Tujiajiri kwa kupitia wazo hili

Tujiajiri kwa kupitia wazo hili

MTOTO KITAA

JF-Expert Member
Joined
Oct 18, 2013
Posts
245
Reaction score
116
Wakuu
heshima kwenu, naomba vijana kumi, wenye laki tatu kila mmoja, lengo ni
kuunganisha nguvu ya mtaji kwa kuanzisha vyuo vinavyotoa certificate
kama vile zoom, the genesis n.k.

Naamini tutapata milion tatu, pia tukipambana huenda tukapata million
mbili na kufikisha tano hii ianaweza saidia kwa kuanzisha chuo. kumbuka
walimu tutakuwa sisi wenyewe na uongozi tutakuwa sisi wenyewe, hii
itategemea na proffesional yako.

Tutategeme kuanzisha ndani ya Dar au nje kidogo ya Dar hii inawezekana
kama tukiamua. kwa mawasiliano nipigie kwa 0757950376;kisha tutapanga
wapi pa kukutana tuweze kujadiliana juu ya kujiajiri sisi wenyewe,
asanteni.
UPDATE
kweli jf ni zaid ya ujuavyo..... ... mimi nilitegemea wadau mngekuja kuboresha wazo hili na kuweza kupata upana zaidi kwa lengo la kufanikiwa vijana wenzeni... nyinyi mnakuja kuponda na kutukana...eboo.... kwa hari hii vijana tutaendelea kuwa watumwa wa wachina na wahindi, na kamwe hatutauwona ufalme wa kaisari.kumbe nimegundua kitu kimoja... baadhi yetu huwa wanafurahi sana kuona vijana wenzao wanaangaika mitaani, ila kumbuka leo upo hapo, kesho haupo. anyway...kesho tunakutana na baadhi ya wadau, kujadili hili wazo. mida ya kukutana ni saa kumi kamili-hadi saa kumi na moja kamili jioni, tunakutana chuo cha udsm-maeneo ya nkrumah hall. TUTATHUBUTU ,TUTAWEZA NA TUTASONGA MBELE....OKOA TANZANIA.
 
Toa mchanganuo wa hizo m5 zitawezaje kuweka hiyo TREININGI SENTA...kwa mfano mimi ni mtu wa IT
 
Leo
ndo nimeamini JF kuna Mataperi dah

mkuu heshima kwako.... mi nilivyojiunga na jf, nilijuwa humu ndani kuna
greater thinkers... kumbe mburura wamejaa humu ndani... inaniita tapeli,
bila hata kufikilia... mimi sijasema mtu anitumie pesa yake... nimesema
kama unakiasi hicho cha pesa basi tukutaneni vijana kumi...tufanye huu
mradi... kwa sababu huwa mnawaza negative... na maisha yako yatakuwa
negative tu. onyesha ni wapi mtu anaweza kutapeliwa... mimi nipo
kazini..... ni nimetokea huo huko kwenye matatizo ya ukosefu wa
ajira.... so najua machungu ya kitaa... nimefikilia hili wazo kwa niaba
ya kuwakwamua wenzangu wa kitaa,,,,, so wewe unakuja kupiga kelele. so
bro jiheshimu ndugu. asante ila sitokata tamaa hata ukiongea. wadau
wakilipokea vyema.... tutalejesha mrejesho humu ndani. fikilia jambo
kubwa... hata kama unapesa ndogo... hata kama ikishikana hilo, bado
tunaweza anzisha shule za watoto, medium school kwa gharama hiyo hiyo
 
wakuu heshima kwenu, naomba vijana kumi, wenye laki tatu kila mmoja, lengo ni kuunganisha nguvu ya mtaji kwa kuanzisha vyuo vinavyotoa certificate kama vile zoom, the genesis n.k. naamini tutapata milion tatu, pia tukipambana huenda tukapata million mbili na kufikisha tano hii ianaweza saidia kwa kuanzisha chuo. kumbuka walimu tutakuwa sisi wenyewe na uongozi tutakuwa sisi wenyewe, hii itategemea na proffesional yako.. tutategeme kuanzisha ndani ya dar au nje kidogo ya dar. hii inawezekana kama tukiamua. kwa mawasiliano nipigie kwa 0757950376;kisha tutapanga wapi pa kukutana tuweze kujadiliana juu ya kujiajiri sisi wenyewe, asanteni

