Tukumbushane Kashfa mbalimbali za Manji/ Quality Group

Tukumbushane Kashfa mbalimbali za Manji/ Quality Group

watu kama manji ni wakufilisiwa safi sana jpm piga kazi wapinzani hawana jipya
 
Hiyo NSSF si ndiyo ilikuwa inaongozwa na mtaalamu wa mambo ya uwekezaji? Ambaye kapewa kazi nyingine? FF ebu njoo hapa kidogo.
 
Nadhani tumeanza kuwa taifa la Chuki kabisa hatutaishia kwa huyo watakuwa wengi Maana roho mbaya hutafuta ubaya!
Ni kweli tusipokuwa makini. Kuna watu wanadhani umaskini wao umesababishwa na wewe.
 
Nadhani tumeanza kuwa taifa la Chuki kabisa hatutaishia kwa huyo watakuwa wengi Maana roho mbaya hutafuta ubaya!

Naam kwa kuchukia maovu na tuhesabike hivyo.Nuru na giza havikai pamoja.
 
Ulivyonijibu mimi umejibu vizuri zaidi kuliko unavyo comment katika mada. Ninachokisema ni kwamba si kila kukicha unamkumbusha Magufuli kuwa CCM ndiyo waliotufikisha hapo tulipo, Ndiyo kila mtanzania anajua hilo kwanini uendelee kuyasema yale ambayo wote tunayajua baada ya kuzungumza nini kinafanyika kwasasa.

Umesema huna haja ya kumsifu maana ni kazi yake ndiyo nakubaliana nawe, lakini kwa mantiki hiyo hiyo huwezi kuendelea kumlaum kwa mambo yaliyofanywa na CHAMA chake kwasababu tu yeye ni mwana CCM.

Jeremy Corbyn haamini kabisa nchi kumiliki nuclear deterrent lakini kwasasa yeye ni kiongozi wa Labour anaweza kuwa waziri mkuu aliulizwa wakati wa kampueni kua ana msimamo gani kwasasa kama amebadili, jibu lake lilikua ni moja mawazo ya mtu mmoja hayawezi kwenda kinyume na mawazo ya chama, hivyo kura imepigwa na chama kinaunga mkono nuclear deterrent hivyo anasupport maoni ya wengi. Ukiangalia majibu ya Jeremy utajua kuwa kuna wakati hata kama unapingana na mambo yanayopitishwa lakini unasema wengi wape. Kuna mawili ya kuyafanya, Jiuzuru halafu upinge ukiwa kama raia wa kawaida, ama ubaki nao kama mjinga huku ukitegemea kama kuna siku utapata nafasi na wewe ukaweza kubadilisha ukiwa ndani.

Unaweza kusema kwanini hakujiuzulu, unaweza ukawa sawa lakini kama angejiuzulu angeishia wapi? Kuna wangapi wamefanya hivyo katika siasa za Tanzania na Africa wambao wamefaulu? Alichokitumia Magufuli ni ungana nao jifanye ni mmoja wao nafasi ikipatikana waumbue na ndivyo anavyofanya sasa.

Mkuu, tunakubaliana kwenye vitu vingi, Mh Rais Magufuri inawezekana kabisa akawa na nia nzuri dhidi ya taifa au pia akawa anacheza sinema ambayo wazee na watu wa ndani wa CCM wakawa wanaifahamu, nina maana anaisafisha CCM kwenye macho ya watanzania baada ya kuona asilimia kubwa ya watanzania wamekata tamaa nayo...

Bado siamini kama CCM inaweza kutatua matatizo ya nchi hii au kutupeleka tunapopahitaji, mentality za wanaCCM kwa asilimia kubwa ni shida.. yapo mengi tunashuhudia ambayo hapa hayatoshi kuyaorozesha ila nitakupa kisa kimoja kilichotokea kwenye macho ya Mh Rais pale sabasaba siku ya uzinduzi wa maonyesho pale TANTRADE waliposimama na kumwambia Mh Rais wanataka kujenga hoteli huku kauli mbiu ya nchi ikiwa viwanda ( hapo ukumbuke TANTRADE walikaa jopo la wasomi wakaja na wazo hilo) nashukuru hili Mh Rais aliliona palepale akawajibu juu ya upuuzi waliotaka kuufanya,, sasa hizi ndio mentality zinazomzunguka Mh Rais..
 
Siku zote masikini anapenda watu wote wawe masikini kama yeye, badala ya yeye kujiinua awe tajiri.
 
Maccm yalifurahi kweli kweli!! Bado yakampa Na zawadi ya udiwani mbele kwa mbele!!
Wewe uhijui CCM, na mimi naijua kama chama makini katika kuboresha mbinu zake kukabiliana na changamoto za kuwaletea maendeleo watanzania. Je. kama huo udiwani ilikuwa hadaa ya kumfanya asitoroke!? Jiongeze mkuu.
 
Tatizo watu wengi bongo hawaelewi ni nani hasa amekula hizo hela. Manji hapo kwenye hizo dili amekula 10% tu kama ganji la kutumia kampuni yake. Waliokula ni hao hao wanao cheka na magufuli. Hizi dili zilikuwepo siku nyingi sana. Viongozi walikua wanafata wafanyabiashara na kuwapa hizi dili. Ukichunguza zaidi utagundua nyingi za hizi dili zilichezwa kabla ya uchaguzi.
 
1. Kashfa ya maghala.
Halafu halitaki kukaa rumande eti likae hospitali, tena wakati tu anapohitajiwa polisi?! Lijizi kabisa hili...nA MISHABIKI YAKE YATAKA TUMUONEE HURUMA! KWELI MAZUZU HAYAISHI TZ! Malipo hapa hapa duniani AKA TZ...
 
Back
Top Bottom