Tujikumbushe kauli hii ya Mzee KINGUNGE

Huwa sielewi, sijui tumelogwa? mbona hawa watu wakiisha toka kwenye system ndo huwa na mawazo mazuri? Nakumbuka Sumaye naye sikumoja aliwahi kusema, taifa haliwezi kuendela kama hatuuzi vitu nje ya nchi, kama tunanunua zaidi bila uuza then hatutakuwa na fedha za kigeni, aliendelea zaidi kwa kudai tujenge zaidi viwanda ili tupate vitu vya kuuza, ni huyu hyu aliyekuwa waziri mkuu wa muda mrefu kupita yeyote aliyewahi kukalia kiti hicho, swali, kwanini viongozi wengi wa magamba huwa wanaona kikwazo cha matatizo yetu mara baada ya kuachia madaraka?

Bila kujali historia yake huyo mzee (ambayo kwakweli huwa nasikia kichefu chefu, hasa baadhi ya kauri zake) aliyo yasema ndio ukweli, hivi mwaka 1988 pale kambi ya jeshi kibaha, wanajeshi wale (mainjinia) si waliweza kutengeneza Gari na wakalipa jina la Nyumbu? nakumbuka liliingia hadi kwenye maonesho ya sabasaba, enzi hizo maonesho yale yalikuwa na mvuto sana, hivi kama akina kingunge wangewaendeleza watu wale, leo situngekuwa tunatengeneza ndege? CDM, mkiingia madarakani 2015, endelezeni hili tafadhari!

Huwa ata mimi hii hali inaniweka ktk wakati mgumu sana kuwaelewa hawa viongozi,wanazungumza mipango mizur sn wakishatoka madarakani.
 
Silly politicain. Alifanya NINI kuwashauri CCM kuendeleza Mang'ula, Kilimanjaro Machine Tools na SIDO? Huko ndiko Nyerere alioana kuna maendeleo ya Nchi. Kingunge na CCM yake wakaona ni Biashara! Hawa hawana tofauti na Sultani Mangungo w Msowero!
 
Hivi huyu mzee mpaka leo bado ni mbunge wa kuteuliwa na Rais?
Ni kweli amezeeka, lakini tusimpuuze! yapo mengi ya kujifunza kutoka kwake, mazuri yatatusaidia kufika tunapotaka, mabaya? yatatusaidia kufanya mazuri. Tusiwadharau hawa wazee wanavitu vya kujifunza.
 
​samahani kingunge ni nani?
Maoni ya Mzee Kingunge alipoulizwa kwa nini anafikiri Afrika bado iko nyuma!

Alisema

" Wakati wazungu walipofanikiwa na mapinduzi ya viwanda waasia wakajiuliza (wajapani) hivi ni nini siri ya mafanikio yao (yani wazungu) wakagundua kwamba siri yao iko kwenye maarifa, wakajifunza maarifa na wakatoka, wakaja wakorea wakajiuliza swali hilo wakagundua kwamba ni maarifa wakaiga wakatoka, wataiwani na wasingapore hivyo hivyo na sasa wachina nao wamegundua siri ya wazungu ni maarifa wameiga wanatoka ila Afrika akasema TUNAFIKIRI SIRI YA MAFANIKIO YA MZUNGU IKO KWENYE LUGHA YAKE NA RANGI YAKE kwa hiyo tunafanya kila tuwezalo kuwekeza katika hayo mambo mawili na ndio kilichotufikisha hapa tulipo"

Hayo ni maneno ya Mzee Kingunge, nini maoni yako, unaafiki naye?
 
​samahani kingunge ni nani?

Kama hujawahi kulisikia hilo jina hata nikianza kuelezea historia yake haitasaidia kitu! Kwa kifupi ni Mzee mtanzania aliyetoa maoni yake kuhusu nchi na Bara lake kwa ujumla!
 
Ni aibu kubwa sana kwa mtu ambae ametumikia umma kwa muda wa maisha yake yote kuja kujua kuwa alichokuwa akikifanya hakikuwa sahihi. Mbaya zaidi amejua hili wakati hana uwezo tena wa kuchangia kubadili uelekeo au mtazamo na fikra za watu wake.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom