Uchaguzi 2020 Tume ya Uchaguzi, NEC ilikuwa kimya kwa TLP na UDP kuiunga mkono CCM iwe kimya pia kwa ACT-Wazalendo

Mimi ni Mwananchi mwenzako ila nakiri hapa unatulisha tango pori. Naweza kusema ndugu yangu Kijana katika hoja yako umekurupuka maana Aliyetia neno kuhusu uchumba wa CHADEMA na ACT wala sio Time bali ni Msajili wa Vyma vya Siasa ambaye ndie msimamizi wa hivyo vyama.

Hebu itafute barua waliyoandikiwa ACT au Chadema Kisha usome anuani imetoka wapi.

Lakini pia, Sheria za Uchaguzi zipo wazi nadhani Tume Kama ingesema kitu katika hilo ingetaka tu Mgombea aliyetangaza kujitoa katika ulingo wa Uchaguzi kuandika barua ambayo ingethibitishwa na Chama chake na Kisha kuiwasilisha tume kabla ya Saa 12 jioni.

Ila sina hakika Kama Benard Kamilius Membe hadi Sasa amesha toa taarifa Tume ya Uchaguzi na Kama wamesha toa Basi Mkurugenzi wa Tume ataitaarifu umma juu ya hilo Kama alivyofanya kwa wagombea wa majimbo ya Chalinze na Madaba walioingia mitini.

Hivyo ndugu yangu hili andiko lako umelikosea na umelenga kuwapotosha wasomaji wa JF na kuwaaminisha kuwa Time ya Uchaguzi ndiyo inakosea. Ilhali ni taasisi nyingine.

Lakini Mbona unauhakika gani Kama TLP na UDP hawakufuata utaratibu wa kutoa taarifa mapema ya kuunga mkono Mgombea wa CCM? Je unavithibitisho? Kumbuka TLP na UDP wao hata Tume hawakusogea kuchukua Fomu lakini ACT alifika na kuchukua Fomu na akateuliwa kuwa Mgombea wa Kiti cha Rais, hivyo mimi nadhani tunadili pia huo utofauti wa Ambaye hajachukua Fomu na aliyechukua na kuteuliwa kuwa Mgombea.
Nguruka, nyangabo,bweru, itebula,mganza, Nguruka Kati,lugongoni A&B hapawezi pakatoa mtu mwenye Mawazo kama wewe. Unawaaibisha wana MAGEUZI wa Nguruka.
 
Wananchi wana akili za kutosha, inachotaka kukifanya ACT kwa chadema hakitofautiani sana na walichokifanya UDP na TLP kwa CCM, uwongo kweli? Hatukisikia mkutano mkuu wa UDP ukiliamua lile na wala hatukuisikia tume ikinyanyua kidole juu.

Lakini hata hivyo sio lazima chama cha siasa kupiga kampeni kwenye majimbo yote, ACT inaweza kukaa kimya au kujitoa kwasababu mbalimbali ikiwemo ya ukata ikaiacha chadema tu ikipiga kampeni majimbo yote.

Hata CCM iliposhinda uchaguzi mwaka 2015 bila kutarajia iliwajumuisha kwenye serikali yake baadhi ya wapinzani. Hii ni dalili kuwa vyama vilivyotoa wanachama waliojiunga kwenye kuunda serikali viliisaidia CCM kwenye uchaguzi kwa aina moja au nyingine kimyakimya, na ndiyo maana hakuna mtu kutoka chadema aliyeteuliwa kuwa hata katibu mtendaji wa kata kwenye serikali ya CCM. Tume yetu haikunyanyua jicho.

