Tukitaka kodi ya SIMcard ifutwe tufanye hivi

Tukitaka kodi ya SIMcard ifutwe tufanye hivi

:horn:NI WAZO TU NATOA::horn:
Kwa nini kwa mtu anaeweza kutunga SMS nzuuri yenye maneno ya kueleweka na kuhamasisha watu juu ya jambo hili asituwekee hapa kisha sisi tuichague inayofaa then MODS wakaiweka pale mwanzo chini ya post ya MwanaHaki ili kwa kuanza tu sisi tuliona uwezo wa internet tui copy kwa simu zetu na kuanza kuwatumia wengine kwa njia ya SMS kuwahamasisha na wengine juu ya harakati hii...mpaka kufika hiyo tarehe itakuwa watu wengi zaidi wamepata taarifa...maana naona maneno yamekuwa mengi kuliko vitendo...:amen:
 
Last edited by a moderator:
TAHADHARI: Nimegundua jambo moja ambalo limenifanya nisitishe mpango wa kuutangaza mgomo huu kwenye vyombo vya habari. Ieleweke kwamba Serikali inakusanya kodi nyingi sana kupitia simu za mkononi, tayari nimebainisha vyanzo vya mapato hayo kwa kampuni za simu, ambayo yanafungamana moja kwa moja na mapato ya Serikali, kwani, kwa kila chanzo cha mapato, kuna kodi ambayo inaenda serikalini. Kwa hiyo, iwapo tutautangaza mgomo huu, kuna hatari ya kutofanikiwa kwa kuwa:


  1. Serikali itadai kwamba tunawachochea wananchi kuinyima mapato Serikali, jambo ambalo ni kosa kisheria
  2. Iko hatari ya sisi kuchukuliwa hatua za kisheria, kutokana na "uchochezi" huo

Hivyo basi, napendekeza kwamba yeyote yule ambaye alitoa taarifa hizi kwa mwandishi yeyote wa habari, AMTAFUTE HARAKA SANA ili amwambie asitishe kutoa habari hizi. Mimi nina imani na Watanzania, kwamba watauitikia kwa kila hali mgomo huu, na kwamba watauunga mkono iwapo wataeleweshwa kwa kina misingi yake yote.

Ninyi, kama wanaharakati, mnalo jukumu hili zito la kuwaelimisha Watanzania, kwani tayari mnaelewa nini kinahitajika.

Nawatakieni mafanikio mema.
 
:horn:NI WAZO TU NATOA::horn:
Kwa nini kwa mtu anaeweza kutunga SMS nzuuri yenye maneno ya kueleweka na kuhamasisha watu juu ya jambo hili asituwekee hapa kisha sisi tuichague inayofaa then MODS wakaiweka pale mwanzo chini ya post ya MwanaHaki ili kwa kuanza tu sisi tuliona uwezo wa internet tui copy kwa simu zetu na kuanza kuwatumia wengine kwa njia ya SMS kuwahamasisha na wengine juu ya harakati hii...mpaka kufika hiyo tarehe itakuwa watu wengi zaidi wamepata taarifa...maana naona maneno yamekuwa mengi kuliko vitendo...:amen:

Naunga mkono hoja yako. Ngoja niuandike ujumbe huo kisha nitaunganisha kwenye post yangu ya kwanza kabisa.

Asante kwa ushauri.
 
Naunga mkono hoja yako. Ngoja niuandike ujumbe huo kisha nitaunganisha kwenye post yangu ya kwanza kabisa.

Asante kwa ushauri.
Afu pale ungeongeza kidogo na vimaneno kama: Tuma ujumbe huu kwa watu wengine labda 5 hivi..maana si unajua mtu anaweza akaupokea then asichukue hatua ya kuwataarifu na wengine maana nia ni kupata as much people as we can!!
 
UJUMBE UNAOPENDEKEZWA AMBAO HUNA HERUFI 155 (HERUFI 5 PUNGUFU YA HERUFI 160 AMBAZO NDIZO HUHESABU UJUMBE MMOJA WA SIMU, YAANI SMS):

Ndugu Mtanzania: Onesha uzalendo wako kupinga kodi ya SIMcard, ya Shs. 1,000 kwa mwezi kwa kuzima simu yako saa 6 usiku, 19/8/13 hadi saa 6 usiku, 20/8/13.

