Tuliowahi kulala Sero/lock up kwa ujinga

Tuliowahi kulala Sero/lock up kwa ujinga

tehteh ilkua arusha bana nliingilia msafa wa first lady mama kikwete
nlkua natabia ya kuiba gari hom af napiga misele kiipindi io nko om nasubiria matokeo ya form4
nlsimamishwa na trafk nkaogopa,nkaliunga kumbe na msafara ndo unataka kuingia barabaran
nlshangaa nmeblokiwa mbele ile nashangashangaa kioo cha upande wa dereva kikavunjwa nkatolewa kuptia palepale dirshan mda uo nshapigwa ngumi ka milioni iv nkarushwa kwe defender nkalazwa chini polisi wakasimama juu yangu sjui nlzimia sjui nlkata network maana nliamka nko lockup na manundu ka30 iv nlkaa siku3 na hospital siku3 pia

mshua ilbidi anisamehe tuu na alkua mkali balaa
 
Maisha ya Ujana ni shida.
Miaka kadhaa iliyopita, rafiki yangu alichepuka kwenye Ndoa yake iliyokuwa changa kwa wakati huo, ambapo hakuonekana kwake kwa siku moja. Mkewe na baadhi ya nduguze walihangaika kumtafuta bila mafanikio. Kwa bahati nzuri au mbaya taarifa ya kutoonekana kwake haikuwa imefikishwa kituo cha Polisi. Hivyo jamaa baadaa ya kutoka kwenye uchepukaji wake alitutafuta baadhi ya marafiki zake ili tumsaidie namna ya kukabiliana na hatari iliyo mbele yake. Baada ya mashauriano ya muda mrefu, tukaamua kumtafuta rafiki yetu ambaye by then alikuwa ni OCCID wa eneo lile. Ikabidi jamaa yetu (mchepukaji), awekwe lock up ili kuonesha kuwa alikamatwa na Polisi waliokuwa doria siku iliyopita kwa kosa la kufanya vurugu mahali fulani.. To cut the story short ni kwamba mkewe ndiye aliyeenda kumuwekea dhamana na jamaa akatolewa lock up.
hahhhaaaaa
 
Kuna wakati polisi una burgain nao khsu hela
Watanza 50000/ mwishoni hadi buku 10 watachkua

Ova
Mkuu umenikumbusha mbali sana kuna siku nimeingia kwenye kumi na nane zao wazee wakakomaa wanataka million sita na hapo mwanaume Nina elfu themanini mfukoni ila tukabargain mpaka wakala elfu thelathini tu.
 
Bora ubaki nazo kuliko kutapeliwa asee...maana hiyo fedheha dooh!
Daah ...historia tamu kinyama

Wanaume wasafi, wazuri zuri ni vimeo kiwango cha lami

Hata akiwa mumeo ndani ni bure tuu

Namuona sista angu yanavyomkuta kisa HB
Hahahaha
Yaani bora nipambane na hali yangu kuliko hawa viumbe wanaume.
Ila sikomi tu.
Mpaka kieleweke
 
Naomba nisitaje majina,ila nikiwa kidato cha sita(6) mimi na wanangu wa utotoni mmoja alikua mtoto wa mkuu wa mkoa Dar maarufu sana na mwingine baba ake alikua Prof pale UD basi kwa wehu wetu yule swahiba angu mtoto wa Prof akaiba risasi kadhaa ambazo mshua wake alikua anatumia kuwindia tukagawana ili tuuze tupate sarafu za x-mass maana tulikua na mbwembwe za ujana hatari duh balaa likaanza yule mwana kapeleka biashara kwa mshua mmoja ambae ni anawinda sana kumbe mzee alikua cop kitambo na basi swahiba kuulizwa kama ana mzigo wa kutosha akatuunganisha na yule mzee cop ili wote tuuze haraka tukajikuta ubaoni pale O'bay alafu mbaya zaidi mkuu wa mkoa kaibuka akasema tunyooshwe kuliko maelezo maana hata Prof tulimuweka matatizoni ndio nikajua wale wana selo kule chini nashukuru mama zetu wakaja kumwaga chozi baada ya siku 5 ndio washua wakalegeza kamba hapo nimeonana na wahuni wangu mara moja kwenye kutoa maelezo ila tulitengwa ila hii ilikua ni mara yangu ya 3 kuingia nyavuni hizo za mwanzo sijawahi kujilamu mpaka kesho nilienda ngome kishujaa hata mshua alikuja kunitoa uku anatabasamu.
Mkuu pole sana
 
Asante my super wifi.
Wifi enzi zangu nilikuwa nadanga, Mungu na malaika wake tu ndio walikuwa mashahidi.
Ila nashukuru Mungu, tangu kaka yako anioe.....nimepunguza kudanga.
Asante, maana lockup si mchezo.

