Tukope Trilioni moja kuukarabati mfumo wa Utawala Bora na Sheria ili kumaliza yote yanayoirudisha nchi yetu nyuma

winnerian

JF-Expert Member
Jul 12, 2015
335
530
Kuukarabati mfumo wa "Utawala bora" pamoja na sheria zetu ili kuziba na kurekebisha mianya, nyufa, matobo, maadili mabovu, uzembe ofisi za umma, pamoja na mambo yote yanayoifanya nchi yetu iende kinyumenyume ikiwa jitahada za dhati zinafanyika na viongozi wakubwa lakini bado matokeo hayaridhishi.

Amini amini nawaambieni hivi leo Rais anatamani sana kuona amefanya kwa ufanisi kwenye awamu yake lakini mfumo wetu hauwezi kumruhusu akatimiza ndoto zake, kwani chini yake ni msururu wa tamaduni zilizojishikiza kwenye mfumo usiotaka maendeleo ya wazi.

Katiba, sheria, na sekta nyingi zinazoelekeza njia ya maendeleo ni kama zimefifia mno kuweza kusomeka barabara.

Tukope hako katrilioni tukatumie kuisuka upya Tanzania na baada ya hapo hata kabilioni kamoja tu kataweza kutuvukisha mbali sana.
 
Wachina na wafanyabiashara wengi wanalalamikia sana namna ofisi za uma zilivyo slow kupush mambo. Yaani wanashangaa kuona jambo dogo sana linaweza kuchukua hata miezi mitatu kupatikana solution.

Nguvu kazi iliyopo katika ofisi za uma ni ndogo sana na bado ufanisi ni chini ya asilimia 40% na hivyo insababisha kupungua kwa kasi ya uzalishaji na maendeleo kwa ujumla.
 
Anzeni kufundisha maadili shuleni sio mnachapa tu watoto ili wakariri utumbo wanaokuja nao bungeni

Wafunzeni watoto kutokuwa waizi, heshima na adabu pamoja na kutokubali uonezi

Unalikuta jitu limekaa hospital au receptionist unamsalimia anakuambia Sema shida yako

Unatamani kumuambia hujalelewa na binadamu wewe
Hauwezi kumkunja samaki akiwa kakauka
 
Back
Top Bottom