carnte
JF-Expert Member
- Aug 8, 2017
- 362
- 425
Sitakuja kuisahau siku ile niliamka asubuhi nikiwa sina chochote, bahati mbaya ndugu mmoja akanipigia simu na kuniambia maneno ya dharau sana.
Nilikasirika sana bahati mbaya mimi ni kati ya wale ambao hukimbilia pombe nikivurugwa, sikuwa na pesa mfukoni ila kuna mtu alikuwa anitumie pesa yangu baadae, nikaondoka nikaenda kwenye pub moja hivi nikaweka simu bond nikaanza kutupia vitu mpaka nikatosheka.
Yule mtu hakutuma pesa, kesho yake nikaamka na hangover nikasema nikacheki simu na pesa labda itakuwa imetumwa kufika sikumkuta yule jamaa, nikakuta wafanyakazi wake, ujinga nikaanza kupakia vitu tena.
Sasa kwenye kulipa, nikawaambia nitakuja kulipa jamaa ana simu yangu, bili inasoma elfu 15, duu bahati mbaya yule mmiliki akatokea, akaniuliza pesa yangu nikawa najiuma uma duh!
Kumbe anamshikaji wake askari, dakika sifuri jamaa alikuja akanichukua hadi lock up, aibu kwanza ni Mara ya kwanza, jamaa hakunipa hata room nikachukue hiyo pesa nililala huko sio pazuri kabisa.
Kesho yake jamaa alienishtaki akaja na simu yangu bahati pesa ilikua imeingia
kilichonitia hofu ni ndugu kama wangejua nimelala huko, liliisha bila kujua na waliponiuliza niliwaambia tuliharibikiwa gari.
Sitakuja kusahau hili
Nilikasirika sana bahati mbaya mimi ni kati ya wale ambao hukimbilia pombe nikivurugwa, sikuwa na pesa mfukoni ila kuna mtu alikuwa anitumie pesa yangu baadae, nikaondoka nikaenda kwenye pub moja hivi nikaweka simu bond nikaanza kutupia vitu mpaka nikatosheka.
Yule mtu hakutuma pesa, kesho yake nikaamka na hangover nikasema nikacheki simu na pesa labda itakuwa imetumwa kufika sikumkuta yule jamaa, nikakuta wafanyakazi wake, ujinga nikaanza kupakia vitu tena.
Sasa kwenye kulipa, nikawaambia nitakuja kulipa jamaa ana simu yangu, bili inasoma elfu 15, duu bahati mbaya yule mmiliki akatokea, akaniuliza pesa yangu nikawa najiuma uma duh!
Kumbe anamshikaji wake askari, dakika sifuri jamaa alikuja akanichukua hadi lock up, aibu kwanza ni Mara ya kwanza, jamaa hakunipa hata room nikachukue hiyo pesa nililala huko sio pazuri kabisa.
Kesho yake jamaa alienishtaki akaja na simu yangu bahati pesa ilikua imeingia
kilichonitia hofu ni ndugu kama wangejua nimelala huko, liliisha bila kujua na waliponiuliza niliwaambia tuliharibikiwa gari.
Sitakuja kusahau hili
