Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,436
- 5,234
Tume ya Rais ya Uchunguzi wa matukio yaliyojitokeza wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025 imeanza kufanya vikao vyake kwa faragha, na kuzuia waandishi wa habari kuingia kwenye ukumbi ambapo waathirika wanatoa ushahidi wao.
Rais Samia Suluhu Hassan aliunda tume hiyo kufuatia maandamano ya vurugu yaliojitokeza siku ya kupiga kura, Oktoba 29, 2025, kwa lengo la kubaini sababu za machafuko hayo na kuweka msingi wa upatanisho wa kitaifa.
Tangu vikao hivyo vya uchunguzi vyaanze, vyombo vya habari vimekuwa vikiripoti kuhusu shughuli za tume hiyo na ushahidi unaotolewa na mashahidi.
Tarehe 23 Januari 2026, gazeti la The Citizen liliripoti kikao kilichofanyika Magomeni, Dar es Salaam, ambapo waathirika mbalimbali walishiriki uzoefu wao.
Leo, Januari 24, 2026, tume hiyo imefanya kikao chake katika Wilaya ya Ubungo, ambapo wakazi walikuja kutoa ushahidi kuhusu matukio waliyojionea au kushuhudia siku ya uchaguzi na jinsi yalivyoathiri maisha yao.
Hata hivyo, tofauti na vikao vya awali, tume hiyo ilitangaza kuwa waandishi wa habari hawataruhusiwa kuingia ukumbi wakati ushahidi unapoonyeshwa.
Tangazo hilo lilitolewa na jaji mstaafu Profesa Ibrahim Juma, aliyekuwa akiongoza kikao, akiwa amefungua mkutano, na kueleza kuwa uamuzi huo ulilenga kulinda faragha ya mashahidi.
============
Akizungumzia uamuzi huo wa Tume, mwandishi wa gazeti la Raia Mwema, Selemani Msuya amesema uamzi wa Tume una athari chanya na hasi.
Kuhusu athari chanya, amesema tangu Tume hiyo imeanza kufanya vikao na matukio mengi yanayoendelea vikaoni kurushwa kwenye vyombo vya habari, yamekuwa yakiibua hisia mbaya katika jamii.
“Baadhi ya vyombo vya habari vimekuwa vikirusha mubashara au kusambaza taarifa za waathirika ambazo kwa watazamaji zinaibua hisia mbaya, ukiona video ukatokwa machozi, kwa eneo hili kuzuia urushaji wa moja kwa moja wa taarifa ni jambo jema,” amesema.
Kwa upande wa mtazamo hasi, Msuya ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi wa Vyombo vya Habari Tanzania (Jowuta), amesema kuzuia waandishi kuingia kwenye vikao kunaathiri ubora wa habari ambazo wangezitoa kwa jamii.
“Kuwataka waandishi wasubiri taarifa ya mtu wa Tume, inawanyima kupata habari ambayo kila mwandishi angeitaka, pia, inaondoa uwazi wa jamii kusikia yanayosemwa na watu huko, ili hata ripoti ya Tume ikitoka watu waiamini,” amesema.
Pia Soma: Rais Samia aunda Tume ya Uchunguzi wa matukio ya Uvunjifu wa Amani wakati na baada ya Uchaguzi 2025
Rais Samia Suluhu Hassan aliunda tume hiyo kufuatia maandamano ya vurugu yaliojitokeza siku ya kupiga kura, Oktoba 29, 2025, kwa lengo la kubaini sababu za machafuko hayo na kuweka msingi wa upatanisho wa kitaifa.
Tangu vikao hivyo vya uchunguzi vyaanze, vyombo vya habari vimekuwa vikiripoti kuhusu shughuli za tume hiyo na ushahidi unaotolewa na mashahidi.
Tarehe 23 Januari 2026, gazeti la The Citizen liliripoti kikao kilichofanyika Magomeni, Dar es Salaam, ambapo waathirika mbalimbali walishiriki uzoefu wao.
Leo, Januari 24, 2026, tume hiyo imefanya kikao chake katika Wilaya ya Ubungo, ambapo wakazi walikuja kutoa ushahidi kuhusu matukio waliyojionea au kushuhudia siku ya uchaguzi na jinsi yalivyoathiri maisha yao.
Hata hivyo, tofauti na vikao vya awali, tume hiyo ilitangaza kuwa waandishi wa habari hawataruhusiwa kuingia ukumbi wakati ushahidi unapoonyeshwa.
Tangazo hilo lilitolewa na jaji mstaafu Profesa Ibrahim Juma, aliyekuwa akiongoza kikao, akiwa amefungua mkutano, na kueleza kuwa uamuzi huo ulilenga kulinda faragha ya mashahidi.
============
Akizungumzia uamuzi huo wa Tume, mwandishi wa gazeti la Raia Mwema, Selemani Msuya amesema uamzi wa Tume una athari chanya na hasi.
Kuhusu athari chanya, amesema tangu Tume hiyo imeanza kufanya vikao na matukio mengi yanayoendelea vikaoni kurushwa kwenye vyombo vya habari, yamekuwa yakiibua hisia mbaya katika jamii.
“Baadhi ya vyombo vya habari vimekuwa vikirusha mubashara au kusambaza taarifa za waathirika ambazo kwa watazamaji zinaibua hisia mbaya, ukiona video ukatokwa machozi, kwa eneo hili kuzuia urushaji wa moja kwa moja wa taarifa ni jambo jema,” amesema.
Kwa upande wa mtazamo hasi, Msuya ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi wa Vyombo vya Habari Tanzania (Jowuta), amesema kuzuia waandishi kuingia kwenye vikao kunaathiri ubora wa habari ambazo wangezitoa kwa jamii.
“Kuwataka waandishi wasubiri taarifa ya mtu wa Tume, inawanyima kupata habari ambayo kila mwandishi angeitaka, pia, inaondoa uwazi wa jamii kusikia yanayosemwa na watu huko, ili hata ripoti ya Tume ikitoka watu waiamini,” amesema.
Pia Soma: Rais Samia aunda Tume ya Uchunguzi wa matukio ya Uvunjifu wa Amani wakati na baada ya Uchaguzi 2025