Tujikumbushe Mabasi ya abiria ya zamani tokea tupate uhuru

Suleiman Roadways, Upendo, Katule Obamka, Desert Line, Kwacha, Katiba,...
 
Naona kuna mchanganyiko wa mabasi kati ya 80s na 90s, na kidogo late 70s. Katika miaka ya 70-80s KAMATA na Relwe ndio walitawaala katika kusafirisha abiria, aidha waliweza kuwa na huduma za luxury, Express na Ordinary.

Kwa mfano, KAMATA walikuwa na watoa mabasi mawili kila siku toka Arusha kwenda Dar. Moja likiondoka saa kumi jioni (ordinary) na lingine likiondoka saa mbili usiku(luxury). Hili la kuondoka usiku ndio liliokuwa likiwahi kufika Dar, kati ya saa moja asubuhi au saa mbili.

Baada ya kuanza kuingia kwa mabasi mengine Arusha ilishuhudia kuongezeka kwa mabasi ya Luxury kama vile Imam na Rafiki ambayo nayo yalikuwa yakitoka saa mbili usiku na kuwahi kuingia Dar mapema asubuhi, huku yakiyapita mabasi ordinary ya saa kumi kama vile Bon City, Ngorika, Masama Cliff na mengine kadha wa kadhaaa...

Kweli Mimi nilikosa nafasi Kamata nauli Tzs 110/= nikapanda Imam kwa
Tzs250/= kwenda Dar toka Ar kati ya Mwaka 1983/85 wakati huo nasoma Pugu High School.
 
Kwa iringa kulikuwa na Embakasy Nyuma iliandikwa ' Che wililye che Chako"

Mabasi yanayoenda Mbeya yanayoitwa KWACHA pia ya RAILWAYS ya shirika la reli.Wakati Mwaka 1985 naenda JKT-Mafinga nilipanda KWACHA pale Mnazi mmoja ndio Stendi yao.
 
1.SAN ABACHA-Ubungo Posta
2.City Bus-Ubungo Posta
3.Special Coach-Ubungo-Mkoa
4.Kiswele-Ubungo - mkoa
 
nakumbuka nshawahi kutana na bus imeandikwa "iga ufe kwa supu ya mawe"
 
Enzi hizo ulishawahi kupita na basi hapa? Ilikuwa ukifika hapa ni kasheshe au faraja.

DSC00625%5B4%5D.jpg

Duh..kunyumba huko...!!
 
Kwa wale waliozaliwa au kuwepo Dar miaka ya 80s watakumbuka usafiri wa UDA kwa kutumia mabasi ya Ikarus 'kumbakumba'.

Mimi nilikuwa napenda kukaa pale kwenye maungio kwa kweli nimekumbuka mbali sana enzi hizo mji msafi,watu wastaarabu kila kitu kiko kwenye mpangilio na wanafunzi hawanyanyaswi, DART wanataka kuleta mabasi aina hii, ya kisasa zaidi.

Kwa wale waliokuwepo hebu tupeni experience yenu.

IMG_7497.jpg

Teh teh sijui inaandikwaje kwa lugha yake ila mie nakumbuka tulikuwa tunaita HEKALUS.
 
Hivi mabasi ya zamani yalikuwa mabovu mabovu sana, lakini mbona yalikuwa hayachinji watu kama haya ya sasa ambayo yanaonekana kuwa ya kisasa na bora zaidi? Mie hata sikumbuki kama kulikuwa na suala la basi kupasuka tairi, kuacha njia nk.

Au madereva?
 

Hii photoshop. Iweje basi la UDA lina usukani kushoto, linaendeshwa upande wa kulia wa barabara, lina endeshwa na mzungu, halina namba za usajiri, linakatisha mitaa ambayo sijawahi kuiona Dar, mtaa ukiwa na miti inayostawi sehemu za baridi?
 
Back
Top Bottom