Spika Dkt. Tulia: Rais mimi ndio Mbunge wa Mbeya Mjini, Wananchi wameniambia Wanakuunga mkono Uwekezaji wa Bandari!

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,791
218,420


Spika Dr. Tulia amesema anaowawakilisha yaani wananchi wote wa Mbeya Mjini wanaunga mkono Uwekezaji wa Bandari.

Dr. Tulia amesema Mkoa wa Mbeya ni wakulima hivyo Uwekezaji wa Bandari utasaidia Mazao yao kufika kwenye Masoko kwa haraka.

Nanukuu
Baada ya kuitaja Bandari, maneno mengi yametoka huku Mbeya, nataka niseme hivi... Mimi ndiye mbunge wa hapa Mbeya Mjini na ni mwakilishi wa wananchi hawa walio wengi hapa. Kama mwakilishi wao, sisi wanambeya mimi kama mwakilishi wao tumekaa wameniambia wanakuunga mkono Rais kwenye uwekezaji ambao unafanyika kwenye bandari ya Dar es Salaam.

Na katika kukuunga mkono kwenye uwekezaji ambao Serikali inawekeza, wanakuunga mkono kwenye kutafuta wawekezaji wengine kuja kuboresha bandari ya Dar es Salaam ili mazao yanayotoka Nyanda za Juu Kusini yaweze kuwahi masoko ya nje.

---
Hili ni dhahiri kwamba Tulia Ackson ameamua kumdanganya Mh Rais kwa lengo la kumpotosha ili ajipatie umaarufu.

Kabla ya kuendelea hebu tuangalie maana halisi ya Uongo kama ilivyoelezwa kwenye kamusi ya kiswahili

Sasa kauli hii ambayo ametoa Tulia Ackson bila uoga mbele ya kiongozi wa Nchi maana yake nini? Kamshirikisha Mwana Mbeya yupi ikiwa sisi watu wa Mbeya hatutaki Mkataba huo?

Hivi kwanini hawa viongozi wanatudharau kiasi hiki , Tufanyeje ili tuheshimike ?
 
Screenshot 2023-08-08 161642.png

Spika Dr. Tulia amesema anaowawakilisha yaani wananchi wote wa Mbeya Mjini wanaunga mkono Uwekezaji wa Bandari.

Dr. Tulia amesema Mkoa wa Mbeya ni wakulima hivyo Uwekezaji wa Bandari utasaidia Mazao yao kufika kwenye Masoko kwa haraka.

Source: Eatv
 
Sio mbeya tu, hataukukwetu tunahitaji kuwa na bandari yenye ufanisi kuliko ilivyo Sasa.

Spika awemkweli uongo hausaidiikitu, watu wasicho taka ni aina ya mkataba wenyewe nasio uwekezaji.

Hatuutaki mkataba wa ainaile, full stop.
 
Spika Dr Tulia PhD amesema anaowawakilisha yaani Wananchi wote wa Mbeya Mjini wanaunga mkono Uwekezaji wa Bandari

Dr Tulia amesema Mkoa wa Mbeya ni Wakulima hivyo Uwekezaji wa Bandari utasaidia Mazao yao kufika Kwenye Masoko kwa haraka

Source: Eatv
Mbona tuliambiwa chawa wamepigwa marufuku Bwashe? Huyu chawa Tulia Akson ametokea wapi?
 
Sio mbeya tu, hataukukwetu tunahitaji kuwa na bandari yenye ufanisi kuliko ilivyo Sasa.

Spika awemkweli uongo hausaidiikitu, watu wasicho taka ni aina ya mkataba wenyewe nasio uwekezaji.

Hatuutaki mkataba wa ainaile, full stop.
Huyu Dada anasali kweli?
 
Back
Top Bottom