Tuliambiwa tusile firigisi

Tuliambiwa tusile firigisi

Ngurubhe

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2014
Posts
1,840
Reaction score
1,049
Dungu zangu,nimeona tu niwarudishe nyuma.kidogo kule tuliko toka. Japo kuna watu bado wanaishi katika hili;
Embu taja baadhi ya vitu ambavyo vilikuwa vinaaminika kama miiko(taboos) aidha kwa nia nzuri au vinginevyo kwenu,na maana yake kulingana na utamaduni wenu.
kwa mfano;
kwetu sisi ilikuwa mwiko.
1.Kula paja la kuku
2.kula firigisi
3.Kunawa kabla ya wakubwa kabla na baada ya kula.
4.kumluka mwenzio mguu au akiwa amelala iliaminika kama ana magonjwa anakuambukiza
6.Hatukuruhusiwa kusimama pembeni au karbu na mwenzio alie kaa ati unamnyonya damu.
7.mama mjamzito hakuruhusiwa kula mayayai ati angemharbu mtoto
Mengne yalikuwa ni haya;
8.mkono ukiwasha(jicho kucheza shemu ya kope) eti utapata hela siku hio.
9.ukijikwaa kuna mtu anakusema vibaya(unatetwa) ulikotoka.
10.mtu mzima akilala akajikojolea eti mtapata taarifa za msiba.
11.jogoo akiwika jioni(mbwa kulia kwa makundi na vilio vya mda mrefu) eti kuna bibi au babu atakufa hapo kitaa(kijijini)
12.jua kuzungukwa na upinde kuna mchawi kafa hivyo anakuwa anajadiliwa na kusomewa hukumu..haya mim naamini ni baadhi tu,embu tuone kwenu pia mliaminishwa nini na wazee wetu wa zamani!
 
Hahahahahaha,umetisha kiongozi,bt ile iman kwamba ;
ukiwashwa miguu utapata viatu,mtoto akifagia mida ya jioni bac kuna mgeni atakuja.
 
Jicho kucheza utapata mgeni sio pesa, mvua inanyesha huku jua likiwaka(simba anazaa) ukikojoa njiani inabidi upake mkojo kwny kitovu unless watu wakiruka ule mkojo mama yako atakufa. Huruhusiwi kuchukua nyama wakati mnakula kabla ya mkubwa hajachukua... Baadhi ya miti hairuhusiwi kutumika km kuni unless mvua haitanyesha mwaka huo,
 
Watu wa zamani walikuwa na hekima sana hebu tuanze na hayo uliyosema
.walizui watoto kula paja,firigisi ililenga kudhibiti ulafi kwa watoto.

.Kumruka mwenzio mguu kwamba kama ana magonjwa atakuambukiza walilenga kuepuka ajali maana unaweza kuruka ukashindwa ukamuangukia ukaumia au ukamumiza.

mama kuzuiwa kula mayai eti mtoto atamharibu au hataota nywele waliogopa mama atazaa mtoto mkubwa na angejifungua kwa shida.

Mkono ukiwasha eti utapata hela walikuwa wanamtibu kisaikolojia badala ya kuwaza sana juu ya tatizo.

ukijikwaa kuna mtu amekusema vibaya kulilenga kuepuka kuwasema wengine vibaya kwani wangesababisha hatari kwa mwingine
.
mtu akilala akajikojolea kuwa atapata habari mbaya walilenga kuwatisha vikojozi waache mchezo wao.

Mbwa kulia makundi kuashiria mabaya hiyo ni kweli mbwa hutoa taarifa maana wanaona wachawi,majini ndiyo maana kwa mtu wa majini au mchawi si rahisi kukuta mbwa.

jua kuzungukwa na upinde kuwa mchawi kafa anapewa hukumu ililenga kuonyesha kuwa uchawi ni kazi mbaya na siku moja itawagharimu hukumu.
 
Hapo kwenye 12: kwenu kila MTU ni mchawi!!!!!????
 
Hapo kwenye 12: kwenu kila MTU ni mchawi!!!!!????

Neno "kuna mchawi" kafa limejitosheleza halijazungumzuia idadi ya wachawi mkuu au wewe umeishia kuelewa hapo?,after all these were the bilieves at my locality,is your time to list at least some frm yours
 
1. Ukimruka mtu inabidi umruke kwa mara nyingine tena sababu atakuwa mfupi

2. Mtoto mchanga anapatikana baharini
 
Hahahahahaha,umetisha kiongozi,bt ile iman kwamba ;
ukiwashwa miguu utapata viatu,mtoto akifagia mida ya jioni bac kuna mgeni atakuja.
Ukifagia nyumba ucku na kuzoa uchafu unafukuza wageni
jicho likicheza utapata mkosi
 
Ile mtoto akiwa na kwikwi unamwekea kipande cha uzi kwenye
paji la uso ina uhusiano na kukata kwikwi ya mtoto?
 
Ukiwashwa mikono katikati ya viganja
Wakushoto = utatoa hela

Wakulia = utapokea hela
Sasa ukiwasha wakulia unamwita mtu anaandika hela utakayo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom