Tujadiliane hili tafadhali

Tujadiliane hili tafadhali

Heaven on Earth sio kwamba unatafsir kupendwa sana na mama kutokana na kufanya majukumu yake ambayo anaona asipoyafanya hakuna mwingne wa kuyafanya?
 
Last edited by a moderator:
kiukweli dada Fixed Point hili suala linatatiza sana kwa kweli ila nachoweza kusema ni kwamba upendo wa mama ni wa asili yaani hauna sababu maaluma kama muonekano labda au sauti ,rangi(vitu ambavyo vinachochea huu upendo mwingine kati ya me na ke au rafiki na rafiki).

Nachokimaanisha ni kwamba upendo wa mama hauzuiliki na hii ni kwa sababu ya hatua zote za kupatikana kwa mtoto mpaka kuzaliwa na kukua,mama anapokuwa na mtoto tumboni huhisi kuwa mtoto huyo ni sehemu ya mwili wake na hivyo tokea hapo ule upendo usio na sababu maalum huanza kukua na hata baada ya kuzaliwa ambapo bado mama huona kama mwanaye ni sehemu ya mwili wake na hivyo kumpenda sana katika hali yeyote kam ambavyo mtu yeyeote angeupenda mwili wake katika hali yeyeote ile.

nimejaribu dada sijui kama nimeeleweka angalau?
 
Last edited by a moderator:
niliposoma hii mada nikawaza upendo niliona kwa mama yangu nizaidi lakini niliporudi kwa mwanangu nikawaza mmmhh nampenda kuliko mama khaa nikizidi kwenda kwa ndugu jamaa na marafiki kila mmoja ana nafasi yake ya upendo kwangu nashindwa kutamka mama/mwanangu.....upande wa mume umechanganya na upendo wa agape/ mapenzi tayari hapa unakuwa upendo wa aina nyingine

Umeona eeh, kila mtu ana nafasi yake. Na come to think of it, nafikiri degree ya upendo kuongezeka au kupungua huchangiwa na tabia au matendo ya mpendwaji/mchukiwaji. Hivyo tukichukiacho ni tabia 'mbaya' (tusiyoipenda) ya mtu na sio mwili wa mtu.
 
Nakubaliana na hiyo statement kiasi kikubwa, ukiachia special cases za wanaoua watoto wao au kuwadhuru.
Vinginevyo upendo wa mama hakuna mtu mwingine anaweza kukupa, it's deep. Na kamwe huwezi kumpenda mzazi wako kama yeye anavyokupenda.

Wee fikiria tu upendo wako kwa wanao, ni kiasi gani waweza sacrifice kwa ajili yao? Unadhani ni rahisi mtu mwignine fanya hivyo kwa ajili yao?
baba yao je hawezi fanya the same?
yaani kama mimi nikiangaliaga jinsi mume wangu anavyowapenda watoto wake, najiulizaga kweli mimi nawapenda hawa wanangu kama baba yao anavyowapenda?
mimi pia nilikuwa mtoto wa baba, yaani baba alikuwa ananipenda balaa..... najiulizaga naweza sema kwa hakika kabisa mama ananipenda zaidi kuliko baba? kwa vigezo gani?
 
Heaven on Earth sio kwamba unatafsir kupendwa sana na mama kutokana na kufanya majukumu yake ambayo anaona asipoyafanya hakuna mwingne wa kuyafanya?
ndo maana nika-warn kabisa..... usiseme sababu kanibeba tumboni miezi kadhaa, kuna wanaobeba mimba na wanatupa watoto....
majukumu ya wazazi kwa watoto ni kawaida. siwezi sema baba ananipenda zaidi sababu ananilipia ada ya shule, ni wajibu wake
 
