Mkuu Kiswahili ni Lugha ngumu sana. Watanzania wengi hawaielewi hasa katika kuandika. Pia kuna lafudhi ambazo zinatuathiri katika matamshi na maandishi ya kiswahili. Wachaga wengi hawawezi kutamka neno nchi lazima atatamka nji! Mhaya hawezi kutamka neno ng'ambo yeye atakuambia ngambo! Mbondei atakutamkia kupunzika badala ya kupumzika. Mkurya hana kitu kinachoitwa la yeye kulala atakutamkia/kuandikia kurara.
Mkuu ndiyo lugha yetu hiyo pamoja na lafudhi zetu. Wengine pia unakuta wako nje ya Tanzania muda mrefu hivyo hata matamshi yanakuwa tabu. Unajua tena raha ya lugha uinene kwa ngeri, vijazi na visifa.