Tuliowahi kulala Sero/lock up kwa ujinga

Tuliowahi kulala Sero/lock up kwa ujinga

nilikuwa na mahusiano na afande mmoja, nikajifanya pendapenda nikatoka na frend wake akipo gundua akanipa kesi ya kuiba laptop na simu kwa afande flani.

Nimekaa sero kama 6hrs akaja nikuta afande mmoja jamaa yangu, kunitoa hawezi maana njagu mwenzake ndo kaniweka. akaenda muomba msamaha akakubali. ila kwa sharti tuendelee mahusiano sikuwa na ujanja nikakubali.
 
nilikuwa na mahusiano na afande mmoja, nikajifanya pendapenda nikatoka na frend wake akipo gundua akanipa kesi ya kuiba laptop na simu kwa afande flani.

Nimekaa sero kama 6hrs akaja nikuta afande mmoja jamaa yangu, kunitoa hawezi maana njagu mwenzake ndo kaniweka. akaenda muomba msamaha akakubali. ila kwa sharti tuendelee mahusiano sikuwa na ujanja nikakubali.
Mmmh! Una miaka mingp mkuu samahn lkn
 
Enzi hizo tunauza sim azam take away pale Kuna sim nlipewa na fundi mmoja pale anaitwa yahaya mitaa ILE,akikopa nkaiuze nkaichkua nkaipeleka central police Kuuza Kuna poti mmoja alikuwa ananisumbua sana kutaka sim kuipeleka kumbe Ilikuwa ya jamaa yake polisi yule alikuwa anaitwa koba kabanda wacha aninganganie hadi kuniweka selo chini kule...
Ushkaji uliwekwa kando hapo ...nlijipeleka mwenyewe Yaani

Ova
Anaitwa Koba Kimanga, jamaa ni askari maarufu pale central na aliwahi kua bondia enzi zake
 
kuna fala mmoja nilikua na bifu nae nikataka kumgonga na gari,akaenda kureport police,wakaja wakanidaka .wakaniweka lock up kama lisaa limoja hivi,baadae wakaja kugundua kumbe na mimi ni mtoto wa poti mwenzao,wakanambia sasa muda wote huo mbona hujatoa hata ishara kama wewe dingi yako ni mwenzetu...nikatolewa nikasepa zangu,ila nimegundua walioko lock up wengi wana vijikesi vya kijinga jinga tu,mara huyu kamtukana mama mwenye nyumba mara mwingine kamkata vibao hawara wake. kesi za za kupotezeana muda tu
 
daaah pabaya mno halafu ishu inayokera zaidi ni giza nene...mtu anakojoa kwa kuestimate location ya ndoo mkojo mwingi unaishia chini na mwisho wa siku mnaishia kuulalia...yaani unakaa unahesabu tu masaa pakuche.ndo utajua kuna jogoo anawika saa tisa usiku we ukadhani ni saa kumi na mbili...
 
Anaitwa Koba Kimanga, jamaa ni askari maarufu pale central na aliwahi kua bondia enzi zake
MIMI ananijua vilivyo nlimsumbua sana enzi hizo sema Mpaka leo Mwana sana alafu anashangaaa watu tumekuwa raia wema maana enzi hizo Ilikuwa shidaaaa

Ova
Dalisalama sasa hivi pakoje.......Pazurieeeeeeeeeeeee..........!!!!!! kuna siku nitakuja huko.....kuja Kunywa CHAI....................

Kawaida tu!enzi za kuishaaa watu tuliwenda mbeleee n'a tukaja kurudi tena
Yahaya ndiyo alikuwa fundi mkuu wa simu mitaa ya posta enzi hizoooo
Wakati huo unauza simu azam n'a salamanda ....najua Kuna watoto humu salamanda hawajaikutaaaa

