fikiria SALIM A. SALIM hana makazi DAR, na anatakiwa afanye kazi ya umma akiwa Dar, wakati huo huo atatakiwa asifanye kazi nyingine yoyote kwa ajili yake na familia yake zaidi ya ile ya tume. pendekeza alipwe kiasi gani? kwa kazi (msalaba) wanayotakiwa kuifanya, hiyo posho ya sh. 300000/= wala si chochote kwa vigezo vyote. pamoja na kwamba mgawanyo wa raslimali zetu haufanywi kwa haki kwa raia wake lakini si kweli vilevile kwamba inatakiwa igawiwe sawasawa (lazima itegemee na uzito wake). kazi inayofanywa na akina warioba si kila mtu anaweza kuifanya. kazi maalumu kwa watu maalumu kwa malipo maalumu. kama katika tume hiyo kuna na watu wa hovyo hovyo basi hiyo ni juu ya aliyewateua. ndiyo maana watu kama kofi anan yuko kila pahala duniani kushughulika na kutatua migogoro. kwani akina ali hassan mwinyi hawapo? mbona hawaendi huko? Ni kazi maalumu kwa watu maalum, na malipo yake lazima yawe maalumu. ni kazi inayoinvolve brain na risk zote. tuwaacheni wachape kazi.