niliposoma hii mada nikawaza upendo niliona kwa mama yangu nizaidi lakini niliporudi kwa mwanangu nikawaza mmmhh nampenda kuliko mama khaa nikizidi kwenda kwa ndugu jamaa na marafiki kila mmoja ana nafasi yake ya upendo kwangu nashindwa kutamka mama/mwanangu.....upande wa mume umechanganya na upendo wa agape/ mapenzi tayari hapa unakuwa upendo wa aina nyingine
umeona eeehhh! yaani ni ngumu sana kujua kiuhakika kabisa nani anakupenda zaidi.....
kuna watu ambao wanaweza kufanya lolote kwa ajili yako....
nakumbuka karibia naolewa kuna kakangu alimpa warning my husband kuwa huyu mdogo wangu nampenda kuliko anavyopendwa na mtu yeyote kwenye hii familia..... ukifanya lolote baya kuhusu huyu, jiandae kupambana na mimi....
 
kiukweli dada Fixed Point hili suala linatatiza sana kwa kweli ila nachoweza kusema ni kwamba upendo wa mama ni wa asili yaani hauna sababu maaluma kama muonekano labda au sauti ,rangi(vitu ambavyo vinachochea huu upendo mwingine kati ya me na ke au rafiki na rafiki).

Nachokimaanisha ni kwamba upendo wa mama hauzuiliki na hii ni kwa sababu ya hatua zote za kupatikana kwa mtoto mpaka kuzaliwa na kukua,mama anapokuwa na mtoto tumboni huhisi kuwa mtoto huyo ni sehemu ya mwili wake na hivyo tokea hapo ule upendo usio na sababu maalum huanza kukua na hata baada ya kuzaliwa ambapo bado mama huona kama mwanaye ni sehemu ya mwili wake na hivyo kumpenda sana katika hali yeyote kam ambavyo mtu yeyeote angeupenda mwili wake katika hali yeyeote ile.

nimejaribu dada sijui kama nimeeleweka angalau?
umeelewa sana mdogo wangu, tena na kupitiliza.
labda tu nikuulize una mtoto?
kama una watoto angalau zaidi ya mmoja unaweza kuniambia kuwa ni vipi upendo wako ulivyo kwa watoto wako, wazazi, na wengineo...... ha haaaa
 
  • Thanks
Reactions: BAK
unamtendea haki mtu mwingine yeyote anayekupenda kwa haya maneno yako?

yani A mother's love is unconditional; it's instinctual and unrelenting.ko hao wataniunderstand tu

ni tofauti na Romantic love which is not not instinctual,
A mother's love is boundless. It doesn't depend on any conditions and doesn't fade.IT IS ALWAYS THERE
When a woman becomes a mother, she learns to walk with her heart outside of her body. It's unexplainable
but your a mother my Sis you know and understand this
 
yani A mother's love is unconditional; it's instinctual and unrelenting.ko hao wataniunderstand tu

ni tofauti na Romantic love which is not not instinctual,
A mother's love is boundless. It doesn't depend on any conditions and doesn't fade.IT IS ALWAYS THERE
When a woman becomes a mother, she learns to walk with her heart outside of her body. It's unexplainable
but your a mother my Sis you know and understand this
ndo maana naogopa sana kuweka kwenye mizani mapenzi ya wapenzi na ya wazazi hasa mama......
ila nikifikiria sana wamama wangapi wapo ambao hawawapendi watoto wao kihivyo? yaani zaidi ya wanavyopendwa na dada, kaka, baba?
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Sijui unaupimaje huo upendo, ila kwa mtizamo wangu, hakun amtu amaewahi nipenda kama mama yangu. Na huwanasikitika kuwa japo nampenda, ila upendo wangu kwake hauwezi fikia upendo wake kwangu.

Na hii niliiona baada ya mie kupata watoto wangu, jinsi ninavyowapenda sitegemei wao wanipende vile. kwa nini? They take me for granted sababu wamezaliwa na kunikuta ninawapenda tu. Na wao wanaona nipo tu kwa ajili yao na siwezi kuondoka. Siwezi kumsemea saana baba, japo nakubali wapo kina baba wanawalea watoto wao utadhani wao ndio mama zao (cc Nyani Ngabu - Sijui kwa nini nahisi ni baba wa mfano)

Tofauti na mie sikuwa nao, ni kitu nimekifanyia kazi kukipata, kuanzia utungaji wa mimba, ukuaji wa mimba na mawasialiano kati yetu, mara kanichoma mbavu na kiwiko, mara anacheza mieleka, mradi tu mawasiliano yako juu juu.