Ova
 
Niliingia mahabusu nusu siku Magomeni Polisi ishu ilikuwa hivi:-
Siku hiyo nilikuwa zangu manispaa Kinondoni nafunga data sheet kwani nilikuwa nahama wilaya kwenda wilaya ingine.
Nilivyomalizana na wadada wa masijala Ile nakata kona kuondoka nje kupitia pale jengo la mkuu wa wilaya Kinondoni nikakutana na mkaka smart tu, simjui.... akaniambia dada mambo, unajua muda mrefu nakufatilia tangu unaingia, yaonekana wewe mstaarabu na blah blah nyingiiiii.....at the end akaniomba tukapate lunch pamoja.
Nami kwa kuwa nilikuwa na njaa nikaona kijana yuko smart afu anaonekana mstaarabu ngoja tu niende ila nikamwambia tusiende mbali sana maana file langu limepelekwa kwa afisa utumishi, akasema sawa.
Basi tukatoka nje akaita teksi tukaingia na kusepa.
Tukaenda mpaka mitaa ya Kigogo cha wote kula.
Dereva taksi baada ya kulipwa alivyotaka kuondoka yule kaka akamwambia kaa na wewe ule.
Dereva akakaa na kuanza kula.
Basi ile tunakaribia kumaliza dereva na yule jamaa wakainuka kwenda msalani, jamaa yule smart nikamuona anarudi kisha akachukua funguo ya gari akaingia kwenye ile taksi peke yake akaiwasha na kusepa.
Mie nikasema kwa kuwa walienda wote msalani itakuwa kamuazima gari.
Dereva anarudi haoni gari wala yule jamaa.
Akaanza kuuliza yule bwana ako yuko wapi?
Nikamwambia mie yule simjui nimekutana nae tu Manispaa.
Afu si mlikuwa wote msalani, nikajua mmeenda kuongea umuazime gari.
Weeeee......yule dereva akasema we dada sikuelewi, utanieleza leo.
Mie yule simjui na wala sijamuona akiingia msalani.
Akaanza kujaza watu....watu walivyojaa akawaeleza kila kitu A to Z.
Mie najitahidi kujitetea ila watu hawaelewi somo.
Wengine wakasema sie majambazi wa magari na nionyeshe yule kaka alikoenda.
Jamani omba yasikukute.
Bili ya chakula haijalipwa, soda hazijalipwa na bado nishaundiwa zengwe.
Kila nikijaribu kujitetea naambiwa wewe dada jambazi, onyesha alipo mwizi mwenzio.
Nikwaambia jamani mie simjui, dereva taksi akaniambia mbona ndani ya gari ulikuwa unaongea nae asi if mnajuana, mie nikamueleza niliamua kumchangamkia tu.
Nikaanza kulia pale....nililia kwa uchungu wa kutuhumiwa jambo ambalo sijafanya.

Baada ya majadiliano ya kama dk 5, ghafla trafiki mmoja akaja mpaka pale, akauliza kulikoni ikabidi wamuelezee maana mie hata nguvu sikuwa nazo.
Baada ya trafiki kusikia vile akasema kuwa kapigiwa simu na trafiki mwenzie kuwa kuna taksi imetelekezwa mitaa ya Magomeni Mapipa baada ya kuishiwa mafuta.
Ikabidi mie, trafiki, wapambe na yule dereva twende Magomeni.
Kufika pale mapipa tukakuta ni ile ile taksi ila ndani hakuna mtu.
Nilipiga magoti na kupiga ishara ya msalaba katikati ya barabara.

Mara akaja mkaka tu akasema vipi mbona mmejaa hapa, tukasema tunamtaka mwenye gari hii, yule kaka akasema huyo dereva kaenda kununua mafuta kasema nimlindie gari yake.
Tukamuuliza yukoje akatutajia, yaani ni yule mwizi kabisa.
Askari akasema tumsubiri ila tutoke hapa barabarani ili hata akija asijue.
Basi tukatoka tukajificha.
Dk 5 yule kaka mwizi akaja na kidumu.
Ila anasogelea gari tu watu wakajitokeza akaachia kidumu akakimbia, akaanza kufukuzwa akaenda kukamatiwa kule mtaa wa Dosi.
Basi alipokamatwa akasema mie siko peke yangu niko na huyu dada.
Weeee.....nililoa sana na kuanza kulia.
Tukabebwa wote tukapelekwa Magomeni polisi.
Kufika pale nikalambwa vibao kama 4 na askari kwa usumbufu kuwa nimewasumbua kumbe najuana na mwizi.
Jamani nilikuwa nalia kama mtoto.

Siku zote mtumaini Mungu hakosi msaada.
Ghafla katika shift za askari pale, aliingia askari ambae namjua na ananijua, baada ya kunikuta pale akaniuliza kulikoni ndipo nikaanza kumueleza yaliyonikuta.
Ndipo yule askari akawasiliana na shemeji yangu ambae ni Afisa uhamiaji airport.

Baada ya kufika pale akasema huyu dada ni shemeji yangu na hana tabia hiyo, huyu kaka mwizi anamsingizia tu.
Basi shemeji wakakaa group na wenzake wakaanza kumuhoji yule mwizi.
At the end ikaja kugundulika kuwa kweli siko nae na wala simjui ila nilikutana nae tu katika harakati zangu za ujana.

Basi kesi ikaisha hapo, yule askari aliyenizaba makofi akanitaka radhi.
Shemeji akanibeba kwenye gari aliyokuja nayo akanishusha nyumbani ye akaelekea ofisini kwake.
Yule dereva akapewa gari yake na mwizi akachapwa makofi na mateke kisha akapelekwa Central.

Tangu siku hiyo:
1. Kama sikujui na ukijifanya kunichangamkia ujue utaishia kutukanwa

2. Ofa za wanaume walio smart, nimekoma tena nimekoma kabisa.

3. Ukinisalimia njiani na nikakuitikia ujue una bahati.
Ila All in All ule ulikuwa ni umalaya tu ambao sitakaa niusahau.
Nilijua nimeopoa mkaka smart kumbe kimeo na kuishia mahabusu.
 
Back
Top Bottom