Tujikumbushe MV Bukoba enzi za uhai wake

Nilikutana na Nahodha wake(Jumanne Rume Mwiru) kwa mara ya kwanza mwaka 2008.

Katika kupiga stori naye, akasema ile meli ilikuwa kubwa sana, anasema alikuwa anaiendesha(operate) akiwa amesimama maana uskani wake ulikuwa mkubwa mno hadi usimame ndio unaweza kuuzungusha.
Yaani pamoja na kukutana na huyo mtu muhimu kwa hii taarifa ukaishia kupiga nae stori kuhusu ukubwa Wa usukani tu? Ulipaswa utuletee episode kadhaa juu ya ile ajali ndugu. Au kama alikueleza zaidi tupe na sisi
 
Kwa msio jua meli ilipinduka ndio ikazama, yaani kichwa chini mi guu juu!!

Hii meli ilikuwa imejaza kupita kiasi na ilikuja upande upande toka bukoba!!

Na ijulikane meli ya victoria na iyo mv bukoba zina sehemu ya kukaa abiria chini kabisa wanaziitaga third class sasa ilipo binuka watu walikua wanagonga kitako cha meli wakiwa ndani ya meli kuomba msaada, ndipo wakaja na wazo watoboe kwenye kitako ili wawatoe kumbe ndio wanaizamisha!!

Izo third class ambazo ndio wengi ujazana huko zinatisha aisee, yaani meli ikiwa inaenda mnakuwa tayari mshazama kama ikotoboka chini, maji yanaanzia kwenu!! Kunakuwa na ngazi mnaingia huko chini kabisa aisee yaani hata kama meli ina kwangua chini mnaisikia!! Wameweka siti.
Duuuu
 
Nimewahi kufanya safari na hii meli mara kadhaa siku za hapo nyuma, Ukweli hii meli ilikuwa si chakavu, Mimi ni mvuvi wa siku nyingi sana, moja ya mambo ambayo avitakiwi ukiwa ziwani ni vitendo vyovyote vya kufanya ngono majini, binafsi ktk safari ndani ya meli hiyo nikiwa ninasafiri nimeshuhudia mara kadhaa abiria wakitenda matendo hayo! Majini huwa kuna majini awapendi huo uchafu, Pia mbali ya idadi kubwa ya watu siku ya tukio la kuzama hiyo meli, Abiria kuelekea upande mmoja nayo ni moja ya sababu ya kutokea maafa siku ile ya tukio la MV Bukoba,pamoja na kwamba siku ile ya tukio hali ya ziwa ilikuwa shwali.

Kwaiyo watu waache kutianaa kisa majini ? Ingekuwa Mungu sawa, ila majini nop, waendelee tu kukazana ... Dunia ni ya Mungu sio majini.. Akikataa Mungu sawa ila sio jini
 
Yaani pamoja na kukutana na huyo mtu muhimu kwa hii taarifa ukaishia kupiga nae stori kuhusu ukubwa Wa usukani tu? Ulipaswa utuletee episode kadhaa juu ya ile ajali ndugu. Au kama alikueleza zaidi tupe na sisi
Kwanza kabisa alikuwa ni mtu wangu wa karibu kipindi hicho nakutana naye, alikiwa ni miongoni mwa wenyeji wangu. Sikuwa na haraka ya kumuuliza kisa cha Meli kuzama maana nilijua atanisimulia siku za mbeleni wakati nikiendelea kuishi sehemu hizo.

Kabla sijafanya ajizi nikaanza mishe zangu sehemu fulani hapo jijini Mwanza na yeye ghafla akaanza kuugua na akaanza kupata matibabu pale Bugando. Nikawa naenda kimsalimia nikiwa na mawazo ya kufikiria juu ya kuugua kwake na nikaelekeza fikra zangu kumliwaza kama ilivyo kawaida ya wagonjwa kuliwazwa na kufarijiwa.

Kadri siku zinavyozidi kwenda hali ikawa mbaya zaidi, kufika mwezi wa 6 mwaka 2009 akawa ameaga Dunia.

Kutopata simulizi ya kisa cha Meli kuzama ni kosa ambalo limelifanya baada ya kukutana na Marehemu mzee Rume.
 
We jamaa umesoma nyanza na umekaa nera?!!the same to me


96 ulikua darasa la ngapi kama la pili itakua we ni classmate wangu tena from the same neighborhood!!!

Nakumbuka tulikua tunakaa kwenye kile kimlima juu(nera)kinachoangalia ziwani kuangalia zoez la uokoaji coz shule ilifungwa due to huo msiba wa kitaifa
Mv bukoba kuna kipindi miaka ya tisini mwanzoni ilikuwa inaenda musoma pia,tukiwa wadogo tuliipanda,nakumbuka kwenye meli walikuwa wanakataa watoto wachanga kulia eti itazama,sifa nyingine ilikuwa inasafiri kiupande upande kama imeelemea upande mmoja!

