Wa-TZ wenzangu, mimi ninachoona ni kuwa: Wakati wa uhai wa Mwalimu ilikuwa vigumu watu kuonesha vitendo vya udini na kuvishabikia kama ilivyo hivi sasa. Wa-Islam walikuwa kimyaaaa lakini hakika yake walikuwa hawakuridhika na mambo mengi ya Nyerere na serikali yao.
Hali halisi ya kutoridhika kwa wa-Islam kulijidhihirisha wakati wa rais m-Zanzibar alipotawala Tanzania. Agenda kubwa ilikuwa (1) Soko huria (2) Kuua Azimio la Arusha na (3) Kujenga u-Islam.
Wakati wa Mkapa (1) Kubinafsisha mashirika ya umma (2) Kubinafsisha (3) kubinafsisha ....
Kipindi cha Kikwete (1) Ufisadi (2) Uswahiba (3) Udini tena na (4) Matumizi ya vyombo vya dola kuumiza watu binafsi na vyama vya siasa
Kwa mtiririko huo, inaonesha kuwa:
(1) Tanzania inaachana na mshikamano wa kitaifa na hakuna dalili zozote za kuuhifadhi
(2) Tanzania inaelekea kuvunjika vipande viwili vya Tanganyika na Zanzibar (no body can stop this trend now)
(3) Uzalendo ni msamiati uliokufa na kupisha ufisadi. Mabadiliko hayo yatakuwa ya kudumu
(4) Suali la ulinganifu wa kidini litazidi kuwa kubwa na kwa sasa hakuna mtu wa kulikomesha.
Hali ya kutoridhika ya wa-Islam iliyokuwepo wakati wa awamu ya kwanza, inapelekea kila rais mu-Islam kuja na agenda ya kidini kwa wazi au kwa kificho. Sasa hivi Kikwete anakaribia kuondoka kwenye madaraka, huenda akatuachia tatizo kubwa asipokuwa mwangalifu.
Wa-Islam na wa-Kristo hawaaminiani kwa sasa. Sababu kubwa ni mbili ama tatu:
(1) Wa-Islam viongozi kwa wafuasi mara kadhaa wamesikika wakitoa malalamiko yao dhidi ya Nyerere, Kanisa Katoliki, na MOU na kadhalika.
Kutokana na hali hiyo, wa-Kristo wamekuwa ni watuhumiwa na hali hiyo imepelekea kuondowa hali ya udugu wa kitaifa na badala yake wanatizamana kama sisi na wao.
(2) Hali inayotokana na matendo ya wa-Islam katika sehemu zingine za dunia. Mfano mashambulizi ya Boko Haram dhidi ya wa-Kristo huko Nigeria, mashambulizi ya makanisa huko Zanzibar, Mwanza, kuuwawa kwa wachungaji wa ki-Kristo kule Arusha, matendo ya Al~Shabab kule Kenya, Uganda na sehem zingine.
Matendo hayo yamewafanya wa-Kristo kujiona kuwa vita dhidi yao ni vya kidini na ni vikubwa.
Makosa makubwa yanayosababisha hali hii ni pamoja na..
- wa-Islam kumdharau hayati baba wa taifa Mwalimu Nyerere aliyefanikiwa kutuunganisha na kutufanya sisi kuwa wamoja bila kujali dini, kabila na rangi zetu
- viongozi waliokuja baada ya Nyerere kutofuata sera, mtizamo na msimamo wa Mwalimu. Karibu wote wameshindwa kutumikia wananchi masikini na badala yake wameamua kutumikia familia zao, marafiki zao na ndugu zao.
- Tumekubali rushwa kutawala serikali, siasa, mahakama na bunge. Rushwa imefika hadi kanisani (ila sijuwi kama imefika misikitini).
Matokeo yake...
1] Elimu imeshuka. Sasa hivi imekuwa kawaida kusikia watoto wasiojuwa kusoma wala kuandika wakichaguliwa kujiunga secondary school
[2] Sasa hivi ni kawaida kusikia watoto wa secondary, au primary school wakifeli mitihani zaidi ya 50%-80%.
[3] Umeme hakuna lakini kuna makampuni yakilipwa pesa in terms of billions
[4] Gas imegunduliwa lakini haijaonesha contribution yoyote katika ukuaji wa uchumi. Inflation imepanda katika viwango vya kutisha. Sisi tunataka kujenga u-Kristo na u-Islam katika taifa la watu wajinga na masikini !!!
[5] Madini yana mikataba yenye siri. Madini yanatoroshwa. Polisi wanatumika kulinda wawekezaji na kuuwa wananchi! Sisi tunajenga u-Islam na u-Kristo. Taifa la watu wajinga wanaoibiwa maliasili zao, lakini wao wanataka kusali na kusali tu.!!!
[6] Univeristies zetu zimeshuka viwango. Shule zetu hazina maabara, na mitaala inabadilika kila kukicha .. walimu mishahara mkia wa mbuzi. Walimu wapo kwenye migomo ya kudumu...sisi tunajenga u-Kristo/u-Islam? Hospital zetu hazina dawa, x-rays ni mbovu, madaktari wameanza kugoma... wanainchi wanashabikia watawala wasio na njozi..Je, dini zitaleta dawa?
[7] Siasa sasa zimegeuka kuwa biashara (1) wafanya biashara wanakimbilia huko (2) ma-professor wanaingia kwenye siasa (3) wachungaji wamewacha makanisa yao wanakwenda kwenye siasa ...
Je, Tanzania inakwenda wapi? Tusipoangalia tutajikuta tupo kwenye hali ya Somalia. Nimekata tamaa kabisa...Yesu rudi haraka.