Nimeuhariri ujumbe huu nikizingatia MSINGI wa harakati hizi pia pamoja na kuweka tarehe. Tafadhalini utumeni ujumbe huu wa watu wengi inavyowezekana, na wao wanaweza kuwaleza watu wengine hata kwa mdomo, bila ya kuwapigia simu. Kampeni zifanyike mitaani, kanisani, misikitini, kwenye baa na sehemu yoyote ile wanapokusanyika watu
 
Afu pale ungeongeza kidogo na vimaneno kama: Tuma ujumbe huu kwa watu wengine labda 5 hivi..maana si unajua mtu anaweza akaupokea then asichukue hatua ya kuwataarifu na wengine maana nia ni kupata as much people as we can!!
sijui nini, nikiongeza maneno hayo hautakuwa ujumbe mmoja mfupi wa simu, bali miwili kwa pamoja. Hebu niambie ni wangapi wanaweza kutuma zaidi ya ujumbe mmoja kwa wakati? Nina imani kwa jinsi watu walivyochoka na hali mbaya ya kiuchumi, na jinsi wanavyoichukia kodi hi, dhahiri watawaeleza wengine kuhusu mgomo huu. Anza kuwatumia watu wako, kama unaona inafaa kuongeza maneno hayo, ongeza.
 
Last edited by a moderator:
sijui nini, nikiongeza maneno hayo hautakuwa ujumbe mmoja mfupi wa simu, bali miwili kwa pamoja. Hebu niambie ni wangapi wanaweza kutuma zaidi ya ujumbe mmoja kwa wakati? Nina imani kwa jinsi watu walivyochoka na hali mbaya ya kiuchumi, na jinsi wanavyoichukia kodi hi, dhahiri watawaeleza wengine kuhusu mgomo huu. Anza kuwatumia watu wako, kama unaona inafaa kuongeza maneno hayo, ongeza.
Anyway, sio mbaya was just findind away ya kuwafanya ujumbe huu uenee kwa haraka zaidi..maana si unajua wabongo na sms za "tuma ujumbe huu kwa rafiki zako watano" zinavyotambaa fasta na kwa wengi zaidi..!! Poa mi nimechaucopy...natutupia kwa watu kwa kutumia sms zangu za bundle zote nlizonazo leo..!!!
 
TAHADHARI: Nimegundua jambo moja ambalo limenifanya nisitishe mpango wa kuutangaza mgomo huu kwenye vyombo vya habari. Ieleweke kwamba Serikali inakusanya kodi nyingi sana kupitia simu za mkononi, tayari nimebainisha vyanzo vya mapato hayo kwa kampuni za simu, ambayo yanafungamana moja kwa moja na mapato ya Serikali, kwani, kwa kila chanzo cha mapato, kuna kodi ambayo inaenda serikalini. Kwa hiyo, iwapo tutautangaza mgomo huu, kuna hatari ya kutofanikiwa kwa kuwa:


  1. Serikali itadai kwamba tunawachochea wananchi kuinyima mapato Serikali, jambo ambalo ni kosa kisheria
  2. Iko hatari ya sisi kuchukuliwa hatua za kisheria, kutokana na "uchochezi" huo

Hivyo basi, napendekeza kwamba yeyote yule ambaye alitoa taarifa hizi kwa mwandishi yeyote wa habari, AMTAFUTE HARAKA SANA ili amwambie asitishe kutoa habari hizi. Mimi nina imani na Watanzania, kwamba watauitikia kwa kila hali mgomo huu, na kwamba watauunga mkono iwapo wataeleweshwa kwa kina misingi yake yote.

Ninyi, kama wanaharakati, mnalo jukumu hili zito la kuwaelimisha Watanzania, kwani tayari mnaelewa nini kinahitajika.

Nawatakieni mafanikio mema.

sasa watu watazima vipi simu bila kuwajulisha? TANGAZA tu kila kitu kina ugumu wake
 
Wakuu,

Ndumilakuwili wa kutugawa tayari wameshaanza kujitokeza. Mtu ambaye sikumtarajia, ambaye nilimheshimu sana, ame-copy and paste mkakati wetu huu. Si mwingine bali ni Mzee Mwanakijiji. Nendeni mkasome alichokiweka kule kwenye Jukwaa la Habari na Hoja Mbali Mbali.

Halafu keshakuja mwingine hapa hapa Jukwaa la Siasa, anapendekeza mgomo wa kuzima simu saa 12.

Vibaraka wa mafisadi ni wengi, lakini msikate tamaa. Tuwe na msimamo. Tusitetereke. Waachieni akina Mzee Mwanakijiji na wenzake waendeleze undumilakuwili wao. Eti mgomo Julai 29, Julai 30 na Julai 31! Mama weee! Watajitokeza watu wangapi katika siku chache hizo? Waambieni wadau wenu, HATUJABADILISHA TAREHE!

Duh! Maajabu hayaishi kumbe. Simshangai tena Musa wala Farao!
 
Last edited by a moderator:
sasa watu watazima vipi simu bila kuwajulisha? TANGAZA tu kila kitu kina ugumu wake

Wewe ni kibaraka, nishakushtukia.

