Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 359,928
- 828,569
Nilitoka Posta kwenye mishe zangu nikawa naelekea Sinza.. Na njia ambayo ingenifikisha kwa urahisi ni kupitia pale Magomeni Morroco then Tandale
Basi nikachukua njia hiyo, Ukiingia hiyo njia kwa mbele kuna shule ya msingi upande wa kushoto na mbele kulia kwenye kona kuna makaburi
Pembezoni mwa makaburi kuna njia inaingia mtaani.. Basi ikatoka Nissan Patrol damu ya mzee toka njia hiyo ya makaburini.. Kwa namna dereva alivyokuwa rafu kuingia main road ikabidi nimpe njia apite
Ile kuingia tu main road hakwenda hata hatua kumi kuna paka mweusi akadondoka barabarani toka chini ya uvungu wa gari na kukimbia kurudi makaburini
Nikakemea kimoyomoyo safari ikaendelea Nissan mbele Mimi nyuma
Kufika usawa wa Shule ya Salma Kikwete tukakuta gari zimesimama pande zote.. Mimi nilikuwa gari ya tatu nyuma.. Pale katikati ya barabara kulikuwa na kilinge cha kondoo saba.. Wawili walikuwa wamekaa chini na wengine watano wamewazunguka wenzao!
Mwanzoni nilidhani wale wawili walikuwa wamegongwa lakini baada ya kuwapita, maana ilibidi tutanue kushoto na kulia kuweza kupita, hapakuwa na ajali yoyote
Baada tu ya kupita naangalia mbele nakuta ile Nissan imeshatembea na kui overtake gari ya mbele
Mpaka sasa najiuliza kulikuwa na uhusiano gani kati ya yule paka mweusi Nissan na wale kondoo.
Basi nikachukua njia hiyo, Ukiingia hiyo njia kwa mbele kuna shule ya msingi upande wa kushoto na mbele kulia kwenye kona kuna makaburi
Pembezoni mwa makaburi kuna njia inaingia mtaani.. Basi ikatoka Nissan Patrol damu ya mzee toka njia hiyo ya makaburini.. Kwa namna dereva alivyokuwa rafu kuingia main road ikabidi nimpe njia apite
Ile kuingia tu main road hakwenda hata hatua kumi kuna paka mweusi akadondoka barabarani toka chini ya uvungu wa gari na kukimbia kurudi makaburini
Nikakemea kimoyomoyo safari ikaendelea Nissan mbele Mimi nyuma
Kufika usawa wa Shule ya Salma Kikwete tukakuta gari zimesimama pande zote.. Mimi nilikuwa gari ya tatu nyuma.. Pale katikati ya barabara kulikuwa na kilinge cha kondoo saba.. Wawili walikuwa wamekaa chini na wengine watano wamewazunguka wenzao!
Mwanzoni nilidhani wale wawili walikuwa wamegongwa lakini baada ya kuwapita, maana ilibidi tutanue kushoto na kulia kuweza kupita, hapakuwa na ajali yoyote
Baada tu ya kupita naangalia mbele nakuta ile Nissan imeshatembea na kui overtake gari ya mbele
Mpaka sasa najiuliza kulikuwa na uhusiano gani kati ya yule paka mweusi Nissan na wale kondoo.