Sisi Wapiga kura tuna imani na tume yetu lakini tume yetu pia lazima iwe na imani na wapigakura kuwa tunazo kumbukumbuku na uelewa wa mambo.
Tume inafanya kazi ya CCM, huu ni mwendelezo tu walianza na kuwajazia form wagombea wa CCM
 
Ndani ya hii tume kuna shida na ofisi ya msajili kuna shida kubwa! Siku zote ukiwasikia wamenyanyua mdomo kukemea jambo ujwe ni kwa faida ya chama kilichoko ikulu na si vingnevyo! Baada ya huu uchaguzi mkuu, lazima tudai katiba mpya ili itakayofumua na kuziondoa taasis zote kutoka mfukoni mwa CCM na kuwa taasis huru! Sote kwa pamoja tuendelee kuelimisha watu watumie vema sanduku la kura tukaiweke kando CCM ndipo haya yote yatawezekana!
Ofisi hizi mbili zinafanya mambo kama yale yaliyokuwa yakifanywa na wakoloni kuchelewesha Uhuru wa Tanganyika na Uhuru wa Zanzibar wakati wa chaguzi. Kuna Uzi mwembamba Sana unaotenganisha tabia ya tume/msajili Sasa na ile tume ya wakoloni nyakati za uchaguzi.
 
Umeshawahi kuhudhuria mikutano ya tundu lissu hivi karibuni? inaonekana huna habari na kinachoendelea wewe. Tume ikiwa huru na ya haki lolote linawezekana.

juzi nmeskia anasema ongezeko la chakula sio maendeleo, daah nkasema apa bangi inahitajika kuwaelewa maaana anaongea pumba juu ya pumba! kama imefika hatua chakula nacho sio maendeleo basi walio upande wa lissu wa moyo mgumu sana
 
Kweli, wacha nichutame kama sehemu ya uungwana, maana jf sio chombo cha wahalifu, kina hadhi yake. Hata hivyo hali ilivyo sasa ya uchaguzi kuna mstari mwembamba sana unaotofautisha malalamiko dhidi ya TUME na Msajili kutoka kwa vyama vya upinzani. Malengo ya Msajili na Tume yana mwelekeo unaorandana dhidi ya vyama vya upinzani na chama tawala. Niliposikia kuwa hakuna hata mgombea mmoja aliyeenguliwa kugombea kutoka CCM Bara na Visiwani na hakuna mfanyakazi wa tume anayejisikia aibu kwa tukio kama hilo nikasema sasa hivi Tanzania inaelekea kubaya.

Hahahaaaa haya bwana! Ila Sidhani kama Tume na Msajili wanamalengo yaliyosawa.
 
Hivi ACT Wazalendo na CHADEMA wakikaidi huu upuuzi, NEC na Msajili wa vyama, watafanya nini? Kuna mahali wataenda kushtaki? Najua ACT na CHADEMA wana mahali pa kushtaki.
NEC inahusikaje hapo jamani. Najaribu kuwaelewesha lakini hamuelewi. Acheni ushabiki maandazi. Istoshe wenye chama chao nadhani watakua wameelewa.
 
Wananchi wanaomwelewa Lissu ni:
√ wafanya biashara waliokuwa hawalipi kodi;
√ wafanya biashara waliokuwa wskushirikiana na watumishi wa Serikali kuihujumu sasa nafasi hiyo sasa imezibwa. Pesa sasa inatumika kufanya shughuli za maendeleo;
√ watumishi wa Serikali waliokuwa wanawalipa mishahara na marupurupu mengine watumishi hewa;
√ watumishi wa Serikali waliokuwa na ajira kwa kutumia vyeti feki;
√ vijana nguvukazi walioshinda vijiweni wakipiga stori, kuvuta bangi na kucheza pool;
√ watu kama wewe ambao mnashabikia vitu msivyojua;
√ na kadharika
Mkuu hoja rahisi sana...unapotosha .
Wapo watu wengi tu hawapo katika makundi hayo na bado wanamuunga mkono TL .na wengine wapo sekta nyeti(siwezi kutaja humu)

Au labda ni hoja ya kujifariji!
 