Mkuu hilo ni wazo zuri sana,ila hebu toa mchanganua mdogo wa hiyo idea ili watu waelewe,pia kuhusu jengo.la kufundishia,usajili,nadhani tungefanya kila mwenye million moja,ili.kifanyike kitu kilicho bora
 
Wazo zuri sana, ila changanua kiasi mchakato mzima na labda itachukua muda gani, mpaka kuanzisha hii project....
 
college kwa mnillion tano serious....mhhhhh ebu zikusanye hzo lak tatutatu mfuge kuku chuo tunadanganyana
 
college kwa mnillion tano serious....mhhhhh ebu zikusanye hzo lak tatutatu mfuge kuku chuo tunadanganyana

Iyo pesa inatosha kabisa...kusajiri mtaala ni million 1...kusajiri brela mpaka kufungua akaunti plus tra haizidi laki mbili.....ukishakuwa na usajili brela na umepitishiwa mtaala,unapewa usajiri wa majaribio....hapo unaruhusiwa kuoperate na kuwa na wanafunzi.....So iyo million 3 iliyobaki mnaweza kukodishia jengo na kuweka miundombinu....Hapo unaanza kukusanya laki nane zao.

Fanyeni kama mna nia msiogope.
 
Iyo pesa inatosha kabisa...kusajiri mtaala ni million 1...kusajiri brela mpaka kufungua akaunti plus tra haizidi laki mbili.....ukishakuwa na usajili brela na umepitishiwa mtaala,unapewa usajiri wa majaribio....hapo unaruhusiwa kuoperate na kuwa na wanafunzi.....So iyo million 3 iliyobaki mnaweza kukodishia jengo na kuweka miundombinu....Hapo unaanza kukusanya laki nane zao.

Fanyeni kama mna nia msiogope.

Una power of convising broooo
 
DOUBT! DOUBT! DOUBT!!! sijui utanisaidiaje hadi nikuamini??????????
wakuu heshima kwenu, naomba vijana kumi, wenye laki tatu kila mmoja, lengo ni kuunganisha nguvu ya mtaji kwa kuanzisha vyuo vinavyotoa certificate kama vile zoom, the genesis n.k. naamini tutapata milion tatu, pia tukipambana huenda tukapata million mbili na kufikisha tano hii ianaweza saidia kwa kuanzisha chuo. kumbuka walimu tutakuwa sisi wenyewe na uongozi tutakuwa sisi wenyewe, hii itategemea na proffesional yako.. tutategeme kuanzisha ndani ya dar au nje kidogo ya dar. hii inawezekana kama tukiamua. kwa mawasiliano nipigie kwa 0757950376;kisha tutapanga wapi pa kukutana tuweze kujadiliana juu ya kujiajiri sisi wenyewe, asanteni
 
we kweli ni mtoto. Embu tafuta wakubwa wakushauri kidogo!
 
we kweli ni mtoto. Embu tafuta wakubwa wakushauri kidogo!

Hili wazo ni zuri ila tatizo la watanzania wamezoea mawazo ya watu wengine ambayo wanadhani ni bora sana, hapa huyu jamaa ameleta idea cha msingi watu tungeangalia namna ya kuiboresha hii idea tu, watu wanakurupuka tu nakumuita tapeli bila ushahidi au aliwahi kumtapeli nani? Tatizo tunapenda kazi za kuajiriwa kuanzisha vyetu wenyewe tunaogopa risk sasa kwa mawazo haya ya kumaliza masomo na kusubiri kuajiriwa hii nchi itafika wapi?
 
Kaka mm ntakutafuta....watu wanaona laki tatu nyingi wakati wanatumia mamilioni kuponda raha clubs na ma bitch
 
Back
Top Bottom