Tunisia ilipinduliwa na Wananchi wake kwa kujipanga kutumia FACEBOOK pekee. Hawakutangaza kwenye media hata moja kwa kuwa wanajua madhara yake. Sasa wewe unataka kutupeleka mahali ambapo hatutaki. Tayari tunaitumia Facebook, Twitter na JF. Zinatosha. Hatutangazi kwenye media.

Hebu tuondokee! Unatuchefua kibaraka weee! Poleeee! Wrong number, jaribu tena! NKTTTTT!
 
Wakuu,

Ndumilakuwili wa kutugawa tayari wameshaanza kujitokeza. Mtu ambaye sikumtarajia, ambaye nilimheshimu sana, ame-copy and paste mkakati wetu huu. Si mwingine bali ni Mzee Mwanakijiji. Nendeni mkasome alichokiweka kule kwenye Jukwaa la Habari na Hoja Mbali Mbali.

Halafu keshakuja mwingine hapa hapa Jukwaa la Siasa, anapendekeza mgomo wa kuzima simu saa 12.

Vibaraka wa mafisadi ni wengi, lakini msikate tamaa. Tuwe na msimamo. Tusitetereke. Waachieni akina Mzee Mwanakijiji na wenzake waendeleze undumilakuwili wao. Eti mgomo Julai 29, Julai 30 na Julai 31! Mama weee! Watajitokeza watu wangapi katika siku chache hizo? Waambieni wadau wenu, HATUJABADILISHA TAREHE!

Duh! Maajabu hayaishi kumbe. Simshangai tena Musa wala Farao!

hivi una akili kweli? angalia mkakati wenu mlitangaza lini na miimi nilianza lini kutangaza hili halafu uje useme nani kamkopy nani...
 
hivi una akili kweli? angalia mkakati wenu mlitangaza lini na miimi nilianza lini kutangaza hili halafu uje useme nani kamkopy nani...
Mzee Mwanakijiji nimefuata ushauri wako na nimeangalia tarehe ambayo umeweka post yako: Today 7:54 PM

Haya, sema kingine. Au labda uende kuangalia post yangu niliiweka lini? Usisumbuke... hii hapa: Yesterday: 9:24 (ilikuwa ni asubuhi kaka... yaani AM)

Kati ya mimi na wewe nani aliyeanza? Kama ninakosea, nipe direct link ya post yako hiyo, niambie iko kwenye Jukwaa gani na ukurasa wa ngapi, kama ni zaidi ya ukurasa mmoja. Vinginevyo, umeingia "choo cha kike"!
 
Last edited by a moderator:
Mzee Mwanakijiji nimefuata ushauri wako na nimeangalia tarehe ambayo umeweka post yako: Today 7:54 PM
Kati ya mimi na wewe nani aliyeanza? Kama ninakosea, nipe direct link ya post yako hiyo, niambie iko kwenye Jukwaa gani na ukurasa wa ngapi, kama ni zaidi ya ukurasa mmoja. Vinginevyo, umeingia "choo cha kike"!

1070089_10151629821526156_1290851848_n.jpg
 
Mzee Mwanakijiji, mbona umefuta tarehe, tena kwa wino mwekundu? Hebu jiweke wazi mzee... funguka. Unaogopa nini? Wewe si ulianza mwanzo?

sijafuta tarehe; kuna Jumatatu moja tu wiki hii; mstari mwekundu ni kukuonesha siku; kwa vile wewe ulifanya Jumatano; Jumatatu yoyote kabla ya hapo itakuwa imekutangulia; haijalishi tarehe. Kwa ajili ya ubishi usio na sababu imebidi niweke tena hapa:

600598_10151629885321156_736004402_n.jpg
 
Mzee Mwanakijiji

Nilipoanzisha mkakati huu sikuwa na habari kwamba hata wewe ulikuwa umeuanzisha, kwani hakuna mtu mwenye "monopoly of ideas". Kwa kuwa uliuanzisha kwenye mtandao mwingine wa kijamii, ambao binafsi naona ni jambo ambalo halikuwa "effective", ulipoamua kuuleta hapa, ikawa rahisi kukuona wewe kuwa mtu wa "copy and paste", na kukudhania kuwa ni kibaraka aliyetumwa kutuvurugia. Kwa hili, niwie radhi.

