Tume imeonyesha udhaifu mkubwa kutumia neno "tanzania bara"

OCTA

Member
Jul 6, 2011
5
24
Haiingii akilini kwamba wajumbe wa tume bado wana woga wa kutumia neno Tanganyika na wakajikuta wanalazimika kutumia neno Tanzania Bara. Huku wakijua kabisa kwamba huu muungano ni wa Tanganyika na Zanzibar. Ule woga wa enzi "zile" bado wanao, kwamba wataonekana wanataka kurudisha serikali ya Tanganyika, wakati kwa rasimu waliyoitoa IMESHARUDI.
Hiki ni kizazi kingine, huo woga wenu musituchanganye na sisi. Hatutaki kusikia hii hitu "Tanzania bara", hii ni TANGANYIKA na si vinginevyo. Kama mukitaka kutumia neno "Tanzania bara" badala ya "Tanganyika", kwa sababu hizo hizo, tumieni neno "Tanzania visiwani" badala ya "Zanzibar".

Na hapo mutajichanganya zaidi, sababu Tanzania visiwani ni pamoja na Mafia, na visiwa vingine....

Kabla hata hatujaijadili hiyo rasimu, tuwe very clear kwenye jina la nchi yetu ya TANGANYIKA...
 
labda jamaa wanataka tubaki na jina la 'tanzania' hata kama zanzibar wataamua kujitenga na kuondoka.
 
Back
Top Bottom