Mkuu;
Pole sana sana kwa masahibu yaliyo kupata. Kitu kimoja tu nadhani kinaweza kukusaidia. Samehe, sahau tu. Ukishindana nao utajiongezea mateso na mwisho utakata tamaa na kuangamia. Kama ulivyo sema, Umepoteza vingi kwa kesi ya kuonewa. Mshukuru Mungu kuwa, umetoka salama na nguvu zako.
Najua moja tu; Mungu alikuwepo, ameona na usidhani hataacha kuwatenda. Kisasi ni mali ya Mungu usijaribu kulipiza. Pia usife moyo. Endelea kuwaelimisha watu kuhusu mabadiliko. Lema aliwekwa ndani miezi mingapi, mbona bado anahubiri mabadiliko?? Wapo wasio amini kuwa ipo siku yatatokea but definitely it will come.