Lockup niliyokaa muda mrefu ni Stakishari, almost 12 days....dah!!!
Ila now nimekuwa, najua kujicontroll.
Pepo lile lisinirudie tena.
haaahaaaa sikuwez wifi yake mtu. uko wazi wifi ashindwe mwenyewe kukusemea kwa kakake
 
tehteh ilkua arusha bana nliingilia msafa wa first lady mama kikwete
nlkua natabia ya kuiba gari hom af napiga misele kiipindi io nko om nasubiria matokeo ya form4
nlsimamishwa na trafk nkaogopa,nkaliunga kumbe na msafara ndo unataka kuingia barabaran
nlshangaa nmeblokiwa mbele ile nashangashangaa kioo cha upande wa dereva kikavunjwa nkatolewa kuptia palepale dirshan mda uo nshapigwa ngumi ka milioni iv nkarushwa kwe defender nkalazwa chini polisi wakasimama juu yangu sjui nlzimia sjui nlkata network maana nliamka nko lockup na manundu ka30 iv nlkaa siku3 na hospital siku3 pia

mshua ilbidi anisamehe tuu na alkua mkali balaa
haaaahaaaaa pole sana
 
Ndugu yetu TRUE TANZANIAN, ninaomba uwendeleze simulizi ya ule ushuhuda wako. Umetueleza vizuri namna ulivyo ingia mtaani lakini hujatujuza namna ulivyotoka mtaani mpaka kufikia uwezo wa kuwa mahiri katika uandishi kama jinsi maandiko yako yanavyoonekana.

Tujulishe pia mpaka kufikia kuishi na mama wa kambo mama yako mzazi alikuwa wapi maana sisi kama vijana lakini pia ni wazazi hivyo tunajifunza mengi kupitia historia za watu kama nyinyi.
 
Niliingia mahabusu nusu siku Magomeni Polisi ishu ilikuwa hivi:-
Siku hiyo nilikuwa zangu manispaa Kinondoni nafunga data sheet kwani nilikuwa nahama wilaya kwenda wilaya ingine.
Nilivyomalizana na wadada wa masijala Ile nakata kona kuondoka nje kupitia pale jengo la mkuu wa wilaya Kinondoni nikakutana na mkaka smart tu, simjui.... akaniambia dada mambo, unajua muda mrefu nakufatilia tangu unaingia, yaonekana wewe mstaarabu na blah blah nyingiiiii.....at the end akaniomba tukapate lunch pamoja.
Nami kwa kuwa nilikuwa na njaa nikaona kijana yuko smart afu anaonekana mstaarabu ngoja tu niende ila nikamwambia tusiende mbali sana maana file langu limepelekwa kwa afisa utumishi, akasema sawa.
Basi tukatoka nje akaita teksi tukaingia na kusepa.
Tukaenda mpaka mitaa ya Kigogo cha wote kula.
Dereva taksi baada ya kulipwa alivyotaka kuondoka yule kaka akamwambia kaa na wewe ule.
Dereva akakaa na kuanza kula.
Basi ile tunakaribia kumaliza dereva na yule jamaa wakainuka kwenda msalani, jamaa yule smart nikamuona anarudi kisha akachukua funguo ya gari akaingia kwenye ile taksi peke yake akaiwasha na kusepa.
Mie nikasema kwa kuwa walienda wote msalani itakuwa kamuazima gari.
Dereva anarudi haoni gari wala yule jamaa.
Akaanza kuuliza yule bwana ako yuko wapi?
Nikamwambia mie yule simjui nimekutana nae tu Manispaa.
Afu si mlikuwa wote msalani, nikajua mmeenda kuongea umuazime gari.
Weeeee......yule dereva akasema we dada sikuelewi, utanieleza leo.
Mie yule simjui na wala sijamuona akiingia msalani.
Akaanza kujaza watu....watu walivyojaa akawaeleza kila kitu A to Z.
Mie najitahidi kujitetea ila watu hawaelewi somo.
Wengine wakasema sie majambazi wa magari na nionyeshe yule kaka alikoenda.
Jamani omba yasikukute.
Bili ya chakula haijalipwa, soda hazijalipwa na bado nishaundiwa zengwe.
Kila nikijaribu kujitetea naambiwa wewe dada jambazi, onyesha alipo mwizi mwenzio.
Nikwaambia jamani mie simjui, dereva taksi akaniambia mbona ndani ya gari ulikuwa unaongea nae asi if mnajuana, mie nikamueleza niliamua kumchangamkia tu.
Nikaanza kulia pale....nililia kwa uchungu wa kutuhumiwa jambo ambalo sijafanya.

