Tuisaidie Taifa Start ili nchi isipate aibu!

Tuisaidie Taifa Start ili nchi isipate aibu!

Wachezaji wetu tatizo Jani. Wanavuta sana ile kitu. Pili, lugha haipandi. Ung'eng'e kwao ni mama mkwe. Kocha afanyaje? Afundishe kizaramo!

Maximo alikuwa anajua kiswahili acha kumtetea huyo kocha ni poyoyo
 
Ukinitajia kitu chochote ambacho Tanzania inafanya vizuri kwenye mashindano yoyote... nitavua nguo Posta mpya!!

Si michezo, uchumi, utamaduni,..... endelea unavyoweza hakuna tunachoweza!!

Haya ni matokeo ya kushindwa kwa Taifa letu. CCM si tu inaharibu uchumi ila ni kila sekta hali ni mbaya!!!

Yaani kama kuna mtu ambaye ni MAtokeo TAratibu KOngosho basi ni wewe. Sasa CCM ndio inayocheza mpira au CCM ndio kocha au CCM ndio Benchi la ufundi? Utakuwa una KENGEZA kama Mwenyekiti wako Jukwaa la michezo unaona la siasa.

Ukija huku changia issue za Mpira sio kutuletea uozo huo wa kipimbi.

Kuna haja ya kurudisha academy za michezo. Fukuza huyo mzungu leta kocha mwingine na TFF waache kuingilia makocha na benchi la ufundi katika kupanga au kuchagua wachezaji wa timu ya taifa hata kama ataita mchezaji kutoka Abajalo FC.
 
Kutokuendelea kwa kitu chochote Tanzania ni kwa sababu ya Utanzania wa Mtanzania...

Laiti kama hulka ya Mtanzania ikibadilika au ikionesha nia ya kubadilika basi hata mambo mengine yataanza kunyooka...
 
Yaani kama kuna mtu ambaye ni MAtokeo TAratibu KOngosho basi ni wewe. Sasa CCM ndio inayocheza mpira au CCM ndio kocha au CCM ndio Benchi la ufundi? Utakuwa una KENGEZA kama Mwenyekiti wako Jukwaa la michezo unaona la siasa.

Ukija huku changia issue za Mpira sio kutuletea uozo huo wa kipimbi.

Kuna haja ya kurudisha academy za michezo. Fukuza huyo mzungu leta kocha mwingine na TFF waache kuingilia makocha na benchi la ufundi katika kupanga au kuchagua wachezaji wa timu ya taifa hata kama ataita mchezaji kutoka Abajalo FC.

Wewe mburura... aliyefuta michezo mashuleni ni nani?? anayejifanya kumiliki viwanja vya michezo ni nani.. anayetunga na kusimamia sera ya michezo ni nani.. kama si CHAMA CHA MAGAMBA CCM...

Kama wameshindwa kusimamia wanyama na kuua tembo wetu wataweza kusimamia michezo...??/

Sasa kwa sababu unafikiri kwa kutumia makalio unafikiri mtu mpaka aingine uwanjani ndiyo anahusika kujenga au kubomoa michezo!!
 
Taifa kubwa kama Tanzania kukosa heshima ni aibu sana.

Tumeshindwa kila kitu yaan aibu Kupigwa na vitaifa uchwara kama

Madagasca
burundi
nk

Matokeo ya kuongozwa na viongozi legelege.
 
Nibora timu kumpa mzawa maana kiwango alichokionesha huyu mpumbavu sioni tofauti na mzawa kuiendesha timu
 
Mtanzania toa maoni yako ni kitu gani kifanyike ili timu ya Taifa iondokane na hii aibu ya kila mwaka! Je tatizo ni kocha au? toa mawazo yako hapa ili hata Jamal Malinzi akipitia hapa aweze kuona watanzania wanasema nini juu ya timu yao ya taifa.Hii ni aibu tuisaidie timu yetu.

