Tuliowahi kupewa suspension tukutane hapa

Tuliowahi kupewa suspension tukutane hapa

Suspension nyingine nilipata kizembe sana .
ILIKUWA HIVI:
Kuna demu nilikuwa nikipata kuongea nae kupitia simu kwa sababu shule yao inakatazwa simu basi hiyo siku naazimisha kwa kupiga msuli mpaka asubuhi sasa siku hiyo nimeongea nae nikajikuta mwamba nikachukua kitini cha Advanced Mathematics cha Necta za Nyuma kama zote nikaenda kuzisolve sasa nikajikuta narudi bwenini saa 11.30 alfajiri bichwa langu lilikuwa lime jam balaa na kesho ndo j3 Assemble ambayo na mkuu wa shule huonekana na mara nyingi wote hutakiwa kuonekana asubuhi hiyo parade.Bwana wee nikajiroga nilale kidogo hata li saa limoja khaa kumbe wenzangu wameshajiandaa wametoka wameenda assemble mida kama ya saa 1.45 wakaja walimu wanne wanaosifika kwa unoko pale shuleni kusweep madoja daa si wakanivuta shuka ghafla na kuanza kuniamsha si nikaamka na wenge langu nikaanza kuwatia mitusi ya nguoni kuja kuangalia vizuri kumbe ni walimu aisee nilikokotwa mpaka assemble nikiwa nimevaa surual truk na kesho yake barua.

Sent using Jamii Forums mobile app
We jamaa visa vyako vya ugomvi kinoma unaonekana ulikua mbavu shule

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Suspension nyingine nilipata kizembe sana .
ILIKUWA HIVI:
Kuna demu nilikuwa nikipata kuongea nae kupitia simu kwa sababu shule yao inakatazwa simu basi hiyo siku naazimisha kwa kupiga msuli mpaka asubuhi sasa siku hiyo nimeongea nae nikajikuta mwamba nikachukua kitini cha Advanced Mathematics cha Necta za Nyuma kama zote nikaenda kuzisolve sasa nikajikuta narudi bwenini saa 11.30 alfajiri bichwa langu lilikuwa lime jam balaa na kesho ndo j3 Assemble ambayo na mkuu wa shule huonekana na mara nyingi wote hutakiwa kuonekana asubuhi hiyo parade...
mkuu uwe na huruma. Usiku wooote huu mpk wife kashtuka akidhani naota kumbe wenge tu. Ni vile unatukana weeee halafu unashangaa uliyemtusi sio.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Heri ya mwaka mpya wadau. Nadhan tumeingia salama.

Niende kwenye mada, leo nimeamka kuna kisa nimekumbuka kilitokea nikiwa nasoma shule ya Secondary mkoa fulani Kanda ya Ziwa ambayo ilikua ni shule ya boarding. Nilikua na kampan ya washkaji kama wanne. Basi bana kama wengi mnavyojua shule za boarding jinsi maisha yake yalivyo kama jeshi kila kitu ni amri.

Sasa ili kulainisha maisha yawe angalau rahisi kuna mshkaji kati ya washkaj zangu alikua mtumiaji wa kuberi mzuri tu, kumbe na washkaji zangu wengne washaunga chama. Mimi nikajitahidi kukaza mwisho wa siku uzalendo ulinishinda nikajikuta naanza kutumia. Dah ujana bana basi ukawa ndo mwendo wa kuberi asubuhi mchana jioni.

Tulikua tunapeana zamu ya kununua mzigo kipindi hicho bei ilikua nadhan shilingi mia. Kuna mtu mmoja alikua kiongozi wa bweni af dini ilimshka kwel bas si akatuchoma kwa mwalimu wa nidham mi siku hyo sina hili wala lile niko kwenye pindi nashtukizwa naitwa kwenye office ya mwalimu wa nidhamu. Kuingia mara nawakuta wana wamepiga magoti ndani ya office hapo hapo.

Nikajua kimenuka kuberi imechacha, basi maswali kama vile magaidi mpaka ofisin kwa headmaster kalishwa kitimoto sana.mwisho wa siku ikapgwa kengele wanafunzi wote na walimu wote wakakusanyika sisi tuko mbele tumesimamia magoti,baada ya maelezo marefu kutoka kwa headmaster tukapgwa suspension ya wiki mbili na bakora sita sita kwa kila kichwa na tukirudi tuje na wazazi.