I could not wait for them to come out nione product yangu. Na kitu cha kushangaza na kufurahisha ni kuona sura 2 katika mtu mmoja, my eyes, his nose, my lips, his ears. Kuanzia siku ya kwanza nilivyokiona kidogo kama ki samaki kimejaa mifupa kila mahali, i was so excited, ambavyo nilihangaika hata kukitoa kitandani nisijue la kufanya. Kumbukumbu hizo zote kwa pamoja zinajikusanya na kuwa upendo mkubwa ambao kwa tafsiri yangu ya sasa, sitegemei kupata upendo wa aina hiyo kwa mtu mwingine zaidi ya mama.

Labda kwa sababu mapenzi ya mzazi na ya mme/mke yanatofautiana.

baba yao je hawezi fanya the same?
yaani kama mimi nikiangaliaga jinsi mume wangu anavyowapenda watoto wake, najiulizaga kweli mimi nawapenda hawa wanangu kama baba yao anavyowapenda?
mimi pia nilikuwa mtoto wa baba, yaani baba alikuwa ananipenda balaa..... najiulizaga naweza sema kwa hakika kabisa mama ananipenda zaidi kuliko baba? kwa vigezo gani?
 
Last edited by a moderator:
1391758_556275424451820_177935180_n.jpg

sina wasiwasi kabisa kuwa mama yangu ananipenda sana tena sana kabisa.......
Najiuliza ni fair kutoa statement kama hii?
Ni kweli kabisa kuwa mama zetu wanatupenda sana kuliko mtu yeyote anavyotupenda?
Nina uhakika naweza kupima mapenzi yangu kwenda kwa mwingine, nina uhakika kabisa nani nampenda zaidi kuliko mwingine, lakini unaweza kujua kwa uhakika kabisa kuwa nani anakupenda sana kuliko mwingine?
Ni kweli wababa hawapendi watoto wao zaidi ya vile ambavyo mama zao wanawapenda?
Tuachane na story za kusema "mama alimbeba mtoto tumboni miezi 9" ndo sababu anampenda sana. kuna wamama ambao wanabeba mimba na wanatupa watoto au kuwatelekeza.
Haya mapenzi ya kutota upande mwingine tunayapimaje?
Naomba tujadiliane hili tafadhali
there is some truth. kumbuka ukiwa kwenye hatari ya ghafla wengi tunascream insticitively "mama nakufa".
 
umeelewa sana mdogo wangu, tena na kupitiliza.
labda tu nikuulize una mtoto?
kama una watoto angalau zaidi ya mmoja unaweza kuniambia kuwa ni vipi upendo wako ulivyo kwa watoto wako, wazazi, na wengineo...... ha haaaa

Bahati mbaya sana bado sijajaliwa kuwa na mtoto,ila nachoweza kusema ni kwamba mama yangu nampenda sana tena sana zaidi ya sana,lakini japo kuwa huu ni ukweli wa karibu kila mmoja wetu ni ukweli ambao mume au mke au mpenzi asingependa kuusikia kwani tulio wengi tunapenda kujua kuwa tunashika namba moja,kwa hiyo ni vizuri kunyamaza nao moyoni tu na kuujua mwenyewe.

lakini tena upendo ni mpana kama bahari kwa sababu unavyowapenda ndugu zako,wazazi wako na mume/mke wako ni tofauti,na hii ni kwa sababu kila upendo una chanzo au sababu yake ya kukua kwa mfano:

1.Kaka na dada zako mnashirikiana katika mambo mengi na labda mmekua pamoja mlitaniana na kucheza michezo pamoja na labada unajua wapo tayari kukusaidia na kukufariji unapopatwa na shida.