Wananchi wanaomwelewa Lissu ni:
√ wafanya biashara waliokuwa hawalipi kodi;
√ wafanya biashara waliokuwa wskushirikiana na watumishi wa Serikali kuihujumu sasa nafasi hiyo sasa imezibwa. Pesa sasa inatumika kufanya shughuli za maendeleo;
√ watumishi wa Serikali waliokuwa wanawalipa mishahara na marupurupu mengine watumishi hewa;
√ watumishi wa Serikali waliokuwa na ajira kwa kutumia vyeti feki;
√ vijana nguvukazi walioshinda vijiweni wakipiga stori, kuvuta bangi na kucheza pool;
√ watu kama wewe ambao mnashabikia vitu msivyojua;
√ na kadharika
Hao vijana unaowasema vibaya wa vijiweni wanatokana na kutokuwa na ajira! Ambayo kwa namna moja ni Tatizo la Uongozi uliopo madarakani.
 
Tume inafanya kazi ya CCM, huu ni mwendelezo tu walianza na kuwajazia form wagombea wa CCM
Kwakua si muelewa basi ngoja nikuache. Mimi nikumusaidia tu kutofautisha baina ya Taasisi hizo mbili. TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI na MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA. Sasa maamuzi ya Msajili halafu mahakamani Unamwita Tume. Au kosa alitende CUF halafu malalamiko unayapeleka Chadema hapo unakua umepatia kweli au umeingia porini wewe na wenzako.
 
Ninachojiuliza ni je nec wanaathirikaje na wagombea kuungana mkono🤔🤔😎😎

Mbona wabunge na madiwani walikazana kununuliwa na ccm huku wakisema wanaunga mkono juhudi nec walikemea huu uchafu?
 
NEC inahusikaje hapo jamani. Najaribu kuwaelewesha lakini hamuelewi. Acheni ushabiki maandazi. Istoshe wenye chama chao nadhani watakua wameelewa.
Mbona jazba? Wewe ushabiki wako kinyesi vipi. Sawa NEC hawahusiki, mbona husemi msajili atashtaki wapi?
 
kweli kabisa, CCM iko madarakani kwa miaka 60 sasa, kama huko kijijini hawana hata maji ya kunywa mpaka leo unataka kuwashawishi na flyover moja iliyojengwa Dar es Salaam? kama wanaenda hospitali hakuna huduma unataka kuwashawishi na ndege ambazo hawajawahi sio kuipanda bali hata kuiona imetua ardhini? Unajuwa hebu tuacheni ushabiki wa vyama tuongelee hatima yetu.
Mnakosa hoja ya kuwashawishi wapiga kura kwa kuamini kuwa Magufuli akizushiwa, kwenye kampeni, tuhuma za matumuzi mabaya ya kodi za wananchi atachukiwa na wapiga kura.

Taratibu tuchambue aina ya wapiga kura:
1) Wasomi kindakindaki, wanajua maana na matokeo chanya ya kuwekeza kwenye vichocheo vya kukuza uchumi (economic drivers).
2) Asilimia zaidi ya 70 inayoishi vijijini kweli haijui maana ya ununuzi wa ndege, ujenzi wa flyovers, nk. Lakini hawa wakieleweshwa umuhimu wake kwa usafirishaji mazao yao au kuwaletea bidhaa muhimu kwa mahitaji yao, kwa haraka iwezekanavyo, watakuelewa.
3) Ujenzi wa hospitali, vituo vya afya na zahanati, si kipaumbele kwa jamii ndogo yenye uwezo wa kumudu gharama za afya kwenye huduma za afya binafsi. Kwa mwanakijiji ambaye alilazimika kufunga safari ndefu kufuata huduma hiyo, kumwambia ni upotevu wa kodi yao, hakika hakuelewi.
4) Ujenzi wa kiwanja cha ndege Chato, kwa Watanzania wasio wa huko, itakuwa vigumu kuelewa kama ni matumizi mazuri ya kodi yao. Kwa wakazi wa huko, aghalabu wanao uwanja wa ndege, kesho yumkini watautumia kwa usafiri na usafirishaji wa bidhaa zao kwa haraka.
5) Bei ya bidhaa za kilimo km korosho, kahawa kuteremka inakuwa nafuu kwa mnunuzi. Kwa mkulima ni hasara tu pale anaposhindwa kupata soko la uhakika kuweza kurejesha angalau gharama zake.

