Rogie
JF-Expert Member
- Nov 22, 2010
- 7,601
- 6,723
Mkuu unampata Nongwa?Hivi alikuwa Kazima au Uyui?Loooh...Yuko wapi yule demu ati?
Nampata sana juzi tu nimeonana nae, alikuwa Kazima mkuu.
Mkuu unampata Nongwa?Hivi alikuwa Kazima au Uyui?Loooh...Yuko wapi yule demu ati?
Ayaaaaa Rogie hatari snaa yule mtoto...Kaolewa?anaishi wapi nowdays??Nampata sana juzi tu nimeonana nae, alikuwa Kazima mkuu.
Eeeeee bwana wewe,hebu achana na hii story yako ya kahawa miaka nenda rudi,unatujazia kurasa,kumbusha watu mambo ya maendeleo na dini,sio kila kukichwa kuongelea wehu na majmbazi ya zamani Tabora,eboooo.Miaka ya 80's mwanzoni nilipata kuishi Tabora Mjini,baadae nikaja kusoma Tabora Boys miaka ya 90's....leo nimekumbuka maisha ya Tabora,Ujio wa Baba Mtakatifu,enzi za ukuu wa Mkoa Ndugu Gama....Timu ya mpira ya Milambo chini ya akina Job Ayoub "kwasakwasa",Quresh Ufunguo,Dadi Phares,Hamad Mwinyimkuu,Abas Mchemba na Bubu fulani alikuwa na mashuti sana wengine siwakumbuki Matajili wa wakati huo ni matajili wa mbao wakiitwa "Digala",kuna jamaa alikuwa tajili wa mbao mitaa ya Kiyungi karibu na Filter akiitwa Fifi(sijui kama yu hai)...mitaa ya ng'ambo mtaa wa Rehani alikuwepo Mavyombo,Msabaha...!kulikuwa na kina Said Kindamba,Waarabu wa Kwihara na Mrema wa Cheyo!...Miaka hiyo Tabora ilisifika kwa kuwa na Majambazi hatari,wengi wakitokea mitaa ya Ng'ambo..kuna jambazi mmoja walimkata mguu ili aache kuiba akawa anatembea na gongo(nimemsahau jina),Vichaa(wehu) wa kutosha na maarufu kama Athumani Nuna,Super Tall,Aman n.k...Mitaa ya wajanja ilikuwa National na Cheyo!!Misosi kama ugali muhogo,makopa,mawese na ngazi...Vipi nani wa Tabora anipe update za leo?mda sijafika Chemichemi,Gongoni,Bachu,Kanyenye,Kiloleni,Isevya,K'koo,Mwanza Road na Ipuli....Wapi vijana wa enzi hizo wa Mboka Manyema?
Baaasi hayo tu,umemaliza?,au kahawa imekwisha?Ukiwa unaenda kiloleni kupitia chekeni au checkline ya kiloleni na rufita clab kuna mzee alikuwa anaitwa Papaa Wemba alimuuzia msukuma Msikiti wa ijumaaa mzee akatoa pesa za mnadani za ng'ombe siku anaenda juwaonesha watoto wake akakuta watu wanaswali weeee ikawa noma mzee kaambiwa aliyemuuzia ana cheti cha wehu.
Papaa wemba alikuwa na gari lake linapeleka watu Nsororo mkifika njiani anawashusha mcheze mziki ukuweza kukata kiuno unaingia kwenye gari.
Mnakumbuka magari ya kazuge!!kaserekandis!! Niache nilivyo!!
Mnamkumbuka mzee Nyembo wa ipuli R.I.P .
Mboka noma.
Jamila Mgumia una mfahamu?Dah.. Wish sehem zote nizifaham, nikisikia stori hizi nakumbuka mbali sana, isevya rest in peace bibi na babu.. Stori nyingi humu huwa naziskia kwa mama n wakubwa zangu wakizungumzia.. I wish n mimi ningekuwa nachangia.. Rest in peace dad mzee mgumia, nikipata stor za tabora nakukumbuka mzee wangu..
Baaasi hayo tu,umemaliza?,au kahawa imekwisha?
Nafikiri wewe akili yako imejaa pumba zilizoungua,ooh mboka kulikuwa na chizi huyu na yule,oooh kulikuwa na muuza mihogo shule ya uyui,oooh kulikuwa na bubu pale sinema ya diamond,ooh kulikuwa na uwanja wa chipukizi,ooh sijui jambazi sugu Kandege,ooh Jetha muhindi alikuwa mwehu,oooh Roshi alikuwa mwehu,oooh Malingumu alikuwa mwehu,sasa wewe uliekimbia umande huna jingine?,kila siku ooh tujikumbushe Mboka,hiyo mboka imedorora kama nyasi zilizokauka,sababu ya majungu,ushirikina,ujambazi na kahawa na kucheza bao baaaaaasi,na yote hiyo imesababishwa na maupuuzi kama hayo,laiti ungekuwa na mawazo ya maendeleo usingekalia upupu unaotuletea marabuku.Acha pumba, kama huelewi kitu ujue hakikihusu
Hapana mkuu, ila nina uhakika atakuwa ni ndugu yangu, kibaya niliondoka tabora mdogo toka 98 sikurud tena hadi mwaka huu, nmefanya kama kupita kwenda urambo katika mazishi ya kaka yangu.. anaweza akawa ananijua, mie sikukaa sana upande wa faza wangu, but i wish niwajue ndugu zangu, naskia tupo wengi kupita maelezoJamila Mgumia una mfahamu?
Simbamwene tulikuwa tunaenda kuangua zambalau na embe boribo juu ya makaburi...vp umekuwa mji?ha ha ha ha ha ha umenikumbusha Mwajuma Ringa?ivi kwanini Mboka Manyema vichaa wengi?...dah Hamis Mambwa aliogopwaje?Diamond near by TMP uwanja wa Chipukizi?ukumbi wa Disco hapo Mwanaisungu geti la kuingia Uhazili...video tunangalizia Maua Bar Opposite na Central Police
nakumbuka tukio la mabehewa ya petroli kuwaka moto pale stesheni..kilikuwa kipindi cha vita ya ghuba,basi tukajua marekani na saddam wameanza kukinukisha na huku tayari.....lol!
I love u tabora, wakulugo.
Ye-ye-ye...mwanakadimu!