Tukisema Royal Tour Tulipigwa tunamaanisha ukweli

voicer

JF-Expert Member
Jul 13, 2020
5,553
11,885



Kwamba Tanzania Royal Tour ilikuwa ni siasa, Royal Tour ilikuzwa kuliko uhalisia wake.

Na pia Royal Tour Documentary haikuwa na maudhui yoyote makubwa yenye ushawishi kwa watalii kuweza kuijua Tanzania pamoja na vivutio vyake.

Bali Royal Tour ilitumika na kundi la wajanja ndani na nje ya nchi hii,ili kumuweka Rais Samia karibu yao zaidi.
Na hatimae kutimiza malengo yao kisiasa na kiuchumi.

Nimeweka video links hapa,za Documentary mbili tofauti,moja ni hiyo Royal Tour,na ingine ni ya mzungu binafsi aliyetumia pesa zake kiduchu,na hatimae kuitangaza Tanzania kuliko hiyo Royal Tour.

Na hapo muelewe kwamba Royal Tour ilitumia zaidi ya Bilioni 12,huku majina ya wachangiaji yakiwekwa kapuni mpaka leo hii
 
Royal Tour ilitumia zaidi ya Bilioni 12,huku majina ya wachangiaji yakiwekwa kapuni mpaka leo hii
Suppose ingetumia 100 billions na kuonyesha tuu the potrait photo ya Samia, kama ilivyo picha ya Mona Lisa iliyochorwa na Leonardo Da Vinci, na hizo billions sio zetu ni za mfadhili wa kujitolea, kuna tatizo gani?.

Watanzania tujifunze kuwa na shukrani hata kwa madogo tuu ili tujaaliwe makubwa!. Kitendo tuu cha a documentary ambayo sterling wake ni citizen number one wa Tanzania, ina impact kubwa kuliko a 100 millions dollars documentary ya National Geographical!.

Don't compare Mbingu na Ardhi!
P
 
Suppose ingetumia 100 billions na kuonyesha tuu the potrait photo ya Samia, kama ilivyo picha ya Mona Lisa iliyochorwa na Leonardo Da Vinci, na hizo billions sio zetu ni za mfadhili wa kujitolea, kuna tatizo gani?...
Mkuu heshima yako.

Vipi kwa mtazamo wako,je ilikuwa na impact yoyote kwa taifa au ilikuwa ni upepo wa kisulisuli na bizness as usuals. Please msaidie mleta mada.
 
Suppose ingetumia 100 billions na kuonyesha tuu the potrait photo ya Samia, kama ilivyo picha ya Mona Lisa iliyochorwa na Leonardo Da Vinci, na hizo billions sio zetu ni za mfadhili wa kujitolea, kuna tatizo gani?...
Huyo mfadhili wa kujitolea ni nani? na alipewa/atapewa nini in return?

Ni aibu kiongozi mkuu wa nchi kupewa pesa uchochoroni na kuja kuzitumia kwenye mambo yetu ya ndani, ni aibu na wala sio jambo la kupongezwa
 
Last edited:
Suppose ingetumia 100 billions na kuonyesha tuu the potrait photo ya Samia, kama ilivyo picha ya Mona Lisa iliyochorwa na Leonardo Da Vinci, na hizo billions sio zetu ni za mfadhili wa kujitolea, kuna tatizo gani?.
..

Mzee hapa umetoa boko.

Mimi ni mfuatiliaji mzuri wa National Geographic Channel zote 2.

Wana watu zaidi ya 2 billion viewers na subscribers, wana data base ya wataalum (exploreres, wild animal doctors,Ecologist ,etc)
Wana fund projects zaidi ya 15,000 kwa mwaka.

Usirudie tena kuongea hiyo kitu.

Kama nchi hii ingekuwa inatumia akili, wangetengeneza extended documentary ambayo ingekuw inarushwa kwa mwezi au miezi kibao, sasa mnatengeneza kapicha na kukazindua marekani mnarudi hapa bongo mmekaa tu.

Viewers zaidi ya 2 BILLION, embu

IHESHIMU NATIONAL GEOGRAPHIC CHANNEL
NA USIRUDIE HII KAULI TENA SAWA?
 


Kwamba Tanzania Royal Tour ilikuwa ni siasa,Royal Tour ilikuzwa kuliko uhalisia wake..

