Aisee, hii style ya ajabu sana. Kule TANROAD na TARURA kila mtumishi ni Eng. .....Wengine wameibuka eti Arch... Ajabu tu!!Kila kukicha TANZANIA haikosi vituko.
Tume ya madini tuambieni mtumishi jina kuanza na neno CPA, ni nini maana yake na kirefu chake ni nini.
Mfano ni huu hapa👇wa watumishi wa Tume ya Madini.
1. CPA. William E. Mtinya
Director, Corporate Services Department.
2. CPA. Elikana P. Buremo
Director, Internal Audit Unit.
3. CPA. Mwagule D. Ikunga
Manager, Finance and Accounts Section.
Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Charles Kichere , Huwa haitumii hizo initial, kwenu huko tume ya madini ni mabosi wa CAG?
Hii imetupa watanzania taharuki, na mambo ya kienda hivi , Kuna siku utumishi wa umma ,utakuwa ni kijiamulia kuchagua cheo cha kujiita.