Baada ya majadiliano ya kama dk 5, ghafla trafiki mmoja akaja mpaka pale, akauliza kulikoni ikabidi wamuelezee maana mie hata nguvu sikuwa nazo.
Baada ya trafiki kusikia vile akasema kuwa kapigiwa simu na trafiki mwenzie kuwa kuna taksi imetelekezwa mitaa ya Magomeni Mapipa baada ya kuishiwa mafuta.
Ikabidi mie, trafiki, wapambe na yule dereva twende Magomeni.
Kufika pale mapipa tukakuta ni ile ile taksi ila ndani hakuna mtu.
Nilipiga magoti na kupiga ishara ya msalaba katikati ya barabara.

Mara akaja mkaka tu akasema vipi mbona mmejaa hapa, tukasema tunamtaka mwenye gari hii, yule kaka akasema huyo dereva kaenda kununua mafuta kasema nimlindie gari yake.
Tukamuuliza yukoje akatutajia, yaani ni yule mwizi kabisa.
Askari akasema tumsubiri ila tutoke hapa barabarani ili hata akija asijue.
Basi tukatoka tukajificha.
Dk 5 yule kaka mwizi akaja na kidumu.
Ila anasogelea gari tu watu wakajitokeza akaachia kidumu akakimbia, akaanza kufukuzwa akaenda kukamatiwa kule mtaa wa Dosi.
Basi alipokamatwa akasema mie siko peke yangu niko na huyu dada.
Weeee.....nililoa sana na kuanza kulia.
Tukabebwa wote tukapelekwa Magomeni polisi.
Kufika pale nikalambwa vibao kama 4 na askari kwa usumbufu kuwa nimewasumbua kumbe najuana na mwizi.
Jamani nilikuwa nalia kama mtoto.

Siku zote mtumaini Mungu hakosi msaada.
Ghafla katika shift za askari pale, aliingia askari ambae namjua na ananijua, baada ya kunikuta pale akaniuliza kulikoni ndipo nikaanza kumueleza yaliyonikuta.
Ndipo yule askari akawasiliana na shemeji yangu ambae ni Afisa uhamiaji airport.

Baada ya kufika pale akasema huyu dada ni shemeji yangu na hana tabia hiyo, huyu kaka mwizi anamsingizia tu.
Basi shemeji wakakaa group na wenzake wakaanza kumuhoji yule mwizi.
At the end ikaja kugundulika kuwa kweli siko nae na wala simjui ila nilikutana nae tu katika harakati zangu za ujana.

Basi kesi ikaisha hapo, yule askari aliyenizaba makofi akanitaka radhi.
Shemeji akanibeba kwenye gari aliyokuja nayo akanishusha nyumbani ye akaelekea ofisini kwake.
Yule dereva akapewa gari yake na mwizi akachapwa makofi na mateke kisha akapelekwa Central.

Tangu siku hiyo:
1. Kama sikujui na ukijifanya kunichangamkia ujue utaishia kutukanwa

2. Ofa za wanaume walio smart, nimekoma tena nimekoma kabisa.

3. Ukinisalimia njiani na nikakuitikia ujue una bahati.
Ila All in All ule ulikuwa ni umalaya tu ambao sitakaa niusahau.
Nilijua nimeopoa mkaka smart kumbe kimeo na kuishia mahabusu.
Pole sana haikuwa umalaya ila ni utoto, Malaya hachagui wewe ulimuamini kutokana na muonekano wake, hata hivyo mtu hujifunza kutokana na makosa
 
Niliingia mahabusu nusu siku Magomeni Polisi ishu ilikuwa hivi:-
Siku hiyo nilikuwa zangu manispaa Kinondoni nafunga data sheet kwani nilikuwa nahama wilaya kwenda wilaya ingine.
Nilivyomalizana na wadada wa masijala Ile nakata kona kuondoka nje kupitia pale jengo la mkuu wa wilaya Kinondoni nikakutana na mkaka smart tu, simjui.... akaniambia dada mambo, unajua muda mrefu nakufatilia tangu unaingia, yaonekana wewe mstaarabu na blah blah nyingiiiii.....at the end akaniomba tukapate lunch pamoja.
Nami kwa kuwa nilikuwa na njaa nikaona kijana yuko smart afu anaonekana mstaarabu ngoja tu niende ila nikamwambia tusiende mbali sana maana file langu limepelekwa kwa afisa utumishi, akasema sawa.
Basi tukatoka nje akaita teksi tukaingia na kusepa.
Tukaenda mpaka mitaa ya Kigogo cha wote kula.
Dereva taksi baada ya kulipwa alivyotaka kuondoka yule kaka akamwambia kaa na wewe ule.
Dereva akakaa na kuanza kula.
Basi ile tunakaribia kumaliza dereva na yule jamaa wakainuka kwenda msalani, jamaa yule smart nikamuona anarudi kisha akachukua funguo ya gari akaingia kwenye ile taksi peke yake akaiwasha na kusepa.
Mie nikasema kwa kuwa walienda wote msalani itakuwa kamuazima gari.
Dereva anarudi haoni gari wala yule jamaa.
Akaanza kuuliza yule bwana ako yuko wapi?
Nikamwambia mie yule simjui nimekutana nae tu Manispaa.
Afu si mlikuwa wote msalani, nikajua mmeenda kuongea umuazime gari.
Weeeee......yule dereva akasema we dada sikuelewi, utanieleza leo.
Mie yule simjui na wala sijamuona akiingia msalani.
Akaanza kujaza watu....watu walivyojaa akawaeleza kila kitu A to Z.
Mie najitahidi kujitetea ila watu hawaelewi somo.
Wengine wakasema sie majambazi wa magari na nionyeshe yule kaka alikoenda.
Jamani omba yasikukute.
Bili ya chakula haijalipwa, soda hazijalipwa na bado nishaundiwa zengwe.
Kila nikijaribu kujitetea naambiwa wewe dada jambazi, onyesha alipo mwizi mwenzio.
Nikwaambia jamani mie simjui, dereva taksi akaniambia mbona ndani ya gari ulikuwa unaongea nae asi if mnajuana, mie nikamueleza niliamua kumchangamkia tu.
Nikaanza kulia pale....nililia kwa uchungu wa kutuhumiwa jambo ambalo sijafanya.

