Tuliopata ajira kimasihara tukutane hapa

Tuliopata ajira kimasihara tukutane hapa

Boeing787-8

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2018
Posts
1,202
Reaction score
1,296
Basi bwana baada ya kumaliza chuo sina mia sina kitu, nkaenda kujibanza kwa sister maana alikuwa ameolewa na wamejenga.

Ni vigumu kukaa kwa sister wako aliyendoani lakini sister wangu na mumewe tuliishi vizuri saaana. Basi nilimaliza chuo mwezi wa 7, Basi nkaanza application za kazi, nilkataa katu katu kuomba kazi physically maofisini.

Yaani nilikuwa naomba kazi online (via email) n.k, kufika mwezi wa 10 nilikuwa nimefanya application 14, na hakuna niliyoitwa hata interview.

Basi mwez wa 11 nikapitia email zangu nkaomba feedback ya application yangu ya kujitolea kwenye shirika moja la Wamarekani, nilipata contacts zote za Director General wa hilo shirika mtandaoni Basi nkamu-email kimasihara, ikumbukwe barua ya kuomba kujitolea nili-type kwenye simu kimasihara na ilipangwa vibaya, Basi yule boss akarespond email yangu akasema nafasi ikipatikana watanicheki.

Tarehe 24/12 napigiwa simu na manager nkafanye interview, yaani huo mwaka sikujua vya Christmas, nilipanda gari kutoka Dar Hadi mkoani nkapiga interview, tulikuwa 4 me nkatoboa nkapata kazi.

Director alipotoka Marekani kuja Bongo, alisema we chalii una confidence hatari, uliwezaje kupata contacts zangu, nkamuambia nilizipata kimasihara.

N.B Hivyo niliandika barua kimasihara ya kuomba volunteering, nkaandika emails ya kuulizia my application kimasihara, Sina hili Wala lile nkaitwa interview kimasihara, na nkaajiriwa mazima badala ya voluteering, so nkaajiriwa kimasihara.

Wale mliopata ajira kimasihara ebu shusha nondo.
 
Mi nakumbuka nilienda kwenye interview na ka lower second kangu, nje nikakuta mabishoo wanajitapa ooh mimi na First class yangu lazima nitoboe.

Tulipoingia kwenye interview niliwagaragaza vibaya sana, confidence ilikuwa juu sana. Aisee mpaka napata lile shavu sitosahau.
 
Mi nakumbuka nilienda kwenye interview na ka lower second kangu, nje nikakuta mabishoo wanajitapa ooh mimi na First class yangu lazima nitoboe.

Tulipoingia kwenye interview niliwagaragaza vibaya sana, confidence ilikuwa juu sana. Aisee mpaka napata lile shavu sitosahau.
Ndo hvy wabongo tunatanguliza mbele makaratasi
 
Sawa, nami nilikuwa nimelala tu usiku saa 7 Kuna giza Nene Mvua inanyesha daah mwewe kaninyea kwenye kiganja cha mkono baada ya week nikapata kazi looh Mungu ahsante ila[emoji24][emoji24][emoji24][emoji3525][emoji3525][emoji3525]
Mmmm
 
Sawa, nami nilikuwa nimelala tu usiku saa 7 Kuna giza Nene Mvua inanyesha daah mwewe kaninyea kwenye kiganja cha mkono baada ya week nikapata kazi looh Mungu ahsante ila[emoji24][emoji24][emoji24][emoji3525][emoji3525][emoji3525]
Ila....
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Hata usiendelee nimeshaelewa

Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom