Tukitaka kodi ya SIMcard ifutwe tufanye hivi

Tukitaka kodi ya SIMcard ifutwe tufanye hivi

Mkuu nimekusoma (kukuelewa) vizuri sana hizo mbinu ni takatifu kama shambulio basi hili naliita KISU CHASHINGO yani hapa adui humpi nafasi hata ya kuomba maji. Ila hizi plane kwa hapa bongo bado ni ngumu ukilinga nisha na mataifa mengine, nakinacho ipa ugumu plani hizi ni unafiki na kutokua wazalendo myoyoni mwetu. Tukubali tukatae plane namba moja ni nzuri kama tusinge kuwa wanafiki, nina uhakika pindi tutakapo kubaliana kuzima simu zetu wapo watakao tusaliti nakuendelea na matumizi yao kama kawa

Waache wafu wakazike wafu wao!

Watakapojikuta wakiwapigia wenzao walio kwenye mgomo, wataona haya na wao kuingia vitani.

Daima tusikubali wanafiki kutukatisha tamaa. Kuwa na imani ndugu yangu.

Hii ni vita takatifu. Imebarikiwa na Mungu wetu!
 
Watanzania tumekuwa waoga sana wa kutekeleza maamuzi yetu wengi wetu ni watu wa porojo nyingi kutekeleza inakuwa ngumu.

Kama CHADEMA iliweza kurejesha kata 4 za Jiji la Arusha, tena kwa kishindo, licha ya vitusho na hujuma nyingi kutoka CCM, basi, mimi naamini kwamba Watanzania wa leo sio watu wa porojo.

Mpango huu ni vita takatifu. Umebarikiwa na Mungu wetu, haijalishi wewe uko dini gani, kwani sisi wote ni watoto wa Mungu. Atakayetusaliti na afanye hivyo, lakini asitukatishe tamaa. NI MARUFUKU kukata tamaa!
 
Ingawa na mimi kipato changu kinategemea kampuni za simu lakini kwa hili lazima niunge mkono.

Hakika wewe Masuke ni shujaa! Umenifanya nijawe na faraja ndugu yangu. Lazima tuungane, tuweke kando itikadi zetu. Watanzania kwanza!
 
Last edited by a moderator:
Mimi nimeshaanza kusambaza sisubiri kuambiwa/kufumbuliwa macho na slaa/msigwa.Nishaanza kusambaza hata ww unaesoma nishakusambazi.a basi tuungane kwa hili.'Tunaanza na Mungu Tutamaliza na mungu'
Mungu Ibariki Tanzania
 
Jamani huu mgomo tuanzishe lini? Maana utatusaidia sana sisi walala hoi.
 
Njia hii itafaa sana lakini ni jinsi gani watanzania wataweza kapata hizo taarifa ili tukubaliane wote pamoja na ili sumu ifike kwenye mifupa na mioyo ya kampuni za simu.

Jana niliongea na mjombawangu kijijini alinipa taarifa kuwa kama tozo la shilingi 1,000/= kwa line litafanyoka basi huenda ikawa ndiyo mwisho wa yeye kumiliki simu. akasema hawezi kulipia shilingi 1,000/ huku hata airtime yenyewe mpaka atumiwe na wajukuu zake, akazidi kusema kuwa kwa kijijini sh 1,000 ni debe la mahindi au mboga ya kula na familia yake. hawezi kuichangia serikali. Nikamuuliza ailaumu serikali na chama chake tawala nikimaanisha CCM kwaani yeye ni mwenyekiti wa kitongoji kupitia CCM. akaniuliza kuwa kwani wao ndiyo wameweka huo ushuru kwenye kodi? nikamwambia ni mapendekezo ya serikali kwenye bajeti ya mwaka huu ambayo ilipishwa na wabunge waliowengi yaani CCM. Akashangaa sana wabunge kupitisha maumivu makubwa kwa wapiga kura wao huku wakijua hali zao. akaniahidi kumuuliza mbunge wake kwa nini alipitisha kodi hii bungeni. baada ya hapo niliongea na mama yangu mdogo akaniambia mwisho wa mwezi simu yake haitakuwa hewani kwa kuwa hawezi kulipa hiyo kodi.
 
Jamani huu mgomo tuanzishe lini? Maana utatusaidia sana sisi walala hoi.
Hakikwanza

Kaka ungesoma post hapo juu. Ni siku 30 baada ya tarehe 20 Julai, ambazo zitaangukia tarehe 19 Agosti. Kwa hiyo, mgomo utaanza saa 6 usiku, 19 Agosti na kukamilika saa 6 usiku, 20 Agosti, ikiwa ni muda wa saa 24.

Anza kuwapa habari wenzako.
 
Last edited by a moderator:
kuanzia trh 26 wajulishe na wengne 15.

Kaka usipotoshe. Hiyo si tarehe stahiki. Lazima tuwe na umoja. Mgomo ni siku 30 baada ya tarehe 20 Julai, ambapo mgomo utaangukia saa 6 usiku, 19 Agosti hadi saa 6 usiku, 20 Agosti, ambao utakuwa ni muda wa saa 24.

Ninapendekeza iwe hivyo kwa kuwa tunahitaji muda wa kutosha kujipanga. Nchi hii ina watu wengi sana. Tarehe unayoitaka wewe haitatupa ufanisi tunaoutaka. Washiriki watakuwa wachache. Kuna maeneo mengine ambapo mawasiliano ya simu ni mpaka mtu upande juu ya paa la nyumba, uende mlimani au upande mti. Sasa unataka kuniambia kwa tarehe yako hiyo habari zitawafikia hao watu?

Usituvurugie! Umetumwa?

Mods: Hebu mpeni ban ya saa 24 huyu fedhuli! Anatuchefua!

NILIJUA MTAKUJA KUTUVURUGIA! NDULI NYIE! VIBARAKA WA MABEBERU!
 
Well written. Mimi nina karibu mwezi situmii simu ya mtandao mmojawapo. Nimeizima.

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums

Good idea. Mimi mwenyewe nimezima moja. Hata hivyo nilihitaji zaidi kujua ni mtandao upi una hisa nyingi za viongozi ndio ni 'mute'.

Ni vizuri kuwaelimisha watanzani 'on austerity measures' za kiuchumi. Nafahamu wengi wana sim cards zaidi ya mbili na walizitafuta kwa uhitaji wa kupunguza gharama zilizokuwa kubwa ktk mitandao tofauti ambayo ilikuwa haitaki kufanyiana bihashara.

Imagine una sim card tatu na kila sim card unakatwa 1000 kila mwezi zidisha mara 12 (miezi). Kama tunazima sim card mojawapo ya mitandao hiyo labda voda (kama ndo kuna hissa kubwa za wabunge) watakosa mapato na zaidi kufunga mtandao huo. Wakati huo sisi hatuna hasara kwa sababu mawasiliano ya mtandao mmoja yanatosha...let's try this...
 
Njia hii itafaa sana lakini ni jinsi gani watanzania wataweza kapata hizo taarifa ili tukubaliane wote pamoja na ili sumu ifike kwenye mifupa na mioyo ya kampuni za simu.

Jana niliongea na mjombawangu kijijini alinipa taarifa kuwa kama tozo la shilingi 1,000/= kwa line litafanyoka basi huenda ikawa ndiyo mwisho wa yeye kumiliki simu. akasema hawezi kulipia shilingi 1,000/ huku hata airtime yenyewe mpaka atumiwe na wajukuu zake, akazidi kusema kuwa kwa kijijini sh 1,000 ni debe la mahindi au mboga ya kula na familia yake. hawezi kuichangia serikali. Nikamuuliza ailaumu serikali na chama chake tawala nikimaanisha CCM kwaani yeye ni mwenyekiti wa kitongoji kupitia CCM. akaniuliza kuwa kwani wao ndiyo wameweka huo ushuru kwenye kodi? nikamwambia ni mapendekezo ya serikali kwenye bajeti ya mwaka huu ambayo ilipishwa na wabunge waliowengi yaani CCM. Akashangaa sana wabunge kupitisha maumivu makubwa kwa wapiga kura wao huku wakijua hali zao. akaniahidi kumuuliza mbunge wake kwa nini alipitisha kodi hii bungeni. baada ya hapo niliongea na mama yangu mdogo akaniambia mwisho wa mwezi simu yake haitakuwa hewani kwa kuwa hawezi kulipa hiyo kodi.
rugumye

Kuna njia mbili ambazo tunaweza kupashana habari. Ya kwanza ni kupitia ujumbe mfupi, ya pili ambayo haina gharama yoyote ile ni kuongea na majirani zetu tukiwaelezea kuhusu mpango huu na kuwaomba wawaambie wenzao.

