Tujitafakari kwa kina: Vikwazo vya Mmarekani vina manufaa kwa siasa za Upinzani?

Nyankurungu2020

JF-Expert Member
Oct 2, 2020
4,086
6,568
Wanabodi wa JF hili ni bandiko linalohitaji majibu chanya kwa mustakabali wa taifa letu.

Maana kila kukicha wanasiasa wa upinzani wamekuwa na munkari wa kutaka nchi yetu iwekewe vikwazo hasa na taifa la marekani kwa kile wao wanafikiri kuwa ni msaada wa kwao ili kupata manufaaa ya kisiasa.

Mfano kipindi taifa ketu limegubikwa na matukio ya raia kutekwa na kupotea , serikali ya Usa wakati huo ilimuwekea zuio la kutoenda Usa aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda. Kwa ufupi wapinzani walifurahi sana maana waliona sasa hii kwao ni adhabu tosha kwa watesi wao. Usa ilienda mbali na kuweka zuio la watanzania wote kutocheza bahati nasibu ya green card kwa watanzania wasiende Usa kusaka maisha.

Pia baada ya uchaguzi kuisha wapinzani wamelalama sana na cha kushangaza serikali ya Usa wakati huo iliweka zuio kwa waliokuwa wasimamizi wa uchaguzi Tanzania bila kutaja majina yao wasikanyage Usa.

Je, haya mazuio ya kutokanyaga Usa yanayowekwa dhidi ya watanzania yana manufaa gani kwa upinzani mpaka wafuasi na viongozi wakenue meno nje? Je toka Paul Makonda awekewe ribiti kwenda USA Upinzani hapa Tanzania umenufaika na nini?
 
Wanaopiga kura ni wananchi! Vyama vya Upinzani viwe na mikakati ya kuleta ushawishi kwa wananchi na hasa vijijini ambako kuna wapiga kura wengi.

Hivyo vikwazo vya kutokwenda Marekani havisaidii kujenga demokrasia. Ikizingatia ni swala BINAFSI. Kwani Marekani ni Mbinguni kwamba usipoenda ndo utakwenda kuzimu? Hao walioambiwa wasiende Marekani hadi leo wamepungukiwa nini?
 
Wanaopiga kura ni wananchi! Vyama vya Upinzani viwe na mikakati ya kuleta ushawishi kwa wananchi na hasa vijijini ambako kuna wapiga kura wengi. Hivyo vikwazo vya kutokwenda Marekani havisaidii kujenga demokrasia. Ikizingatia ni swala BINAFSI. Kwani Marekani ni Mbinguni kwamba usipoenda ndo utakwenda kuzimu? Hao walioambiwa wasiende Marekani hadi leo wamepungukiwa nini?
Nashukuru kwa ufafanuzi mzuri.
 
Well, wewe unaishi maisha yako kwa kutegemea posho unazopata toka ccm., Ni wazi kwamba hufahamu chochote kuhusua Nchi maskini kama Tanzania kuwa na mahusiano mabaya na nchi za mataifa ya nje kama America na Ulaya.,

Takribani miradi yote iliyopo nchini ambayo saivi munajitapa ni ufadhili kutoka kwenye hizo nchi., huo ni mfano mdogo tu yako mambo mengi lakini hili la wapinzani kufurahia Tanzania inapowekewa vikwazo ni advantage ya kisiasa kwamba ccm na aila zao imeshindwa kuongoza nchi kwa haki na usawa na kwamba sasa dunia nayo pia imeelewa na kufahamu yale ambayo wapinzani wa Tanzania wamekuwa wakiyaonyesha kuhusu udhaifu wa hiyo munayoiita JMT.,

Sasa kama dunia imeyafahamu hayo kuna haja gani kuendelea na huo utawala, ndio mana wapinzani wanataka ku-take advantage ili kuondoa hilo gape na weknesses za Taifa kuhujumiwa na Watanzania kuondokana na umasikini uliokubuhu takriban miaka 57 sasa ambao umechangiwa pa kubwa na hizo tunazoziita ban kutoka kwenye Mataifa yaliyoendelea kama America na Ulaya.
 
Hujakomaa kiakili za kidipromasia na kifalsafa,nk.

Nchi ikiwekewa vikwazo vya kiuchumi, serikali inapewa adhabu yake ili iache mambo mabaya inayofanya,kama kuminya demokrasia,uhuru,na pengine ufisadi.

Je,hivi vitu serikali ikikoma kuvifanya,vyama vya upinzani havitapata faida?

Na je,nchi kama Tunisia, Misri na Libya, wapinzani walipata faida gani baada ya Marais wa nchi hizo kupndolewa madarakani kwa nguvu na USA na majeshi ya NATO?

Wewe bado mtoto wa secondary school,haya mambo hata serikali ya Tanzania inayajua vizuri, siyo kama unavyojua wewe.Ukikua utayaelewa.
 
Well, wewe unaishi maisha yako kwa kutegemea posho unazopata toka ccm., Ni wazi kwamba hufahamu chochote kuhusua Nchi maskini kama Tanzania kuwa na mahusiano mabaya na nchi za mataifa ya nje kama America na Ulaya...
Acha kashfa za kipuuzi. Nani anapata posho toka Ccm?

Kwa akili yako finyu Tanzania ina uhusiano mbaya na Usa?

Upinzani umenufaika nini na hivi vikwazo vya kuzuia watanzania kwenda usa?
 
Well, wewe unaishi maisha yako kwa kutegemea posho unazopata toka ccm., Ni wazi kwamba hufahamu chochote kuhusua Nchi maskini kama Tanzania kuwa na mahusiano mabaya na nchi za mataifa ya nje kama America na Ulaya...
Asante kwa kumwelewesha huyo msaka vyeo. Inaonekana ni kijana wa form 4 au6 tu hivi. Bado anasoma concepts.
 
Acha kashfa za kipuuzi. Nani anapata posho toka Ccm?

Kwa akili yako finyu Tanzania ina uhusiano mbaya na Usa?

Upinzani umenufaika nini na hivi vikwazo vya kuzuia watanzania kwenda usa?
Soma dhana ya international relations na diplomacy,acha kutumia plain knowledge.
 
Wanaopiga kura ni wananchi! Vyama vya Upinzani viwe na mikakati ya kuleta ushawishi kwa wananchi na hasa vijijini ambako kuna wapiga kura wengi. Hivyo vikwazo vya kutokwenda Marekani havisaidii kujenga demokrasia. Ikizingatia ni swala BINAFSI. Kwani Marekani ni Mbinguni kwamba usipoenda ndo utakwenda kuzimu? Hao walioambiwa wasiende Marekani hadi leo wamepungukiwa nini?
Bado unayo yale mawazo eti wapiga kura wengi wako vijijini.
Ni kweli Mtaa wa Congo wamejaa wamachinga wengi saana na kila siku wanaingia Dar kutoka huko vijijini hapo bado huja angalia miji mingine.
Anyway bakia huko huko.
 
Faida si kwa wapinzani bali ni kwa taifa zima. Utekaji, utesaji, mashambulizi ya risasi na mauji yakikoma ni faida kwa taifa!
Yawezekana kabisa katika fikra za watawala na wanaCCM wa sasa, wapinzani kwao si Watanzania na hawasitahili heshima na utu.
Kwa kuwa Watawala na wanaCCM wamegeuka na kuwa wanyama hatari, basi waendelee kuwekewa vikwazo labda watakuwa binadamu tena, na taifa litapona.
 
Back
Top Bottom