Siku inazama pale shule ya nyanza primary mapema tulipata taarifa,sie tuliokuwa tunakaa nera kando ya ziwa,kuna muda miili ilikuwa unaikuta ufukweni mwa ziwa ukienda kupiga mswaki "bichi"
Ilikuwa hatari sana tulimpoteza mwanafunzi mwenzetu wa nyanza ali mwarabu na familia yake wakitoka harusini,pia imam wa kwanza wa masjid al asais makongoro nae mauti yalimkuta humo!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwanza kabisa alikuwa ni mtu wangu wa karibu kipindi hicho nakutana naye, alikiwa ni miongoni mwa wenyeji wangu. Sikuwa na haraka ya kumuuliza kisa cha Meli kuzama maana nilijua atanisimulia siku za mbeleni wakati nikiendelea kuishi sehemu hizo.

Kabla sijafanya ajizi nikaanza mishe zangu sehemu fulani hapo jijini Mwanza na yeye ghafla akaanza kuugua na akaanza kupata matibabu pale Bugando. Nikawa naenda kimsalimia nikiwa na mawazo ya kufikiria juu ya kuugua kwake na nikaelekeza fikra zangu kumliwaza kama ilivyo kawaida ya wagonjwa kuliwazwa na kufarijiwa.

Kadri siku zinavyozidi kwenda hali ikawa mbaya zaidi, kufika mwezi wa 6 mwaka 2009 akawa ameaga Dunia.

Kutopata simulizi ya kisa cha Meli kuzama ni kosa ambalo limelifanya baada ya kukutana na Marehemu mzee Rume.
Doooh Sawa ndugu,pole pia kwa kuondokewa na jamaa aisee japo ni kitambo.
 
Kipindi hicho Mwanza hakukua na simu za mkononi, mobitel ilianza huku mwaka 1997 na Mwanza nzima walikuwa na mnara mmoja tu kule juu ya ghorofa la 10 Bugando. Hao waliobeba mitungi ilikuwa ni timu ya uokoaji iliyokuwa na baraka za mamlaka husika.

Siku hiyo tukiwa tumetoka mapumziko ya saa 4 shule ya msingi Bugando tuliona magari mengi yakiwa yamebeba watu yakipanda mlima kuwahi Bugando hospital na tukasikia watu wakubwa wakisema kuna meli imezama.

Tulipotoka darasani saa 8 mchana mwisho wa vipindi darasani mimi sikusubili mpaka tutawanyishwe nilikimbia mpaka Kastam kwa maana ya bandarini kwenda kushuhudia kinachojili. Pale nilikuta watu wengi sana na wengine wanamitungi ya gas iliyokuwa imepelekwa kutobolea meli wakiwatangazia watu kuwa wametoka eneo la ajari wakiacha meli imezama na kutoonekana kabisa. Hapo umati ulianza kutawanyika na wengine kukimbilia Bugando hospital kuona maiti na walionusurika.

Maiti zilizo oza liliwekwa pale Nyamagana stadium ili ndugu waende kuzitambua na zile zilizokosa ndugu zilipelekwa kuzikwa Igoma kwenye kiwanja maarum.
Kwa dar mobitel ilianza mwaka gani?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakati ilikuwa hiv
9dd77946cc154f56bd09416a8abaa2e0.jpg
Si lenyewe hili bwanaaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yaani pamoja na kukutana na huyo mtu muhimu kwa hii taarifa ukaishia kupiga nae stori kuhusu ukubwa Wa usukani tu? Ulipaswa utuletee episode kadhaa juu ya ile ajali ndugu. Au kama alikueleza zaidi tupe na sisi
Ile meli nilikuwa naipanda toka niko form one had kidato cha nne ilipozama haikuwa kubwa kihivyo.Meli kubwa zaidi ni MV Victoria.Zote nimezipanda.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kiliniuma sana wale wanafunzi wasichana wa Rugabwa waliokuwa wamemaliza kidato cha sita wote waliteketea; walivyoona sasa wanakufa walishikana wote kuagana kwa safari ya milele - too sad.
Tulisalia wachache ambao hatukupanda meli ile
 
Tupe historia Kidogo ilkuaje na vipi maisha baada ya ajali, kwan naambiwa mtihani ulipoteaa ikabdii kuurudia

Sent using Jamii Forums mobile app
Yes tulirudia mitihani kwa sababu ya awali ilizama katika meli. Katika darasa la watu 58 tulibaki 26. Tulirudi shule kabla hawajafungua likizo ya June. Kufanya mitihani ukiwa kwenye tension ya kupoteza wenzio na kwamba huna materials za kujisomea na wakati huo mko wachache sana shuleni ilikua changamoto lakini lilipita na maisha yanaendelea.
 
Back
Top Bottom