Jamal Malinzi ni number one soccer spoiler. Nafasi ya Mbeya City Fc kawapa Simba bila ya sababu yoyote ya msingi. Kwa hili ajieleze Watanzania wamuelewe
 
Last edited by a moderator:
Walipocheza Starz,na Mozambique nilishangilia Mozambique, mlisema mimi sio mzalendo.!!Hata Leo ningeiona hiyo game ningeshangilia hao Madagascar inaonekana inaujua mpira.

Presha aliyonipa Moyes mwaka Jana yatosha!!

siku starz ikicheza naangalia clips za Gaucho na Zidane, napata satsfication nzuri kuliko nyie mnaoangalia stars.


In short mpira sio fani yetu,tuuvumbue mchezo mwingine tu
 
Hatua ya kwanza ni kumuondoa Malinzi,then kufukuza huyo kocha aliyemleta.Si kweli kwamba hatuna wachezaji wazuri Maximo alipata mafanikio na kina Tegete,Ngasa,Nizar,Maftaha,Nditi,Nyoni,Boni,Nsajigwa,Mapunda,Yondani iweje hawa wa sasa wanafungwa kila siku
 
Taifa kubwa kama Tanzania kukosa heshima ni aibu sana.

Tumeshindwa kila kitu yaan aibu Kupigwa na vitaifa uchwara kama

Madagasca
burundi
nk

Matokeo ya kuongozwa na viongozi legelege.


Kazi yao ni fitina tu
 
ushauri wangu ni kumwomba yule mzee wa awamu ya pili, mzee al Hassan mwinyi ikibidi tukampigie magoti aje atengue ile kauli yake ya kichwa cha mwendawazimu..maana aliiachia laana söka yetu kwa kauli hiyo vinginevyo tutaendelea kuwa kichwa cha mwenda wazimu tena yatubidi tuwahi kabla Mungu 'hajampenda' mzee wa watu la sivyo tutakuwa kichwa cha mwendawazimu milele yote daima
 
polen sana Watanganyika wenzangu mnaowekeza matumaini ya ushindi kwa taifa starz! mimi niliacha kuishabikia hii timu tangu tulipofungwa 4-0 na senegal tukitokea kambin huko Brazil.
 
Nimetokea kutompenda huyo kocha. Aende tu, timu wampe Minziro
 
Nimetokea kutompenda huyo kocha. Aende tu, timu wampe Minziro
Aiseeee kama mimi yaan simpendi huyu kocha!
Hivi kwel huyu mtu aliwahi kucheza mpira kweli kabla hajawa kocha au mahiliz alimkuta anafanya shooting ya x ndo akamchukuwa??
Tena asirudi tz tena atokee huko huko south'
 
Malinzi Ccm ung'atuke hapo TFF

Taifa stars ni kichwa cha mwendawazimu by Alhaj Mwinyi.
 
Malinzi uamuzi wa busara ni bora aachie ngazi mana, toka ashike nafasi hakuna jambo la maana analojivunia zaidi ya kuiba waziwazi bila haya, Na aondoke yeye pamoja na kocha wake. Na hatutakuja uwanjani mpaka muondoke nyie wezi
 
Mimi ilifikia hatua nikazani labda kufatilia ligi za nje labda kumenipofusha. kuna mtu nimemwambia kuna uwezekano haya mashindano tukatoka bila hata bao moja. Nikawaza hivi tukikutana na Uganda au Rwanda kwenye cecafa si tutadhalilishwa?
 
Kwanza huyo Jamal Malinzi aondoke kabisa TFF akatafute kazi nyingine za kufanya, hana ubunifu, hana mawazo, hana ujanja, haijuwi soka, hawezi kuiendeleza soka hata awepo hapo miaka 100.

Sijuwi hao waliomchaguwa walikuwa na kigezo kipi kilichowafanya wachaguwe.

cc Bishanga
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom