Mkuu umemshauri sawa.
Changamoto kama hiyo niliishuhudia kwa dada mmoja muuza gongo mashuhuri hapa kitaa.
Alikuwa akishikwa mara kwa mara, anahonga na kuachiwa.
Ilifikia hatua akapewa masharti ya kudumu na huyo polisi aliyekuwa akimkamata mara kwa mara kwamba, ''wewe nimekukamata sana na hautaki kuacha hii biashara yako haramu, sasa hautaona sura yangu tena kwako.
Ukuniona elewa kuwa hautanihonga, ni jela moja kwa moja".
"Kuanzia leo sehemu yoyote tutakayoonana ama kukutana na wewe lazima utoe hela, yaani popote tukikutana, iwe sokoni, barabarani, kwenye sherehe, popote pale bila kujali tumeonana ama tumekutana mara ngapi kwa siku hiyo. Na kiwango cha kunipa hiyo shukrani yako ni kuanzia elf10 kuendelea''.
Yule mama alitoatoa mwishowe akanyenyua mikono. Faida yote ikawa inalambwa na yule polisi.
Sasa hivi namuona akiuza sokoni, katulia.
Kiukweli biashara haramu siyo. Itakugharimu sana bila faida ya maana yenye kueleweka.