Tuliotembea umbali mrefu kwa miguu kwa sababu yoyote ile tukutane hapa

Jua la dar unalijua vizuri mkuu?

labda upige hizo ruti usiku ila dar hii

Jua litakukwmisha na ukijikaza hata siku 1

kesho utaamka umekua mweusi kama tairi la boxa
Na kwa Dar hali ya Hewa ndio tatizo kubwa.Isingekuwa joto watu wangetembea sana kwa mguu.Unakuta mtu anatoka Mapipa anaenda Fire au Muhimbili au Kariakoo anapanda gari ile sehemu ni ya kucharaza tu mguu
 
Wakati nipo Mdogo tuliwahi Kaa Kijiji kimoja cha Ikondo (Kipo Lupembe) Mkoani Njombe.Sasa Kuna watu toka vijiji vya Ukalawa Kanikelele Lupembe walikuwa wanaenda Mgololo kununua Mapipa ambayo walikuwa wanaenda kutumia kupika Pombe za Kienyeji,ule umbali sijui ni km ngapi lkn angalau ni parefu jamaa walikuwa wanachoka sio mchezo
 
Tuliokulia vijijini kutembea umbali mrefu wala siyo story.

Moja kufuata huduma za kijamii kama hospital, maduka etc

Mbili,kwenda kusaga mahindi vijiji jirani vyenye machine ya diesel.

Kwenda minadani kuuza mazao kilometa kadhaa ili kupata kipata cha familia
Bila kusahau kwenda mashamba ya kilimo yaliyopo mpakani na kenya hasa kwa wachaga, umbali makadirio km 50 na zaidi kwa baadhi yao.
 
Tulikuwa JKT Bulombora. 2ic Major Mzena akaitisha mkutano wa Kikosi kizima jioni moja. Tumefika Conference Hall kikosi kizima kombania zote, tumekaa tumetulia na kombati zetu safi, baada ya roll call, tumekaa chini. Muda Afande Mzena akaingia. Afande RSM Mbilinyi baada ya kumsalimia kwa saluti ya ukakamavu sana, akaanza kumpa maelezo,... AFANDE MBELE YAKO KUNA WAPIGANAJI SO AND SO,... NA SERVICE MEN SO AND SO (RSM akataja idadi).....kumbe 2iC akaona idadi ya watu haiko sawa kulingana na takwimu za kikosi, imekuwa ndogo, akauliza WANGAPI? RSM akarudia tena kutaja idadi aliyoitaja mwanzo. Pale pale Afande Mzena,Aakaamuru kwa kusema "kesho asubuhi saa 12 hapa! Tukaanza kugawanwa tena,.. foleni, foleni,....na hatimaye tukatawanyishwa tukarudi kwenye mahanga yetu. Kesho yake saa 12 asubuhi kikosi kizima safari hii kwa idadi kamili ya watu, kikawa kipo tena mahali pale. Afande Mzena wala hakuonekana tena, akaja msaidizi wake CI Major Mtekele. Alipoingia tu conference room, akatamka maneno haya ROOT MUCH MPAKA NSIMBO, MIMI NITAKUJA NA PAJERO LANGU NINAWAFUATA! I see, Nsimbo iko km si chini ya 40 kutoka Bulombora JKT. Zoezi likabadilika ghafula, ikawa ni root much!. Nikajaribu kutengeneza mbinu niingie kwenye kundi la wapishi, ikashindikana, nikaamua kutoroka kupitia mahanga ya wasichana SERENGETI, nikakutana na msichana anakimbia amevurumushwa huko, ananiambia makanyaga huko kuna MP. I see, tulitembea root much mpaka Nsimbo kwenda na kurudi, km zaidi ya 80! I will never forget that day. Jeshini nilikuwa na tecnik za kukwepa visanga na kwa akili nyingi sana, lakini zote siku hiyo zilikwama!
Hivi jamani hili neno ni root much au ni route xxxx... yaani hakuna hata wa kunirekebisha! Kiranga uko wapi? Halafu kuna siku niliwahi kuandika packed badala ya parked na sijamsikia mtu akinirekebisha
 
Vyombo vya usafili vingi hv hafu ntembee mguu huwa nawapiga fix nyingi sana za kisomi kisomi nahakikisha konda na dereva wote wapo mkononi sijawahi kutembea umbali mrefu labda nafanya mazoezi ,ila kama sina nauli hata kama ni km 200 ntapanda gali tu mbele mbelee tutaelewana.
 
Kimara hadi ubungo. Kulikuwa na foleni kutokea mbezi hadi ubungo siku hiyo usiku wa saa mbili. Nauli haitoshi kupanda pikipiki, na siku hiyo walikuwa wanatwanga watu bei kubwa sana.. Ikabidi nikanyage. Ilikuwa 2012 au 2011.
 
Kuna siku nilienda kumsalimia bibi . Wakati wa kwenda nilipanda gari, nilishuka kituoni nikatembea kuanzia saa 9alasiri hadi saa 12 na nusu jioni(Sijui ni km ngapi)
Kesho yake tukaondoka saa 12 nasu asubuhi tukafika saa 4 asubuhi
Pia kuna siku nilitembea kutoka mnazi mmoja hadi ukonga banana. Ilikuwa 1987
Shikamoo
 
Zaidi ya 120km, nilitoka wilaya ya Rungwe (saivi Busokelo) eneo linaitwa Rwangwa mpaka Mbeya mjini..bahati mbaya sijui cha shortcut wala nini kwahyo nanyoka tu na barabara. Nilitoka kule saa kumi na moja alfajiri mpaka saa mbili usiku ndo naingia Mbeya mjini, form three kipindi hicho. Nilitoroka home nikaenda kule wakawa hawanitaki kwahyo kunisema kila Siku, nikashundwa kuvumilia
 
Back
Top Bottom