katika mijadala kama hii.

Mimi sibishani na mtu ila hujadili ideals na issues navyoziona na nina misimamo isoteteleka wala kugeukageuka.

Sina Ushabiki wa mpira sijui wee Simba au Yanga, Manchester vs Arsenal sijui kuchukua upande kwa sababu ambazo hazinisaidii.

Majuzi tu hapa nilisema Chadema wanataka rais amwachue Tundu Lissu na hawataingia maridhiano mpaka Lissu atoke jela, watu wakanivamia kuwa Chadema haitaki msamaha wa rais wala nani. Bila shaka sasa hivi mnanielewa.

Maasalaam
 
Endapo, wafuasi wa CCM hawataona hayo kuhusu chama hicho
Hili la "wafuasi wa CCM" tuwe wakweli wenyewe.
Ni wafuasi gani hawa wa CCM wanaokubali viongozi wao wanayoyafanya sasa. Hao wafuasi wa CCM kweli wapo; au na wao wamelazimishwa kama sisi sote tunavyolazimishwa kukubali haya yanayoendelea.

Wewe, mkuu 'Drifter' hata kweli hukuona hata uteuzi tu wa watia nia ndani ya chama, hadi ngazi ya Rais ilivyovurugwa maksudi, kuwanyima ushiriki hao hao wafuasi wa CCM?

Ni hoja yangu kwamba tunawahusisha tu kwa makosa hao wafuasi wa CCM na hili kundi ambalo limeamua kukitumia chama (jina) vibaya.
 
Hiyo ni dhana yako wewe, waulize watu wa zamani hapa kijiwen
Watu wa zamani hapa ni akina nani kama hata hujui unayejadili naye na anakueleza hayo hayo aliyoyashuhudia toka huko mwanzo.
Au Alzheimer ilishakuingilia tayari?

Mambo yako yapo vilevile, kama yalivyokuwa huko mwanzo, hujabadilika chochote.
Hata sijui kama Kibara bado unajuwa ipo wapi katika kumbukumbu zako.
 
Nimesoma hayo unayoyaita maoni yako na kikubwa nilichoona ni kwamba yana VIASHIRIA VYA UHAINI.
 
Exactly! Mkapa alutuachia janga.
 
Mgawanyiko wa CCM mwaka 2015 ilikuwa ni descendant ya uchaguzi wa mwaka 2005.
 
Ndio kawaida yenu watu wa Chadema, mkipigwa pini tu mnaanza kwenda personal!

Nilimkosoa Mkapa enzi za #Jambofurums, tukahamia #Bcstimes wakati wa JK na tukamkoma nyani vizuri sana zile scandal za Richmond, Tanesco na Dowans. Yalofuata ndwele tugange yajayo. Hunijui, sikujui uwe msingi wa hoja zetu.

KIongozi pekee ambaye mimi binafsi nakiri nilikuwa upande wake muda wote ni Magufuli kwa sababu simkubali Lowassa na hata Tundu Lissu maana sio viongozi wanao nivutia kwa sifa, iitikadi wala kimaadili.

Hilo halina Ubishi kabisa lakini siwezi kukidharau chama chochote au Wanachama wake kwa sababu ya misimamo ya Kiongozi wake. Labda niseme ACT Wazalendo pekee ndio chama nachoshindwa kabisa kuelewa mwelekeo wake.
 
Unapointi haswa!

Sijui kwa nini Mkapa alikomaria sana zile chaguzi kana kwamba ni mwisho wa dunia!

Nakubaliana nawe, matatizo yalianzia hapo kwa Mkapa.
 
Ndio kawaida yenu watu wa Chadema, mkipigwa pini tu mnaanza kwenda personal!
sijui ni mara ngapi wewe umenihusisha na CHADEMA.
Ulikwishaona mahali popote nikidai kuwa nipo CHADEMA?

Kwani siwezi kuzungumzia maswala ya Tanzania bila kuwa ndani ya chama chochote?

Nijuavyo, wewe hata huko CCM hupo; bali unatetea huko kwa sababu zinazojulikana

Mimi nawatetea CHADEMA sasa hivi, kwa sababu ni tofauti kabisa na hiyo CCM unayoitetea wewe; na huipendi CHADEMA kwa sababu ndiyo inayotishia maslahi yanayokufanya uambatane na CCM bandia inayovuruga utulivu wa taifa hili.

Achana na unafiki, kuuliza maswali ambayo unajuwa majibu yake.
 
Lugha yako mkuu pekee inakuacha Uchi. Mtu yeyote anaye wachambua wafuasi wa Chama kingine cha Siasa kwa imani zao tayari inamweka yeye upande wa pili. Isitoshe kauli zako kwangu zinaashiria wazi unadhani mimi CCM na hata kama niwe CCM sidhani kama ni kosa au hoja ya msingi kwa sababu sote KIKATIBA tuna HAKI sawa ya kujiunga na chama chochote cha Siasa. Mzee Warioba mpaka kesho ni CCM unamuonaje?

Unachofanya wewe ni kama vile leo nikianza kuwasema Waislaam wafuasi wa dini yao kwa ubaya, bila shaka watu watajua mimi ni Mkristu laaa kwa nini nawatukana?
Wewe fuata Chama unachokiamini kwa itikadi, mrengo au sera zake na wengine nao waachie Haki yao ya Kikatiba kufuata chama wanachokipenda.
 