Binafsi, tarehe ulizozitaja na namna ambayo wewe unataka boycott ifanyike haitakuwa effective, kwa kuwa inahitajika si chini ya siku 30 kuratibu boycott kwa mafanikio. Kumbuka, Tanzania ni nchi kubwa yenye watu wengi. Kuna sehemu ambazo ili upate mawasiliano ya simu za mkononi, lazima upande juu ya paa la nyumba, mti mrefu au hata sehemu ya mlima au kilima kirefu. Halafu unawapangia watu kwamba siku fulani ni ya mtandao fulani. Dawa ni kusema, mitandao yote kwa muda wa saa kadhaa, kama nilivyotamka. Pia, tukiwa na united front tutakuwa more effective, kuliko kufanya mambo kila mtu kivyake. Endelea na mkakati wako, lakini nakushauri uzingatie suala la muda. Umeingiza mkakati huu JF, halafu kwenye Jukwa la Habari na Hoja Mchanganyiko, ambalo si effective kama Jukwaa la Siasa. Wewe ni mwanachama wa JF wa miaka mingi, hili walijua.

Kila la heri.
 
Last edited by a moderator:
Wakuu

Hiki ndicho kipeperushi nilichoandaa kwa ajili ya mkakati wetu huu.

TANZANIA KWANZA FLYER.jpg
 

Attachments

  • TANZANIA KWANZA FLYER.jpg
    TANZANIA KWANZA FLYER.jpg
    486.1 KB · Views: 56
Mzee Mwanakijiji

Nilipoanzisha mkakati huu sikuwa na habari kwamba hata wewe ulikuwa umeuanzisha, kwani hakuna mtu mwenye "monopoly of ideas". Kwa kuwa uliuanzisha kwenye mtandao mwingine wa kijamii, ambao binafsi naona ni jambo ambalo halikuwa "effective", ulipoamua kuuleta hapa, ikawa rahisi kukuona wewe kuwa mtu wa "copy and paste", na kukudhania kuwa ni kibaraka aliyetumwa kutuvurugia. Kwa hili, niwie radhi.

Nimekusamehe. Good luck and keep up the fight.
 
hivi una akili kweli? angalia mkakati wenu mlitangaza lini na miimi nilianza lini kutangaza hili halafu uje useme nani kamkopy nani...

hahahaha MwanaHaki ni kama anagombana na yeyote aliingia kwenye harakati za kupinga hii kodi, mimi simuelewi kwa nini anataka njia yake tu ndio ifiatwe na kukanda nyingine au kusema wamemcopy? tatizo ni nini?
 
Last edited by a moderator:
[h=2]CCM yapinga tozo laini za simu[/h]ALHAMISI, JULAI 18, 2013 06:13 NA MWANDISHI WETU

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimekuja juu na kuitaka Serikali kuangalia njia nyingine mbadala ya kukusanya kodi na kuachana na mpango wa kuanza kuwatoza wananchi tozo ya Sh 1,000 kila mwezi kwa kila laini ya simu ya kiganjani.

Hatua hiyo, inatokana na kilio cha wananchi ambao tangu Bunge la Bajeti kwa mwaka 2013/14 kupitisha sheria hiyo, kumekuwa na manung’uniko mengi.

Uamuzi huo, ulipitishwa na Bunge baada ya mjadala mkali pindi bajeti ilipotangazwa kitendo kilichomfanya Waziri wa Fedha na Uchumi, Dk. William Mgimwa kuomba Serikali ipewe muda wa kutosha wa kujadili suala hilo.

Baada ya majadiliano na Kamati ya Bajeti ambayo inaongozwa na Mbunge wa Bariadi, Chenge Chenge (CCM), Waziri Mgimwa pamoja na Bunge waliridhia wananchi waanze kutozwa fedha hizo, kuanzia Julai mosi mwaka huu.

Taarifa iliyotolewa na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye mjini Dar es Salaam jana, ilisema CCM inapinga tozo hiyo kwa sababu itaongeza mzigo kwa mwananchi wa kawaida na kusababisha usumbufu usiokuwa na sababu kwa walalahoi.

Tozo hiyo, ilipitishwa na Bunge la Bajeti ikielezwa kuwa ni utaratibu wa kawaida wa kuibua vyanzo vipya vya kodi pale vinapoondoshwa vilivyopo kwa sababu mbalimbali.

Katika taarifa hiyo, Nape alisema licha ya umuhimu huo, vigezo vilivyotumika kupanga viwango sawia vya kodi hiyo kwa kila mtu mwenye laini ya simu, havijazingatia hali ya utofauti wa kipato kwa Watanzania.

Alisema wengi wao, matumizi yao ya simu ni ya kiwango cha chini mno tofauti na Serikali inavyofikiria.

"Kama chama tawala, tunaona hatuwezi kukaa kimya kwenye jambo ambalo tunaliona linawabebesha mzigo wananchi na huenda likarudisha nyuma maendeleo na kuchelewesha jitihada za kuboresha maisha ya Watanzania kwa ujumla," ilisema taarifa hiyo.
 
Back
Top Bottom