Tulioonewa na kufungwa na serikali

Tulioonewa na kufungwa na serikali

Mkuu;
Pole sana sana kwa masahibu yaliyo kupata. Kitu kimoja tu nadhani kinaweza kukusaidia. Samehe, sahau tu. Ukishindana nao utajiongezea mateso na mwisho utakata tamaa na kuangamia. Kama ulivyo sema, Umepoteza vingi kwa kesi ya kuonewa. Mshukuru Mungu kuwa, umetoka salama na nguvu zako.
Najua moja tu; Mungu alikuwepo, ameona na usidhani hataacha kuwatenda. Kisasi ni mali ya Mungu usijaribu kulipiza. Pia usife moyo. Endelea kuwaelimisha watu kuhusu mabadiliko. Lema aliwekwa ndani miezi mingapi, mbona bado anahubiri mabadiliko?? Wapo wasio amini kuwa ipo siku yatatokea but definitely it will come.
Well said mkuu
 
Cdm razma isemwe na wote wanao onyesha kuwa kinyume na akili mgando za ccm na kwakuwa ndicho chama kinachowafanya ccm kutokulala ukitaka kujua hilo kutana na hao waliokukamata harafu sema mm ni cdm kama ni giza watakuuwa na siku zote mkweli hapendeki
 
Miaka miwili iliyopita yalinipata haya kwa sababu ya kusupport UKAWA.
Sikuwahi kuwa mwanachama wa chama chochote cha kisiasa ila niliamini katika MABADILIKO YA UKAWA

Nilijitahidi sana kuwaelimisha watu juu ya uhitaji wa mabadiliko Pasipo kuvunja sheria.

Kilichotokea siku moja usiku tuliingiliwa na watu watano wakiwa na silaha na sare za kipolisi, wakatukamata kimyakimya nikiwa na rafiki yangu tuliekuwa tukiishi naye hapa jijini mwanza.

Walianza kwa kusema wamepigiwa simu na wananchi wema kuwa tunatengeneza kemikali.

Wakaingia ndani kwa nguvu hawakukuta kiashiria chochote cha hicho walichodai kemikali.

Ajabu wakatupakia kwenye deffender mpaka Central Police Mwanza,
Cha ajabu kingine walikataa tusimjulishe mtu yeyote hata ndugu juu ya ukamataji wetu.Tuliwekwa sero week nzima.

Siku ya tano usiku alikuja mkuu wa kituo na kuuliza "wale vijana wa chadema wako wapi?" Tulikaa kimya kwani tulijua labda miongoni tuliopo sero kuna wanachadema wamekamatwa, la hasha! kumbe alikua akimaanisha ni sisi.

Akatuita kwa majina, tulishangaa sana, tukamuuliza mbona wakati mnatukamata mlisema tunatengeneza kemikali? Sasa mmetubatiza jina vijana wa chadema, pia kuwa chadema ni kosa kisheria? Tulimuuliza kwa upole tukitaka msaada wa kutoka sero.

Akatujibu "Mbowe yupo nyumbani kalala usingizi nyie mpo huku sero mnaliwa na mbu" tulishangaa kwani maswali na majibu hayaendani.Tulirudishwa sero.

Asubuhi yake tulikua na hasira sana tukaanza kupiga kelele angalau ndg zetu wajulishwe kuwa tupo kituoni, baadae wakatupeleka mahakamani na wakaja na vibobo vimejaa liquid flani wakidai ni ushahidi wameupata.

Case iliendelea baada ya kupewa dhamana na mahakama na hivi karibuni mahakama ikatuachia maana hakuna case ya kujibu.

Najua si sisi yaliyotupata haya, kama na wewe ulipatwa na haya share nasi.

Maisha yanaendelea niliathirika sana kisaikolojia, nilipoteza fedha nyingi katika case na kilichoniuma sikuwahi kuwa mfuasi wa CHADEMA ila niliunga mkono mabadiliko
Nimerudi nyuma kimaisha na kimaendeleo kwani mnajua case ni ugonjwa mbaya sana.

Nipo namuomba mungu anipe nafasi niweze kulipa kisasi kabla sijafa na kupotea kabisa.

Mtanisamehe siyo mzuri kudeliver story.


Kafungue kesi ya Fidia dhidi ya Mkuu wa Kituo kwa Mashitaka ya nia Mbaya (Malicious Prosecution), unamshitaki in his personal capacity. Kama kweli mmesingiziwa na hamna connection yoyote na shughuli za kemikali, mnaweza kuset precedent nzuri sana.
 
