MchunguZI
JF-Expert Member
- Jun 14, 2008
- 4,009
- 2,171
Haya ndo matokeo ya kuhodhi kila nafasi ya kazi ipitie tume ya ajira utumishi. Ni kuanzia mhudumu hadi profesa!
Hivi karibuni baada ya utumishi kutangaza nafasi za kazi za aina hii, wengi tulitegemea watakusanya maombi na kuzipa taasisi husika kuendesha zoezi la usaili. Hali imekuwa kinyume na sasa hivi Utumishi wanajiandaa kuendesha usaili huo.
Taarifa niliyoipata toka chuo kikuu (UD), wamepelekewa barua toka utumishi eti chuo kitunge maswali na majibu kwa ajili ya nafasi walizoomba kuajili. Yaonekana hawana uwezo wa kusaili ngazi hizo za elimu sasa wanaifanya tume ya utumishi kama baraza la mitihani.
Ukisha shindwa kujua nini uulize muomba kazi, maoni yangu ni kwamba umeshindwa kumusaili muomba kazi. Na kwa hali tuliyo nayo lazima washindwe. Siamini kama mwalimu anayefaa atapatikana kwa maswali ya kuandikiwa halafu atumwe kwenda kufundisha chuoni baada ya kupitishwa kwa mtindo huo.
Kwa kuwa wanaendesha usaili kwa maswali na majibu yaliyotungwa hakika sasa tutakuwa na wallimu wabovu vyuoni na hata sekta zingine za serikali. Hatutaweza kukwepa uvujaji wa maswali (au mitihani) hayo.
Hata hivyo, lengo la utumishi kuhodhi mamulaka ya kuajiri ni nini? Nini wanakiondoa? Nini wanakiweka? Au ni haya mambo tunayoyasikia mitaani? Yaani ku-balance dini, kabila, ukanda, n.k.
Hivi karibuni baada ya utumishi kutangaza nafasi za kazi za aina hii, wengi tulitegemea watakusanya maombi na kuzipa taasisi husika kuendesha zoezi la usaili. Hali imekuwa kinyume na sasa hivi Utumishi wanajiandaa kuendesha usaili huo.
Taarifa niliyoipata toka chuo kikuu (UD), wamepelekewa barua toka utumishi eti chuo kitunge maswali na majibu kwa ajili ya nafasi walizoomba kuajili. Yaonekana hawana uwezo wa kusaili ngazi hizo za elimu sasa wanaifanya tume ya utumishi kama baraza la mitihani.
Ukisha shindwa kujua nini uulize muomba kazi, maoni yangu ni kwamba umeshindwa kumusaili muomba kazi. Na kwa hali tuliyo nayo lazima washindwe. Siamini kama mwalimu anayefaa atapatikana kwa maswali ya kuandikiwa halafu atumwe kwenda kufundisha chuoni baada ya kupitishwa kwa mtindo huo.
Kwa kuwa wanaendesha usaili kwa maswali na majibu yaliyotungwa hakika sasa tutakuwa na wallimu wabovu vyuoni na hata sekta zingine za serikali. Hatutaweza kukwepa uvujaji wa maswali (au mitihani) hayo.
Hata hivyo, lengo la utumishi kuhodhi mamulaka ya kuajiri ni nini? Nini wanakiondoa? Nini wanakiweka? Au ni haya mambo tunayoyasikia mitaani? Yaani ku-balance dini, kabila, ukanda, n.k.