Tarehe ninayokubaliana nayo ni siku 30 baada ya 20 Julai, ambapo itaangukia saa 6 usiku wa 19 Agosti hadi saa 6 usiku wa 20 Agosti, ambapo itakuwa ni muda wa saa 24.

Ukiweza kuongea na waandishi wa habari itasaidia pia.
 
Last edited by a moderator:
Kaka usipotoshe. Hiyo si tarehe stahiki. Lazima tuwe na umoja. Mgomo ni siku 30 baada ya tarehe 20 Julai, ambapo mgomo utaangukia saa 6 usiku, 19 Agosti hadi saa 6 usiku, 20 Agosti, ambao utakuwa ni muda wa saa 24.

Ninapendekeza iwe hivyo kwa kuwa tunahitaji muda wa kutosha kujipanga. Nchi hii ina watu wengi sana. Tarehe unayoitaka wewe haitatupa ufanisi tunaoutaka. Washiriki watakuwa wachache. Kuna maeneo mengine ambapo mawasiliano ya simu ni mpaka mtu upande juu ya paa la nyumba, uende mlimani au upande mti. Sasa unataka kuniambia kwa tarehe yako hiyo habari zitawafikia hao watu?

Usituvurugie! Umetumwa?

Mods: Hebu mpeni ban ya saa 24 huyu fedhuli! Anatuchefua!

NILIJUA MTAKUJA KUTUVURUGIA! NDULI NYIE! VIBARAKA WA MABEBERU!
Nimeshaanza ku edit.nakuunga mkono ni trh 19.Wajurishe na wenzio 15
 
I support the move. Tutaarifiane siku ya kufanya hivyo. hata hivyo ningeshauri vyama vya siasa viingilie kati suala hili. CDM my political party, tafadhari engineer mpango huu ili huwe na ufanisi. Watanzania wanaagamizwa na hawa mabeberu!!
 
Hii ni njia nzuri zaidi kuwafunza hawa waonevu
dizzle kiraka

Hayo ni mawazo finyu. Hebu nenda VETA Dar es Salaam uombe kuonana na wanafunzi vijana kabisha waliovumbua mashine za kuzalisha umeme kwa njia ya pekee. Mmoja amevumbua mashine ya kuzalisha umeme kwa kubadilisha sauti na mwanga kuwa umeme. Mwenzake amevumbua mashine ya kuzalisha umeme kwa kuukuza, akitumia betri ya Volt 12 DC, ambapo amevumbua jenereta inayozalisha umeme wa 5KVA, unaotosha kutoa umeme kwa kaya TANO!

Huu ni uvumbuzi wa Kitanzania. Kwa hiyo bado unaamini kwamba Wazungu wana akili kuliko sisi?

Jifungue hiyo minyororo ya utumwa wa kifikra! WAAFRIKA TUNAWEZA TUKIAMUA! Sasa tumeamua!
 
Last edited by a moderator:
I support the move. Tutaarifiane siku ya kufanya hivyo. hata hivyo ningeshauri vyama vya siasa viingilie kati suala hili. CDM my political party, tafadhari engineer mpango huu ili huwe na ufanisi. Watanzania wanaagamizwa na hawa mabeberu!!

Mutakyamirwa

Mkuu, tukitaka mpango huu UFANIKIWE, tuweke kando vyama vya siasa. Tusihusishe chama HATA KIMOJA, kiwe cha upinzani AU OTHERWISE! Sikuanzisha mpango huu ili kuwasaliti walalahoi wenzangu kwa wanasiasa. Wengi wao ndio chanzo cha matatizo, watatuvurugia. Huu ni mpango wa Watanzania! Umeanzia JF, lakini utaenea nchi nzima.

Ukombozi huletwa na wananchi, SI wanasiasa!

Kuhusu siku ya mgomo ni muda wa siku 30 baada ya tarehe 20 Julai 2013, ambazo zitaangukia saa 6 usiku, 19 Agosti hadi saa 6 usiku, 20 Agoosti 2013.

Tanzania ni nchi kubwa, inahitaji muda wa kutosha kujipanga ili mgomo huu ufanikiwe.

IMETOSHA SASA!
 
Tuwekee tarehe ya kuzima hizi cm zetu na ujitolee kuitangaza kwa njia nyengine tarehe hiyo, Na hata kama hili Watanzania watashindwa kulitekeleza nitajua kuwa mabadiliko hayawezi kupatikana katika ardhi hii.
kuanzia 19.wajulishe na wengine 15
 
Back
Top Bottom