Umesema kweli. Tulishasema mama aliwahiwa na wajanja wenye kumjua fikra zake wakapiga hela refu. Binafsi nilikerwa sana na mlaghai tony blair kuwahi kabla mama hajatoa tongotongo akapiga zaidi ya dola laki kadhaa ule mkopo wa imf eti kuitangaza tz na kuisafisha dhidi ya sifa mbaya aliyoleta magufuli?

Huyu mhuni wa royal tour naye akaja kutupiga mabilioni. Alichofanya sio chochote kwa hiyo hela. Kuna documentary nyingi zinazagaa kuhusu vivutio vya tanzania wala royal tour sio chochote. Kuna tanzania safari ya tbc nayo ina roll yake.

Kilichotokea baada ya royal tour ni watalii waliyokua wamekwama kwa covid 19 na kazi nzuri ya ttc kwa kushirikiana na ubalozi zetu kuitangaza tanzania.
 
Huyo mfadhili wa kujitolea ni nani? na alipewa nini in return?

Ni aibu kiongozi mkuu wa nchi kupewa pesa uchochoroni na kuja kuzitumia kwenye mambo yetu ya ndani, ni aibu sio
Sidhani kama Kuna favor maana hii nchi wanaojikomba ni wengi. Shigongo alilipwa Nini licha ya kujikomba vile Hadi kutengeneza ma T shirt nchi nzima?

Nakumbuka hata Private Sector ilimuita JPM na kumpigia kampeni ya wazi and possibly walimchangia Hela ya kampeni. So kwa Tanzania usishangae ni CRDB na NSSF ndio walikimbilia kutoa Hela Ili wajikombe kombe kwa Rais!!

Wanaotoa Hela wapate favor labda huko wazungu ila wa humu huwa kama mazombie yenyewe yanatoa Hela kama kujikomba sio kuomba favor.
 
Suppose ingetumia 100 billions na kuonyesha tuu the potrait photo ya Samia, kama ilivyo picha ya Mona Lisa iliyochorwa na Leonardo Da Vinci, na hizo billions sio zetu ni za mfadhili wa kujitolea, kuna tatizo gani?...
Hayo ni mawazo na imani yako kama Pascal Mayalla.Na kama kwako wewe ni kushukuru zaidi ya kuhoji uhalali wa kuyaficha majina ya hao wafadhili.

Wewe endelea kushukuru na kusubiri shukurani za kushukuru.

Mimi kama ni kushukuru nitamshukuru huyu mzungu aliyejitolea kutoka huko kwao na kuja kutumia muda na pesa zake kuitangaza Tanzania huku,akiwa hajaficha jina lake !

Watanzania ndio taufa pekee ambako tunamshukuru Rais badala ya kumkumbusha wajibu wake kwa walipa kodi.
 
Kama nchi hii ingekuwa inatumia akili, wangetengeneza extended documentary ambayo ingekuw inarushwa kwa mwezi au miezi kibao, sasa mnatengeneza kapicha na kukazindua marekani mnarudi hapa bongo mmekaa tu.
Sidhani kama Ile ni documentary ya wanyama per se Ile ni branding tu ya Rais Samia na sababu yule jamaa alifanya Royal Tours na Marais kadhaa ndio maana na yeye kamtumia yule it's not about viewership ila aina ya documentary.

So hao washauri wa Rais walitaka wamtambulishe Samia kwa Dunia na sio kutambulisha wanyama kwa Dunia maana documentary za Serengeti zimejaa national geographic kila siku.
 
Mzee hapa umetoa boko.

Mimi ni mfuatiliaji mzuri wa National Geographic Channel zote 2.

Wana watu zaidi ya 2 billion viewers na subscribers, wana data base ya wataalum (exploreres, wild animal doctors, Ecologist, etc) Wana fund projects zaidi ya 15,000 kwa mwaka...
Mimi ndio maana nimeweka video mbili ili kudhihirisha kwamba,Royal Tour sio kitu ukiamua kufuatilia Documentary zingine huko National Geographic na kwingineko.

Lakini Tanzania tunalazimishwa kuamini Royal Tour ndio imeifungua Tanzania!
 
Sidhani kama Ile ni documentary ya wanyama per se Ile ni branding tu ya Rais Samia na sababu yule jamaa alifanya Royal Tours na Marais kadhaa ndio maana na yeye kamtumia yule it's not about viewership ila aina ya documentary. So hao washauri wa Rais walitaka wamtambulishe Samia kwa Dunia na sio kutambulisha wanyama kwa Dunia maana documentary za Serengeti zimejaa national geographic kila siku.
Na hayo ndio maneno sahihi ya kutumika pale inapotajwa Roya Tour Samia Version!
 
Back
Top Bottom