Baada ya majadiliano ya kama dk 5, ghafla trafiki mmoja akaja mpaka pale, akauliza kulikoni ikabidi wamuelezee maana mie hata nguvu sikuwa nazo.
Baada ya trafiki kusikia vile akasema kuwa kapigiwa simu na trafiki mwenzie kuwa kuna taksi imetelekezwa mitaa ya Magomeni Mapipa baada ya kuishiwa mafuta.
Ikabidi mie, trafiki, wapambe na yule dereva twende Magomeni.
Kufika pale mapipa tukakuta ni ile ile taksi ila ndani hakuna mtu.
Nilipiga magoti na kupiga ishara ya msalaba katikati ya barabara.

Mara akaja mkaka tu akasema vipi mbona mmejaa hapa, tukasema tunamtaka mwenye gari hii, yule kaka akasema huyo dereva kaenda kununua mafuta kasema nimlindie gari yake.
Tukamuuliza yukoje akatutajia, yaani ni yule mwizi kabisa.
Askari akasema tumsubiri ila tutoke hapa barabarani ili hata akija asijue.
Basi tukatoka tukajificha.
Dk 5 yule kaka mwizi akaja na kidumu.
Ila anasogelea gari tu watu wakajitokeza akaachia kidumu akakimbia, akaanza kufukuzwa akaenda kukamatiwa kule mtaa wa Dosi.
Basi alipokamatwa akasema mie siko peke yangu niko na huyu dada.
Weeee.....nililoa sana na kuanza kulia.
Tukabebwa wote tukapelekwa Magomeni polisi.
Kufika pale nikalambwa vibao kama 4 na askari kwa usumbufu kuwa nimewasumbua kumbe najuana na mwizi.
Jamani nilikuwa nalia kama mtoto.

Siku zote mtumaini Mungu hakosi msaada.
Ghafla katika shift za askari pale, aliingia askari ambae namjua na ananijua, baada ya kunikuta pale akaniuliza kulikoni ndipo nikaanza kumueleza yaliyonikuta.
Ndipo yule askari akawasiliana na shemeji yangu ambae ni Afisa uhamiaji airport.

Baada ya kufika pale akasema huyu dada ni shemeji yangu na hana tabia hiyo, huyu kaka mwizi anamsingizia tu.
Basi shemeji wakakaa group na wenzake wakaanza kumuhoji yule mwizi.
At the end ikaja kugundulika kuwa kweli siko nae na wala simjui ila nilikutana nae tu katika harakati zangu za ujana.

Basi kesi ikaisha hapo, yule askari aliyenizaba makofi akanitaka radhi.
Shemeji akanibeba kwenye gari aliyokuja nayo akanishusha nyumbani ye akaelekea ofisini kwake.
Yule dereva akapewa gari yake na mwizi akachapwa makofi na mateke kisha akapelekwa Central.

Tangu siku hiyo:
1. Kama sikujui na ukijifanya kunichangamkia ujue utaishia kutukanwa

2. Ofa za wanaume walio smart, nimekoma tena nimekoma kabisa.

3. Ukinisalimia njiani na nikakuitikia ujue una bahati.
Ila All in All ule ulikuwa ni umalaya tu ambao sitakaa niusahau.
Nilijua nimeopoa mkaka smart kumbe kimeo na kuishia mahabusu.
Doh aisee Pole sana ila story yako imetufundisha kitu na sie wengine
 
Back
Top Bottom