Tujifunze BBMA strategy

Tujifunze BBMA strategy

The Master pizo

Senior Member
Joined
Dec 18, 2019
Posts
149
Reaction score
125
Habari za asubuhi wandugu poleni kwa majukumu ya hapa na pale Mungu atawapigania Siku yenu itakuwa njema kabisa.
Tuwaombee Dua wagonjwa wote waweze kupata nafuu na kurejea kwenye shughuli za kunufaisha familia.

Basi baada ya kutakiana Heri naomba leo nilete uzi ambao nitafundisha BBMA strategy kuanzia mwanzo kabisa na nitajitahidi tuimalize, Hii ni kwa wale wenye elimu ya basic ya forex na niwasihi sana usianze kusoma strategy kama hujui basic utapoteza pesa yako.

BBMA
BOLINGER BAND & MOVING AVERAGE


=> Strategy hii hii pia inafahamika kwa jina la GURU strategy
=> Mwanzilishi wa strategy hii anafahika kwa jina la OMA ALLY mtu wa Malaysia huko

BOLINGER BAND
=>Bolinger band ni indicator yenye mistari mitatu.
(a) Top Bolinger band {TBB}
=> Hii hutumika kama Resistance
(b) Middle Bolinger band {MBB}
=> Hii hutumika kugawanya uptrend na downtrend {increase and decrease}
(c) Lower Bolinger band {LBB}
=> Hii hutumika kama Support

tazama picha hapo chini
1603433175478.png



HIVYO
=> Candle zikiwa zinatembea juu ya middle bollinger band hiyo ni Uptrend na zikiwa zinatembea chini ya middle bollinger band hiyo ni downtrend
=> Kiujumla BB ni technical tool ambayo inatumika kama dynamic Support and Resistance.
WHY DYNAMIC?
=> Because BB lines changes according to the power of the market
=> BB ina sheria inayoitwa BOUNCE
Bounce ni kudunda kwa kitu ila katika BB tunaiangalia kwatika price yaani Price huwa haivuki nje ya BB lines.
=> The fact is BB lines are Zones na zones siku zote zina tabia ya kureject price.
tazama picha chini
1603434126642.png



=> So candle zitakuwa zinatembea ndani ya TBB na LBB
=> Ikitokea zimevunja BB yaani zimefungia nje ya BB kuna jambo ambalo litatokea
kumbuka hizi ni zones na zina tabia zote za zones
{1} Ku acttract price toward it.
{2} Baada ya ku acttract price ikifika karibu yake zone inafanya usaliti au tunasema inafanya price rejection inaisukuma price irudi ilikotokea.


WAJUBA TUTAENDELEA ................
 
Somo zuri... ICT itakuwa lini mkuu..?
What about stop loss..?
 
sijamaster ICT tutadili na BBMA na MMM ambazo zinakaribia kisha huko mbeleni tutaona namna ya kuweka zingine zaidi
Ulete na picha za profit isijekuwa wapaka watu mafuta kwa mgongo wa chupa wakiingia wakaume meno huko..😂

Sio unatuandikia tu kumbe usikute inakugaragaza.. Sasa hivi watapiamlo watakuja kukukandia..😅
 
Ulete na picha za profit isijekuwa wapaka watu mafuta kwa mgongo wa chupa wakiingia wakaume meno huko..😂

Sio unatuandikia tu kumbe usikute inakugaragaza.. Sasa hivi watapiamlo watakuja kukukandia..😅
mimi sio mtu wa show off mzee natoa kile nilichonacho na sipo humu kudai pesa ya mtu wala kumbembeleza mtu.
profit ipo
loss zipo
mnababaishwa na wale wanaotuma profit za kubahatisha na loss za mazoea 🤣 🤣 🤣 hii biashara sio ya lele mama ni ujitoe ufahamu asee kusoma sana

sasa hao raia wanaokujaga kuibia wenzao kwa profit huwa tunawazingua sana ndio maana kwenye channel yetu telegram tunafundisha free tena kwa zoom kila mtu anaruhusiwa kujoin na kuchangia
sasa hapo ndio ujue nani yupo kwa show off na yule anayetoa alichonacho
 
mimi sio mtu wa show off mzee natoa kile nilichonacho na sipo humu kudai pesa ya mtu wala kumbembeleza mtu.
profit ipo
loss zipo
mnababaishwa na wale wanaotuma profit za kubahatisha na loss za mazoea 🤣 🤣 🤣 hii biashara sio ya lele mama ni ujitoe ufahamu asee kusoma sana

sasa hao raia wanaokujaga kuibia wenzao kwa profit huwa tunawazingua sana ndio maana kwenye channel yetu telegram tunafundisha free tena kwa zoom kila mtu anaruhusiwa kujoin na kuchangia
sasa hapo ndio ujue nani yupo kwa show off na yule anayetoa alichonacho
Okay endelea kuleta mambo.
 
Tuendelee...............

BB INA TABIA TATU 3
{1} Expansion
{2} Constriction
{3} Consolidation / side way / Horizintal movements

{1} EXPANSION (KUTANUKA)
=> Hii ni tabia ya BB ambayo inasababishwa na kuongezeka kwa movements au liquidity ya soko either kwa kupanuka kwa juu au kwa kushuka chini.

=> BB zinapotanuka ina maana movement ya soko inazidi kuwa kubwa au pia tunasema soko lime gain momentum.

{2} CONSTRICTION (KUSINYAA)
=> Hii ni tabia ya kusinyaa kwa BB iwapo nguvu ya soko inapungua hapa ndipo mahali ambapo trader wengi huchukua profit zao
WHY??
=> kwa sababu movement inapopungua mara nyingi soko huwa linafanya side way / horizontal movement kwa ajili ya kukusanya contract nyingine za buyers au sellers ili liweze ku establish movement nyingine.

{3} CONSOLIDATION
=> Hii ndio side way movement yenyewe, ambapo soko linakuwa linatembea katika Range kwa kushuka na kupanda kutoka eneo A kwenda B na kisha kutoka B kurudi A

=> Market maker wanakusanya contracts nyingi kisha kufanya movement kubwa.
tazama picha chini
1603447948739.png
 
mimi sio mtu wa show off mzee natoa kile nilichonacho na sipo humu kudai pesa ya mtu wala kumbembeleza mtu.
profit ipo
loss zipo
mnababaishwa na wale wanaotuma profit za kubahatisha na loss za mazoea hii biashara sio ya lele mama ni ujitoe ufahamu asee kusoma sana

sasa hao raia wanaokujaga kuibia wenzao kwa profit huwa tunawazingua sana ndio maana kwenye channel yetu telegram tunafundisha free tena kwa zoom kila mtu anaruhusiwa kujoin na kuchangia
sasa hapo ndio ujue nani yupo kwa show off na yule anayetoa alichonacho
Naomba channel yenu ya telegram boss
 
Back
Top Bottom