Dada, unataka nini kwani? Unadhani mwenye cheti feki kama wewe unaweza hata kudiriki kupiga simu kwenye jumuiya ya wasomi kama hii? Endelea kujifurahisha nyuma ya ki-ID chako feki kama kilivyo cheti chako. Ulizia kuhusu mimi kabla hujaropoka Dada.
Sasa Nikuulize Kwa Kipi? Au unataka nitaje na Hicho ki net salary chako? Piga Kazi Acha Mipasho na Siasa Mama wewe.

Kutwa nzima Kuiponda serikali huku mnachukua Mishahara.
 
Sasa Nikuulize Kwa Kipi? Au unataka nitaje na Hicho ki net salary chako? Piga Kazi Acha Mipasho na Siasa Mama wewe.

Kutwa nzima Kuiponda serikali huku mnachukua Mishahara.
Mkuu, kama unajiamini usijifiche nyuma ya ID feki. Jitokeze tujenge hoja. Unathibitisha uoga na unafiki wako kwa ki-ID chako feki dada. Tafuta wengine wa kuwazoea. Si mimi. Mimi ni mtu huru na nitaendelea kuwa huru. Vyama, kama ulichomo cha CCM, vina wenyewe hivyo. Mtapata magonjwa ya moyo kwa kutetea mali za watu.

Fahamu kuwa, sijawahi kuwa muoga wala mnafiki kama wewe wa kusema au kutenda kwa staha ninachokiamini. Hayo ya kuponda pondeni na ya kusifia sifieni nyinyi wanachama wa vyama. Usipofanya hivyo, utakufa njaa. Ni aibu mdada kama wewe kutegemea porojo katika kuishi.
 
Walianza kwa kusema wamepigiwa simu na wananchi wema kuwa tunatengeneza kemikali.

Wakaingia ndani kwa nguvu hawakukuta kiashiria chochote cha hicho walichodai kemikali.

Ajabu wakatupakia kwenye deffender mpaka Central Police Mwanza,
Cha ajabu kingine walikataa tusimjulishe mtu yeyote hata ndugu juu ya ukamataji wetu.Tuliwekwa sero week nzima.

Ni kweli mlikuwa mnatengeneza kemikali. Kemikali mliyokuwa mnatengeneza ni ile yenye manufaa kwa taifa. Hamasa ya kuleta mabadiliko ndio hiyo kemikali mliyokuwa mnatengeneza. Dawa ya mbu kama X-pel ni kemikali ambayo inamanufaa makubwa kwa afya ya binadamu kwani umkinga na ugonjwa wa malaria na mengine yaenezwayo na mbu.

Pia kuleta mada hii hapa ni muendelezo wa kusambaza hiyo kemikali mlikwisha tengeneza, na itaua tu mbu, na kulinda afya za wengine.

Ni vyema mngeweka ushahidi wa vielelezo vya kesi yetu kwa kuondoa taarifa ambazo zitawatambulisha moja kwa moja.
 
Mkuu, kama unajiamini usijifiche nyuma ya ID feki. Jitokeze tujenge hoja. Unathibitisha uoga na unafiki wako kwa ki-ID chako feki dada. Tafuta wengine wa kuwazoea. Si mimi. Mimi ni mtu huru na nitaendelea kuwa huru. Vyama, kama ulichomo cha CCM, vina wenyewe hivyo. Mtapata magonjwa ya moyo kwa kutetea mali za watu.

Fahamu kuwa, sijawahi kuwa muoga wala mnafiki kama wewe wa kusema au kutenda kwa staha ninachokiamini. Hayo ya kuponda pondeni na ya kusifia sifieni nyinyi wanachama wa vyama. Usipofanya hivyo, utakufa njaa. Ni aibu mdada kama wewe kutegemea porojo katika kuishi.


Huyo yuko kwenye deiz zake ndiyo maana anahangaika sana.
 
Sasa kuna umuhimu gani wa kuwa na vyama vingi si wafute tu tujue moja nasema hivi [HASHTAG]#tusipangiane[/HASHTAG]

Marehemu Nyerere alisema 'wakubwa wanataka vyama vingi' hivyo hakukuwa na namna ya kukwepa vyama vingi.
 
Pole mkuu, usilipe kisasi hata siku moja, shetani hajawahi kumshinda Mungu hata mara moja.
Ni vema wakalipa kisasi kwanza , halafu baadaye watubu .

Unajua , siku zote hawa polisi , tunawaambia kwamba kuna maisha baada ya huo upolisi wenu ,

Kwa mfano , Omary Mahita baada ya kustaafu alidhalilishwa mahakamani kwa kosa la kumtelekeza house girl wake baada ya kumtundika mimba , haikufahamika kama alimbaka au walikubaliana .
 
Back
Top Bottom