2.Mama huyu toka u mdogo umenyonya ziwa lake ulipoanza kutambaa unaye kila hatua uipitiayo unamwona yeye unakua unaona jinsi anvyokusimamia katika mambo mbalimbali na wakati mwingine kukuteteta upatapo shida na ukiumwa unamwona anavyohangaika akikesha juu yako.

3.Mpenzi/mke/mume huyu sasa mna mengi mnayoyafanya kuelezana siri zenu kufarijiana kuahidiana ahadi tele tele ukimwona moyo wako unaruka utulivu kushnei,unahisi hujawahi kuona mtu mwenye mvuto kama yeye.

kwa hiyo nafikiria upendo unatofautiana huwezi kuwapenda baba,mama,dad,kaka,binamu,mume/mke kinamna moja.
 
Kongosho umeelezea wewe mpaka sijui niongeze nini,ila tena kuna hili jambo nimesikia likisemwa kuwa mtoto anapokuwa umri fulani na kifo cha mzazi mmojawapo sana sana mama kikitokea huumia kupita maelezo,lakini kinapotokea wakati tayari mtoto ana mke/mume haumizwi sana na kifo hicho kama ambavyo ataumizwa na kifo cha mume/mke wake,sijui hili pia limekaaje jamani nimekuwa nikijaribu kuona ukweli wa hili lakini nimekuwa sipati jibu halisi.

copy Fixed Point
Sijui unaupimaje huo upendo, ila kwa mtizamo wangu, hakun amtu amaewahi nipenda kama mama yangu. Na huwanasikitika kuwa japo nampenda, ila upendo wangu kwake hauwezi fikia upendo wake kwangu.

Na hii niliiona baada ya mie kupata watoto wangu, jinsi ninavyowapenda sitegemei wao wanipende vile. kwa nini? They take me for granted sababu wamezaliwa na kunikuta ninawapenda tu. Na wao wanaona nipo tu kwa ajili yao na siwezi kuondoka. Siwezi kumsemea saana baba, japo nakubali wapo kina baba wanawalea watoto wao utadhani wao ndio mama zao (cc Nyani Ngabu - Sijui kwa nini nahisi ni baba wa mfano)

Tofauti na mie sikuwa nao, ni kitu nimekifanyia kazi kukipata, kuanzia utungaji wa mimba, ukuaji wa mimba na mawasialiano kati yetu, mara kanichoma mbavu na kiwiko, mara anacheza mieleka, mradi tu mawasiliano yako juu juu.

I could not wait for them to come out nione product yangu. Na kitu cha kushangaza na kufurahisha ni kuona sura 2 katika mtu mmoja, my eyes, his nose, my lips, his ears. Kuanzia siku ya kwanza nilivyokiona kidogo kama ki samaki kimejaa mifupa kila mahali, i was so excited, ambavyo nilihangaika hata kukitoa kitandani nisijue la kufanya. Kumbukumbu hizo zote kwa pamoja zinajikusanya na kuwa upendo mkubwa ambao kwa tafsiri yangu ya sasa, sitegemei kupata upendo wa aina hiyo kwa mtu mwingine zaidi ya mama.

Labda kwa sababu mapenzi ya mzazi na ya mme/mke yanatofautiana.
 
Last edited by a moderator:
baba yao je hawezi fanya the same?
yaani kama mimi nikiangaliaga jinsi mume wangu anavyowapenda watoto wake, najiulizaga kweli mimi nawapenda hawa wanangu kama baba yao anavyowapenda?
mimi pia nilikuwa mtoto wa baba, yaani baba alikuwa ananipenda balaa..... najiulizaga naweza sema kwa hakika kabisa mama ananipenda zaidi kuliko baba? kwa vigezo gani?

kuna baba mmoja rafiki yetu anapenda watoto hata zaidi ya mke hadi sie wa nje tunaona upendo uliopo na mkewe aliwahi kukiri mbele yetu jinsi mumewe alivyo naupendo kwa wanawe na watoto wanampenda baba zaidi ya mama......hapa nafikiri watoto wanapopenda baba/mama zaidi ya mwingine ni kutokana na upendo anaopata kutoka kwa mmoja wao mie kweli huwezi sema kitu juu ya mama yangu lakini baba mmmhh nilipokuja pata mtoto hapo nachanganyikiwa kabisa
 
Heaven on Earth sio kwamba unatafsir kupendwa sana na mama kutokana na kufanya majukumu yake ambayo anaona asipoyafanya hakuna mwingne wa kuyafanya?
Mapi it's not all about the 9 months in the womb as you think,It's the day to to day care you get
alivyo sensitive kwenye matatizo yangu na mahitaji yangu,there is SOMETHING with her that i cant get
it anywhere....

anavyonipenda ni zaidi ya nimpendavyo...anavyonifanyia mie siwezi kumfanyia......
napata shida hadi kuelezea
 
Sijui unaupimaje huo upendo, ila kwa mtizamo wangu, hakun amtu amaewahi nipenda kama mama yangu. Na huwanasikitika kuwa japo nampenda, ila upendo wangu kwake hauwezi fikia upendo wake kwangu.

Na hii niliiona baada ya mie kupata watoto wangu, jinsi ninavyowapenda sitegemei wao wanipende vile. kwa nini? They take me for granted sababu wamezaliwa na kunikuta ninawapenda tu. Na wao wanaona nipo tu kwa ajili yao na siwezi kuondoka. Siwezi kumsemea saana baba, japo nakubali wapo kina baba wanawalea watoto wao utadhani wao ndio mama zao (cc Nyani Ngabu - Sijui kwa nini nahisi ni baba wa mfano)

Tofauti na mie sikuwa nao, ni kitu nimekifanyia kazi kukipata, kuanzia utungaji wa mimba, ukuaji wa mimba na mawasialiano kati yetu, mara kanichoma mbavu na kiwiko, mara anacheza mieleka, mradi tu mawasiliano yako juu juu.

I could not wait for them to come out nione product yangu. Na kitu cha kushangaza na kufurahisha ni kuona sura 2 katika mtu mmoja, my eyes, his nose, my lips, his ears. Kuanzia siku ya kwanza nilivyokiona kidogo kama ki samaki kimejaa mifupa kila mahali, i was so excited, ambavyo nilihangaika hata kukitoa kitandani nisijue la kufanya. Kumbukumbu hizo zote kwa pamoja zinajikusanya na kuwa upendo mkubwa ambao kwa tafsiri yangu ya sasa, sitegemei kupata upendo wa aina hiyo kwa mtu mwingine zaidi ya mama.

Labda kwa sababu mapenzi ya mzazi na ya mme/mke yanatofautiana.

Maelezo yako yanaonyesha jinsi gani mwanaume na mwanamke walivyo tofauti.. asanteni kwa somo zuri!
 
Last edited by a moderator:
kuna baba mmoja rafiki yetu anapenda watoto hata zaidi ya mke hadi sie wa nje tunaona upendo uliopo na mkewe aliwahi kukiri mbele yetu jinsi mumewe alivyo naupendo kwa wanawe na watoto wanampenda baba zaidi ya mama......hapa nafikiri watoto wanapopenda baba/mama zaidi ya mwingine ni kutokana na upendo anaopata kutoka kwa mmoja wao mie kweli huwezi sema kitu juu ya mama yangu lakini baba mmmhh nilipokuja pata mtoto hapo nachanganyikiwa kabisa
ha haaa, mimi najua kuwa napenda sana watoto wangu, wote..... but ninavyomwangalia baba yao, ukweli siwezi kusema upendo wangu kwa watoto ni mkubwa kuliko wake, nitakuwa namwonea. hapa upendo sisemei uwajibikaji, upendo
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Back
Top Bottom