Blaki Womani
JF-Expert Member
- Feb 28, 2011
- 11,228
- 13,448
Kongosho umenifurahisha jinsi ulivyoeleza.......mama hafananishwi na kitu kingine upendo anaokuwa nao kwa mwanawe hata wakati mwingine naangalia mafanikio/maisha niliyonayo nikimwondoa Mwenyezi Mungu muweza wa yote ni mama kwa sala na upendo dhati.Sijui unaupimaje huo upendo, ila kwa mtizamo wangu, hakun amtu amaewahi nipenda kama mama yangu. Na huwanasikitika kuwa japo nampenda, ila upendo wangu kwake hauwezi fikia upendo wake kwangu.
Na hii niliiona baada ya mie kupata watoto wangu, jinsi ninavyowapenda sitegemei wao wanipende vile. kwa nini? They take me for granted sababu wamezaliwa na kunikuta ninawapenda tu. Na wao wanaona nipo tu kwa ajili yao na siwezi kuondoka. Siwezi kumsemea saana baba, japo nakubali wapo kina baba wanawalea watoto wao utadhani wao ndio mama zao (cc Nyani Ngabu - Sijui kwa nini nahisi ni baba wa mfano)
Tofauti na mie sikuwa nao, ni kitu nimekifanyia kazi kukipata, kuanzia utungaji wa mimba, ukuaji wa mimba na mawasialiano kati yetu, mara kanichoma mbavu na kiwiko, mara anacheza mieleka, mradi tu mawasiliano yako juu juu.
I could not wait for them to come out nione product yangu. Na kitu cha kushangaza na kufurahisha ni kuona sura 2 katika mtu mmoja, my eyes, his nose, my lips, his ears. Kuanzia siku ya kwanza nilivyokiona kidogo kama ki samaki kimejaa mifupa kila mahali, i was so excited, ambavyo nilihangaika hata kukitoa kitandani nisijue la kufanya. Kumbukumbu hizo zote kwa pamoja zinajikusanya na kuwa upendo mkubwa ambao kwa tafsiri yangu ya sasa, sitegemei kupata upendo wa aina hiyo kwa mtu mwingine zaidi ya mama.
Labda kwa sababu mapenzi ya mzazi na ya mme/mke yanatofautiana.
Last edited by a moderator: