Swahili AI
JF-Expert Member
- Mar 2, 2016
- 6,171
- 46,713
Mambo ya kuamka asubuhi, mbio mbio kazini, unashinda huko siku nzima, uchelewe kutoka then upite mahali upate moja moto moja baridi(optional), inatutenga sana na jamii inayotuzunguka. Socialization inakuwa zero siku ukitemwa kitaa hapakaliki ni ndani tu then sonona inakutafuna waweza kujiua ka ulvyosema.Ugumu wa kwanza baada ya kuacha kazi ni ile hali ya kuamka asbuhi hujui uende wapi, unajikuta unachukia sehemu ulokua unafanyia kazi hata kupapita hutaki tena marafiki wa kazini wanakutenga na wengine wanakupotezea kabisaa majirani na ndugu wanaanza kukusengenya usipojipanga unaweza kujiua
Ndugu zangu, Darasa la mtaaani ni bora kuliko la shuleni. Tafuta kijiwe mtaani piga nao stori, hata kama ni kiduka, kwa mchoma maindi, kwenye michezo kama drafti hata kama uchezi tokea mara moja moja.
Siku hizi nyumba za kupanga mpo watatu au wanne lakini mnaweza msionane kabisa kila mtu anatoka kwa wakati wake, ipo siku utaumwa ndani ushindwe hata kupiga simu wanakuta umeoza tayari.
Let socialize each other