Mifano iko mingi, itoshe kusema, mchambuzi makini anaweza kubaini kundi gani lina turufu ya nani ataibuka mshindi.
 
Mnakosa hoja ya kuwashawishi wapiga kura kwa kuamini kuwa Magufuli akizushiwa, kwenye kampeni, tuhuma za matumuzi mabaya ya kodi za wananchi atachukiwa na wapiga kura.

Taratibu tuchambue aina ya wapiga kura:
1) Wasomi kindakindaki, wanajua maana na matokeo chanya ya kuwekeza kwenye vichocheo vya kukuza uchumi (economic drivers).
2) Asilimia zaidi ya 70 inayoishi vijijini kweli haijui maana ya ununuzi wa ndege, ujenzi wa flyovers, nk. Lakini hawa wakieleweshwa umuhimu wake kwa usafirishaji mazao yao au kuwaletea bidhaa muhimu kwa mahitaji yao, kwa haraka iwezekanavyo, watakuelewa.
3) Ujenzi wa hospitali, vituo vya afya na zahanati, si kipaumbele kwa jamii ndogo yenye uwezo wa kumudu gharama za afya kwenye huduma za afya binafsi. Kwa mwanakijiji ambaye alilazimika kufunga safari ndefu kufuata huduma hiyo, kumwambia ni upotevu wa kodi yao, hakika hakuelewi.
4) Ujenzi wa kiwanja cha ndege Chato, kwa Watanzania wasio wa huko, itakuwa vigumu kuelewa kama ni matumizi mazuri ya kodi yao. Kwa wakazi wa huko, aghalabu wanao uwanja wa ndege, kesho yumkini watautumia kwa usafiri na usafirishaji wa bidhaa zao kwa haraka.
5) Bei ya bidhaa za kilimo km korosho, kahawa kuteremka inakuwa nafuu kwa mnunuzi. Kwa mkulima ni hasara tu pale anaposhindwa kupata soko la uhakika kuweza kurejesha angalau gharama zake.

Mifano iko mingi, itoshe kusema, mchambuzi makini anaweza kubaini kundi gani lina turufu ya nani ataibuka mshindi.
Makaburu na wareno hawakufukuzwa kwasababu hawakujenga flyovers na viwanja vya ndege South Africa na Angola, Bali walifujuzwa kwasababu waliwanyima wananchi mahitaji ya msingi Kama chakula, elimu, haki ya kusikilizwa, kujieleza , na kujiamulia mambo yao. Basic needs should come first before the secondary and tertiary needs. Kwa miaka 60 CCM ilipaswa iwe imeshafuta shida za maji, umeme, hispitali, madawa na kilimo Cha jembe la mkono na kutegemea mvua. Ni aibu kwa chama kilichotawala kwa miaka 60 kutaka kisifiwe leo kwa kusambaza umeme, maji, hospitali, barabara.

CCM ilitakiwa Sasa hivi itafute sifa kwa kupeleka satellite yetu angani, kutengeneza magari, matrectors, madawa ya binadamu na mifugo, mitambo ya kuvunia mazao mashambani combine harvesters na misitu.

Lazima
 
Tume inabidi wajifunze mtoto mmoja akifanya makosa ukimwacha na mwingine kesho atafanya kubwa zaidi ,na utashindwa kumwonya. Hicho ndicho kinachotokea hivi sasa. Na lissu anatumia udhaifu wao huo Huo. Ni kama vile na wao tume wameathirika na spana za Lissu
 
Back
Top Bottom