jimmygatete
JF-Expert Member
- Aug 30, 2022
- 2,698
- 5,909
Kama Mada Inavyosema.
Mimi nimekulia Morogoro na nimecheza sana ndondo miaka ya late 1990's na 2000's nikitokea timu ya Ghetto Boys ya Mvomero.
Katika makuzi yetu tulikuwa tunacheza sana ndondo huko Mvomero na Moro kwa Ujumla na katika mashindani ya Kiwilaya na Mkoa tulikuwa tunakutana na timu za Wilaya nyingine au mikoa mingine pale uwanja wa shujaa Morogoro Mjini.
Timu nyingi zilitoa wachezaji wa iliyokuwa ligi daraja la Kwanza sasa Ligi Kuu mfano Reli, Moro United, Mtibwa Sugar n.k za Moro na nyingine nyingi za nje ya Moro kama Prisons, AFC, Simba na Yanga n.k.
Wachezaji maarufu wa Ndondo ambao binafsi nimewashuhudia na kimsingi walikosa njia nzuri tokana na "Zama za giza tulizokuwa tunacheza na kizazi," ila wangekuwa wachezaji bora nchini na duniani kama wangecheza sasa ni kama wafuatao:
1. David Izengo-Toka timu ya Magereza huyu kwangu mimi ni mchezaji bora kumshuhudia kwa macho yangu nchini sema zama alizokuwa ziliua kipaji chake akaja cheza Prison. Hapa "Triple C" hamfikii.
2. Paul Mokiwa alicheza reli Morogoro na baadaye Prison ambapo alipata majeraha na kuacha kucheza Mpira.
3. Ramadhani Lundenga. Alikuwa ndugu na Hashimu Lundenga na alikuja chezea Yanga B.
4. Abu Ramadhani alikuja chezea Yanga.
5. Salum wa Gheto Boys ya Mvomero
6. Mimi Jimmy Gatete a.k.a mungu ya Magoli toka ghetto boys ya Mvomero.
7. Kipa Maarufu wa Ndondo Yusuph Dezo toka Timu ya Kishingo ya Dakawa pale alikuwa anampiga mikwara Kaseja kuwa yeye Kaseja ni "Tanzania 2" mbele yake naye ni "Tanzania 1" ila mfumo tu umembeba.
Timu maarufu za Ndondo Moro ninazozifahamu na tulizokutana nazo kwenye michuano mbalimbali ni:
1. Jamaica ya Moro Mjini.
2. Young Boys ya Mikese.
3. Jiwe ya Dumila.
4. Ghetto Boys na Asec za Mvomero.
5. Burkina ya Moro Mjini.
6. Kulikuwa na timu moja ya Kihonda waliyokuwa wanachezea akina Ulimboka Mwakingwe, Jumanne Shengo Tondoro na akina Kaseja siikumbuki vizuri.
7. Kulikuwa na timu moja toka turiani iliyokuwa ina wachezaji toka mtibwa kipindi hiko akina Mkangwa, salhina mjengwa, Zuberi Katwila, Mecky n.k
Je, wewe unaikumbuka timu gani maarufu ya ndondo ya mtaani kwenu na wachezaji maarufu waliokuwa wanaichezea?
Nakumbuka Dar walikuwa na Abajalo ya Sinza waliyocheza akina "Kali Mangonga Ongara Mbele kwa Mbele."
Mimi nimekulia Morogoro na nimecheza sana ndondo miaka ya late 1990's na 2000's nikitokea timu ya Ghetto Boys ya Mvomero.
Katika makuzi yetu tulikuwa tunacheza sana ndondo huko Mvomero na Moro kwa Ujumla na katika mashindani ya Kiwilaya na Mkoa tulikuwa tunakutana na timu za Wilaya nyingine au mikoa mingine pale uwanja wa shujaa Morogoro Mjini.
Timu nyingi zilitoa wachezaji wa iliyokuwa ligi daraja la Kwanza sasa Ligi Kuu mfano Reli, Moro United, Mtibwa Sugar n.k za Moro na nyingine nyingi za nje ya Moro kama Prisons, AFC, Simba na Yanga n.k.
Wachezaji maarufu wa Ndondo ambao binafsi nimewashuhudia na kimsingi walikosa njia nzuri tokana na "Zama za giza tulizokuwa tunacheza na kizazi," ila wangekuwa wachezaji bora nchini na duniani kama wangecheza sasa ni kama wafuatao:
1. David Izengo-Toka timu ya Magereza huyu kwangu mimi ni mchezaji bora kumshuhudia kwa macho yangu nchini sema zama alizokuwa ziliua kipaji chake akaja cheza Prison. Hapa "Triple C" hamfikii.
2. Paul Mokiwa alicheza reli Morogoro na baadaye Prison ambapo alipata majeraha na kuacha kucheza Mpira.
3. Ramadhani Lundenga. Alikuwa ndugu na Hashimu Lundenga na alikuja chezea Yanga B.
4. Abu Ramadhani alikuja chezea Yanga.
5. Salum wa Gheto Boys ya Mvomero
6. Mimi Jimmy Gatete a.k.a mungu ya Magoli toka ghetto boys ya Mvomero.
7. Kipa Maarufu wa Ndondo Yusuph Dezo toka Timu ya Kishingo ya Dakawa pale alikuwa anampiga mikwara Kaseja kuwa yeye Kaseja ni "Tanzania 2" mbele yake naye ni "Tanzania 1" ila mfumo tu umembeba.
Timu maarufu za Ndondo Moro ninazozifahamu na tulizokutana nazo kwenye michuano mbalimbali ni:
1. Jamaica ya Moro Mjini.
2. Young Boys ya Mikese.
3. Jiwe ya Dumila.
4. Ghetto Boys na Asec za Mvomero.
5. Burkina ya Moro Mjini.
6. Kulikuwa na timu moja ya Kihonda waliyokuwa wanachezea akina Ulimboka Mwakingwe, Jumanne Shengo Tondoro na akina Kaseja siikumbuki vizuri.
7. Kulikuwa na timu moja toka turiani iliyokuwa ina wachezaji toka mtibwa kipindi hiko akina Mkangwa, salhina mjengwa, Zuberi Katwila, Mecky n.k
Je, wewe unaikumbuka timu gani maarufu ya ndondo ya mtaani kwenu na wachezaji maarufu waliokuwa wanaichezea?
Nakumbuka Dar walikuwa na Abajalo ya Sinza waliyocheza akina "Kali Mangonga Ongara Mbele kwa Mbele."