Hamna cku kichwa kimeniuma kama siku ile najiulza naenda home naanzaje kuwaambia kuwa nimekua suspended. palikua hakuna namna niliwaambia japo hzo wiki mbili zilikua chungu sana kwangu maana imani kwa wazee iliisha majina mengi niliitwa mara mvuta bangi.mbwia ugoro n.k. Siku tunarudi bado msala ulikua ni mkubwa maana baada ya vikao vya board kukaa na kutuhoji kengele ilipigwa tena kama kawaida wote wakakusanyika washkaji zangu wote wakapgwa chini ni mimi pekee ambae nilipewa nafasi ya kufanya mtihani wa mwisho nikitokea nyumbani,na hii ilitokea sabab kdg nilikua vizur darasan pia nilikua kiranja wa michezo kubwa zaidi sikuwahi kua na record yoyote mbaya.

Nashukuru mtihan nilifanya na mungu alisaidia nilitusua kwa kiwango ambacho sio kibaya sahivi niko na maisha yangu.

Nimeandika kiufupi lakn ni mengi yalitokea.
Njoo na wewe utushirikishe kisa chako,karibu
 
kuberi, gutka, tambuu, mjani, fegi, simu za vyooni, njuka kukatwa mikia, wizi wa magodoro, wiki dume, kuchenga walimu wa field, kuwa na funguo za kutosha ( kama 300 ) hz zinafungua tranker zote, nyumba za walimu mpaka kufuri za wanakiji mpaka kituo kidogo cha polisi...utemi ktk misosi wengine wanawekewa kipeto lakin kuna mchizi kichizi anajaza msosi ktk ndoo ya lita kumi na nyama kisado, matukio ya kuchoma moto! ah mambo ni mengi mno, ila mwisho wa siku unakuja kuishi mtaan maisha yanaendelea ya shule yanabaki shuleni
 
Wacha na mie niwashirikishe kisa changu. Suspension yangu nilipigwa nikiwa kidato cha tano katika moja ya shule kongwe ya serikali huko Kilimanjaro, kiufupi tuseme nlikua form five wa Kwanza kabisa kupigwa suspension, ishu ilikuwa hivi, mie nlikuwa na kawaida kama naripoti shule mpya huwa sibebi tranka na mazaga yote siku ya kwanza.

Hua nafika kwanza nasoma mazingira kwa muda af ntahamishia vitu vyangu vyote kadri siku zinavyozidi kwenda. Sasa niliripoti shule na mabegi madogo mawili, la mgongoni, na la kushika mkononi, yote nikawa nayatunza bwenini, class napanda na madaftari mkononi, lile begi la mgongoni nliweka boxer, vest, dawa ya meno, mswaki na diary, sasa kuna ijumaa moja nlienda kuomba ruhusa ili nkanunue mahitaji town. Nimepewa ruhusa nkaenda dorm chap nkachkua begi bila kutoa vitu. Wakati nataka kuvuka geti la shule kuna ticha mmoja akanisimamisha ili anikague..

Mara akaona Vest, boxer, t-shirt, diary, bukta, mswaki na dawa ya meno, duuuh ticha aka suspect kua natoroka shule kutokana vitu alivyonikuta navyo, na mbaya zaidi ilikua wikiendi, so walihisi naenda kula maisha town na mademu, moja Kwa moja akanipeleka ofisi ya nidhamu, aisee jamaa walinishambulia siku ile, na mbaya zaidi wakaguzi walikuwepo, na katika kukagua begi zaidi wakakuta simu, msala ukawa mkubwa zaidi.

Basi tulihangaishana pale mwishowe nikapigwa suspension ya wiki tatu, barua ilielezea makosa kibao.haha, hapo ndipo nilichoka zaidi, nilipewa mpaka kesi ya uvutaji bangi, Basi nikarudi maskani nikaongea na maza na mshua uzuri walielewa, suspension ilipoisha nikarudi skuli na maza, kesi ikaisha....
 
Heri ya mwaka mpya wadau. Nadhan tumeingia salama.

Niende kwenye mada, leo nimeamka kuna kisa nimekumbuka kilitokea nikiwa nasoma shule ya Secondary mkoa fulani Kanda ya Ziwa ambayo ilikua ni shule ya boarding. Nilikua na kampan ya washkaji kama wanne. Basi bana kama wengi mnavyojua shule za boarding jinsi maisha yake yalivyo kama jeshi kila kitu ni amri...
Pole saana mkuu naikumbuka kuberi ilikuwa kwenye pakiti ya kijani unaweka kama ugoro first time najaribu, si nikameza yale mate yenye kuberi.

