Haha, hatari! Exacly miaka 11 nyuma, shule moja maarufu kwa kutoboa. Ilikuwa sherehe yangu ya graduation kabla ya final pepa A-level (graduation ilikuwa tunafanya jmosi, pepa inaanza j3). Sasa bwana, baada ya sherehe ilipofika jioni mimi na washkaji tukatoroka tukaenda chimbo kupata moja mbili kama njia ya kusherekea milestone ya graduation. Hatukuwa wazoefu, tukalewa fasta, akili zikasema tununue kreti ya bia tukamalizie gambe shuleni!! Hee, kufika shuleni tukaaza vurumai, tukavunja vioo vya madarasa then tukaingia darasa mojawapo kuendelea kula vitu. Dakika kumi nyingi, askari Hawa hapa (wale wale waliokuja kulinda mitihani, maana iliwasili jioni Hiyo)!! Wakanidaka na jamaa zangu, tukafungwa kamba moja kwa moja tukaongoza centro. Maticha wakataka tufukuzwe, mkuu wa Kituo akasema tufanye mitihani tukitokea selo, (nahisi alijua tungefeli tu). Basi bana, wiki tatu naamkia selo, naenda kupiga pepa, narudi selo! Hakuna kusoma wala kujikumbushia nini, noma saana. Duh, baada ya mtihani wa mwisho nikatoka, hapo nadaiwa pesa ya uharibifu wa shule. Sina kitu mfukoni, home hawajui lolote, ikabidi niuze kagodoro kangu na tranka, nikabembeleza wakapokea pesa. Nikapanda basi siku Hiyo Hiyo kwenda home, sikubeba kitu zaidi ya nguo zangu nilizovaa!! Matokeo kutoka nina division one nzuri, nikaenda kusoma medicine chuo maarufu mjini. Leo mimi ni Daktari wako unayemtegemea zaidi, ila yale matukio siwezi sahau!