Unayo matatizo 'Mkandara'.
Sasa eleza ni nani hakuwepo Jambo, au BUsinessTimes. "Kumkoma Nyani Giledi", mbona ni juzi hapa na lile dude la Malicela!

Nasema unayo matatizo, kwa sababu hapa unajifanya kumkubali Magufuli; kwa sababu tofauti kabisa na hizo ulizotaja wewe. Magufuli alikuwa na "itikadi" zipi za kusema zilikuvutia. "Maadili? kwa magufuli?
Magufuli alikuvutia kwa sababu zilezile nilizozitaja walizo nazo akina Ritz na watu wa aina hiyo.

ACT na CUF najuwa huna habari navyo kabisa vyama hivyo. Hukuhitaji hata kuvitaja kabisa. ulaghai wote huu hasa ni wa nini?

Ni hivi: kama hunijui, mimi huwa sina simile na watu wanafiki. Siwezi kamwe kusema nyeusi ni nyekundu. Nitaisema vilevile ilivyo.
Kutompenda kwako Lissu, inawezekana ikawa ni kwa sababu hizo hizo za yeye kutopindisha mambo.

Vipi, unamwonaje Samia, maana hujamzungumzia kabisa.
 
Daaah, sababu gani hizo? ebu nijulishe maana miye sijui kama nawatetea CCM. Na sijui kama nayoyasema hapa yataniacha salama jambo ni imani yangu kwa Maslahi mapana ya Taifa letu.

Hivi kweli kuna mtu hapa (at that time and day tarehe 31 October 2025) aliweza kusema hadharani kumtaka rais Samia ajiuzuru kulinusuri Taifa? I did that...
 
Lugha yako mkuu pekee inakuacha Uchi. Mtu yeyote anaye wachambua wafuasi wa Chama kingine cha Siasa kwa imani zao tayari inamweka yeye upande wa pili
Hii siyo mbinu mpya hata kidogo kwa watu wa mlengo wako.
Sina tatizo kabisa na hilo kwa sababu siogopi kulizungumzia. Watu ninaowasema juu ya imani yao ni kundi la aina yenu, mnaojifichaficha, au mnakuwa wawazi kwama walevi kwa imani. Unapojipambanua kuwa kundi la aina hiyo, sina tatizo lolote la kukujadili; kwa sababu maslahi yenu ni kinyume na maslahi ya waTanazia wanaotaka mshikamano baina yao bila ya kujali imani zao.

Kwa hiyo usiwe na shaka, ukiwa upande wa ulevi wa imani, nitakujadili tu, bila ya hofu ya kusemwa juu ya kuchambua watu.
 
Umenena vyema! Wa kututoa hapa tulipo ni kichaa mmoja tu atakayejitokeza kutoka JWTZ. Tusitegemee viongozi wa vyama vya siasa kwamba ndio watatuondoa kwenye huu mkwamo! Bahati mbaya tumekuwa na Jeshi ambalo nalo linaongozwa na machawa! Shenzi kabisa!
 
Hivi kweli kuna mtu hapa (at that time and day tarehe 31 October 2025) aliweza kusema hadharani kumtaka rais Samia ajiuzuru kulinusuri Taifa? I did that...
Najuwa hata CHADEMA walitamani sana "aachie" kama ulivyosema wewe; sasa sijui tatizo lako na CHADEMA ni lipi; kwa sababu ya Tundu Lissu pekee?
Lakini umekwishasema mwenyewe huwapendi CHADEMA; hata wakati wakipambania kuleta mabadiliko, ambayo naona baadhi yake na wewe kumbe unayapenda.
 
Kifupi Mkuu wewe unamkubali Tundu Lissu kwa sababu zako nami nilimkubali Magufuli kwa sababu alifanya exactly Chadema walivyojitangaza kabla ya Uchaguzi wa 2010 - 2015 baada ya kuona nchi hii haitawaliki pasipo kumpata rais DIKTETA. Rais anayeweza kufanya maamuzi magumu na sera zikaandaliwa ambazo Magufuli alizifuata.

Ukiniuliza kama Udikteta ule ulikuwa mzuri nitasema YES! na watu kama Shangazi na Tundu Lissu ambao hata baada ya rais kutangaza hali ya Vita vya Kiuchumi wao wakawa upande wa maadui sikupenda kabisa utovu wa Uzalendo kufikia kiasi kile.

Na bahati mbaya sana kwao nilikuwa nawajua vizuri kiasi kwamba sikuweza kubadilisha msimamo wangu.

Anyway tuache kuzungumzia hisia zetu maana haziwasaidii Watanzania katika adha tuliyopo. Kama sikosei tulionana Ohio 2008 kwenye Old Skools..am I right?

Maasalaam
 
Umenena vyema! Wa kututoa hapa tulipo ni kichaa mmoja tu atakayejitokeza kutoka JWTZ. Tusitegemee viongozi wa vyama vya siasa kwamba ndio watatuondoa kwenye huu mkwamo! Bahati mbaya tumekuwa na Jeshi ambalo nalo linaongozwa na machawa! Shenzi kabisa!
Waambie waTanzania kwa umoja wao na wingi wao washirikiane na chama kufanya kazi hiyo. Inawezekana sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…