Weeeeh kichwa kilizunguka balaa na nikaenda kulala nje imagine baridi la Monduli na bado jasho lilinitoka, ukawa mwanzo na mwisho kujaribu hio kiti

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hhahahaaaaaa! Hata Mimi ningekuwa mwl ningehic kuwa unatoroka
Wacha na mie niwashirikishe kisa changu. Suspension yangu nilipigwa nikiwa kidato cha tano katika moja ya shule kongwe ya serikali huko Kilimanjaro, kiufupi tuseme nlikua form five wa Kwanza kabisa kupigwa suspension,...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maxence Melo unganisha huu uzi
Na upi???
20200106_184746.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dingi aligoma kukupeleka maana tulio wengi hurudishwa shule na maza,
Wacha na mie niwashirikishe kisa changu. Suspension yangu nilipigwa nikiwa kidato cha tano katika moja ya shule kongwe ya serikali huko Kilimanjaro, kiufupi tuseme nlikua form five wa Kwanza kabisa kupigwa suspension, ishu ilikuwa hivi, mie nlikuwa na kawaida kama naripoti shule mpya huwa sibebi tranka na mazaga yote siku ya kwanza...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilipewa sunspension kwa kosa la kunuka ulanzi muda wa prep na mwalimu Juma Mbau pale Ulayasi Sec. Nilikana mashitaka kuwa kunuka ulanzi sio ushahidi kuwa nakunywa ulanzi kwa sababu mazingira tunayoishi tumezungukwa na vitindi vya ulanzi, hapo nikaonekana mjuaji.

Mwisho wa siku nikakubali kuwa ni kweli nakunywa ulanzi ila ni ule wa asubuhi na natumia kama kitafunio yaani nakunywa na mikate (ni kweli nilikuwa nafanya hivyo) kwa sababu kipindi kile chai sh 100 kikombe, na ulanzi sh 500 lita kumi.

Nikawa nataka kusamehewa ila bahati mbaya tena nilikuwa na simu mfukoni ambayo ikahalalisha makosa yote mawili.
 
Nilipewa sunspension kwa kosa la kunuka ulanzi muda wa prep na mwalimu Juma Mbau pale Ulayasi Sec. Nilikana mashitaka kuwa kunuka ulanzi sio ushahidi kuwa nakunywa ulanzi kwa sababu mazingira tunayoishi tumezungukwa na vitindi vya ulanzi, hapo nikaonekana mjuaji. Mwisho wa siku nikakubali kuwa ni kweli nakunywa ulanzi ila ni ule wa asubuhi na natumia kama kitafunio yaani nakunywa na mikate (ni kweli nilikuwa nafanya hivyo) kwa sababu kipindi kile chai sh 100 kikombe, na ulanzi sh 500 lita kumi.
Nikawa nataka kusamehewa ila bahati mbaya tena nilikuwa na simu mfukoni ambayo ikahalalisha makosa yote mawili.
Iringa-1

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dah umenikumbusha kitambo sana me nilipigwa suspension nikiwa form2 head master akasema niende kuchukua barua yangu nikagoma na nikawa naingia class kama kawa lakn barua ya suspension alikuja kuchukua rafiki yangu na kuipeleka hom nikiwa form4.

kwahyo mda wote huo toka form2 nilivyoipata hiyo suspension ilikuja kugundulika hom nikiwa form4 lakn mda wote nilikua natoka home naninaenda shule ikifika saa3 asubuh naingia mtaan kufanya mishe mishe lakn form4 nilikuja kutoboa
 
Dah umenikumbusha kitambo sana me nilipigwa suspension nikiwa form2 head master akasema niende kuchukua barua yangu nikagoma na nikawa naingia class kama kawa lakn barua ya suspension alikuja kuchukua rafiki yangu na kuipeleka hom nikiwa form4 kwahyo mda wote huo toka form2 nilivyoipata hiyo suspension ilikuja kugundulika hom nikiwa form4 lakn mda wote nilikua natoka home naninaenda shule ikifika saa3 asubuh naingia mtaan kufanya mishe mishe lakn form4 nilikuja kutoboa
Ulisoma Day ndomana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom