Umesema vyema. Wakisema ni uzungu waseme tu ila swala la shosti kuja bila taarifa kukiwa hamna emergency sikubaliani nalo kabisaaaaa.
Je kama mnaishi chumba na sebule na mume anataka apumzike sebleni kwake unataka pia awapishe akajifungie chumbani? Kama ni dharura nadhani hata shosti ataelewa tu nikimtoa tukazungumze nje hahahaha
Nashangaa hakuna anayekataza ndugu zake wa kike + house girls kufika kwake; kwani hao hawawezi kumbeba mumeo? Eeh kweli ndoa wito mweeh
huo ushost huo ndo siutakiHuwezi kuwa mbali na marafikiwa kuja kukutembelea, ila kuna ule ushost wa kuvuka mipaka kuna mkoa mmoja shaost akija akipiga hodi sauti itakotokea anakuja huko huko hata kama ni chumbani sasa hayo mazoea gani
Sent using Jamii Forums mobile app
Ndiyo waje kukutembelea shost wangu mme akija asalimie nakupita chumbani kwa wiki mara 4 unasahau hata kumpokea mme kwa mziko alikokuja nakoHivi ukiwa na ndoa unahitaji mashosti wa kazi gani? Maana mimi binafsi sina huo muda wa kumgaia shosti, Alfajiri nipo barabarani kwenda kusaudia kunyanyua kipato cha familia saa 10 jioni narejea nikiwa too stressed na kitu pekee ninachohitaji ni faraja ya stress zangu sio hadithi za shosti
Sent using Jamii Forums mobile app
Mimi nilichomwelewa mtoa uzi ni ile kila mara mashost nyumbani, unajua kuna urafiki ambao hata akija nyumbani mwenyewe hata mme ana furahia ugeni, ila kuna wale mara waimba kwaya gani, mara sijui mashost wanini wa group la what's app hiyo ndiyo kaisema, sizani kama rafiki naye ana mme atakuwa kutwa kusalimia marafiki zake na kuacha mmewe nyumbaniMi huwa naamini hivi!
Sitatembelea kwa shosti si kwa kuwa nahofia mumewe kunitamani, NATAMANIWA na WANAUME HATA HAWANIJUI SURA!
Sitazuia shosti kunitembelea nyumbani kwangu kwa hofu ya mume wangu kumtamani, KAMA MIMI NATAMANIWA NA WASIO NIJUA SURA NA AMBAO NI WAUME ZA WATU!,wangu ANA NINI CHA TOFAUTI AMBACHO WA WENZANGU HAWANA!
WATAKUJA NA HAWATAKUJA kwa sababu zingine!, SIO KUHOFIA MUME ATAINGIA KWENYE MAHUSIANO NAO!
hii ni mimi!
Mwenye mme hajui? Si wameshibana huwezi jua kabisa hapo alifanywa mjinga balaa, kuna mama mmoja mastafu wa mmewe walikuwa wakiishi sehemu 1 na huyo mdada mmewe ni rafiki wa huyo mama kufa na kuzikana kumbe wanakulana huyo mama alikuja kujua baada ya huyo shemeji yake kufariki na walivyokuwa na upendo huwezi gundua hata kidogkTena ni mwiko mkubwa ............nimewahi kushuhudia mtu kabeba kama anaenda kujinyonga kisa mumewe kalala na rafiki yake wa kufa na kupona kwa kipindi cha miaka 11
Sent using Jamii Forums mobile app
Haka mie sitaki kifo cha hivyo bora nisiye mjua hata nikipambana huku yataisha , ila unayemwani huwa inauma sanaUtashangaa the dearest and nearest ndiye akakutenda.
Marafiki kweli wapo, tena mpaka waume wanajua wake zetu ni marafiki, lakini sio ile kumba kumba unamwamini mtu kuzidi hata mama yako, kuna mwaka nikiwa binti mdogo nilijifunza wamama marafiki mpaka kuvaa sare wananunuliana kumbe mmoja anamzunguka mwezie kilichofuata visasi walikulana wote wote yule mchozi ilibidi aombe uhamishona watu tunapenda kweli kutafuta wachawi huku tunasahau kuwa tunajiroga wenyewe,.
Mie mwenyewe siendi kwa mtu bila sababu ya msingi, hatujaonana siku nyingi sawa,huo ushost huo ndo siutaki
Heaven hapa nimegundua kuna kundi la walioko kwenye mahusiano wanalinganisha na ndoa
Kuna sehemu kwenye maisha marafiki wana sehemu yake, kuna biashara nyingine tumezianzisha na marafiki,
Japokuwa siyo marafiki mpaka kuingilia uhuru wako.
Hivi unaanzaje Kumlinda mume!!
Ambaye saa nyingine ni mtu mzima kaka yako kabisa!
Unajiwekeza kwenye uzungu wa kila mtu na maisha yake!
Hawa ndo wale uhofia hata ndugu kufika kwao anawaza anatembea na mumewe!
Hapana kuolewa sio mwisho wa maisha, mume ni muhimu na marafiki ni muhimu pia. Maybe chumbani ila kwangu rafiki yangu atakuja tu labd aaamue mwenyewe.
Haya mafisi utajifanya kujitenga na rafiki zako kumbe anakula house girl humo humo ndani na majirani.
Birds of the same feathers........
Kwajiyo ninawaamini rafiki zangu, likitokea la kutokea ni mipango ya shetani tu kama ilivyo kwa mengine.
Teh wenginie ndo hata ukienda kwa ndugu, unaambiwa Kabisa hakuna kuvaa nguo za aina fulani na fulani, utamtega mume wangu; anazivaa tu mama mjengo. Sasa unajiuliza huko barabarani/kazini na duniani huwa unamfumba macho mumeo asione vimini na vijeans/vitight? Huyo mume wa kuchungwa hivyo ni mume au mfano wa mume? Ukicheza kidogo kichaa cha ndoa kitakupata
Ndoa zimekuwa kama utumwa kwa baadhi ya watu
Unakuta mtu anajitenga na jamii kabisa ili kumridhisha mwenza wake!!
Mtu anafanya mambo ya kumuumiza ili kumridhisha mwenza!
Ndoa siyo gunia la misumari
Hapana jamani, sio kwa userious huo. Utayafanya maish ayawe magumu bila sababu za msingi.No wonder you are my mommy.
Kuna watu ndoa wanachukulia kama ndo kukutana na Mungu uso kwa uso, ndo ushamaliza maisha sasa. Kama ulikubali kuolewa na gumegume ila ukajipa moyo utamchunga, basi you will surely make a career kwenye ulinzi. Ndo wale ukipiga tu simu kwa mumewe unapokelewa na matusi hadi udate. Na watu wa hivi hawakawiagi kuwa vichaa, nani huwa anachunga na kugombana na watu hovyo?
Teh wenginie ndo hata ukienda kwa ndugu, unaambiwa Kabisa hakuna kuvaa nguo za aina fulani na fulani, utamtega mume wangu; anazivaa tu mama mjengo. Sasa unajiuliza huko barabarani/kazini na duniani huwa unamfumba macho mumeo asione vimini na vijeans/vitight? Huyo mume wa kuchungwa hivyo ni mume au mfano wa mume? Ukicheza kidogo kichaa cha ndoa kitakupata