Tuipeleke Singeli intaneshenali!

donlucchese

JF-Expert Member
Mar 23, 2011
17,042
21,517
Salam wakuu,

Straight to the point. Nimekaa sehemu flani hapa wanapaita Bambalaga, Dj amegonga magoma ya amapiano hapa watu wote wamewehuka kwa vishindo vya magoma. S.A kiukweli wameweza kupenetrate muziki wa kimataifa kwa mtindo wao (midundo yao).

Wakiwa Ni waanzilishi wa mtindo wa kwaito, wasanii wa bongo walifanya sana kwaito kipindi hiko kujaribu kucope na wasauzi Ila Sina kumbukumbuku sahihi kama kuna waliotoboa thru kwaito music. Wamekuja sasa na huu mtindo wa amapiano ambapo mpaka sasa unatikisa dunia na kufanya na baadhi ya wasanii wa bongo wajiongeze.

Kwa sasa kuna ngoma za kutosha za amapiano za wabongo na zinatikisa sana (pengine kuwazidi waanzilishi wenyewe). Ngoma kama bia tamu, waiona hiyooo, ticha, nikilewa etc

Ukisikiliza kwenye spika za maana lazima ukubali. Wanaijeria pia wana identity yao wamejitengezea (japo kama wanafanana na WA Ghana). Ukisikiliza rythm ya wimbo unajua tu mapema wacongo ndio usiseme.

Nauliza kwanini singeli ambayo inatutambulisha wabongo isiende kimataifa? Enzi za mnanda kina marehemu Juma Mpogo, Jenero Lopozi, Seven Survivor, Jagwa waliupeleka mziki kimataifa. Jagwa mepiga shoo nyingi za mnanda ulaya ukichek wazungu wanavyopagawa huwezi amini. Maoni yangu, singeli hii ikiboreshwa na kuongezewa vionjo inaweza fika mbali sana. Angalia Alicia keys alivyokua anaserebuka na ngoma ya wanga wabaya ya Meja kinda.
 
Kulikuwa na movement ya singeli to the worldmwaka jana, lakini ikaishia katikati.

Tatizo wabongo huwa tunapenda shortcut na hatukubali vya kwetu, mfano singeli kuna wabongo "wakishua" watakuambia hawasikilizi mziki wa uswazi lakini zikipigwa amapiano ambazo hizo hizo zinasikilizwa huko sauzi uswazi wanaruka nazo na mizuka yote.

Sasa msanii akiona hilo vibe akiingia studio atataka na yeye arekodi ngoma kama msauzi, tulishaiga wanaija pia kupiga ule mtindo wa afrobeats na ukija mtindo mwingine tutaruka nao hivyo hivyo, hakuna msanii mwenye moyo wa kutengeneza identity ya muziki wetu maana identity haiendi tu na trends, mwanzoni utakomaa na watu wanaweza wasikuelewe.
 
SINGELI NI MZIKI WA ASILI YA TANZANIA NZIMA AU BAADHINYA SEHEMU???MAANA UKIZUNGUMZIA KWAITO NI SA NZIMA,BOLINGO NI CONGO NZIMA ILA HII SINGELI NI MZIKI WA ASILI TOKA KABILA FULANI TU,JE UNAWEZA KUWA NDO MUZIKI WETU WA TAIFA KAMA UTAMBULISHO WETU???
 
Inawezekana kama Singeli ikiongezwa vionjo na maudhui ya nyimbo yabadilike kidogo kuendana na soko la kimataifa. Kwasasa nikisikiliza naburudika lakini naona ujumbe kwenye nyimbo za waimba Singeli wote unawalenga watu wa Mbagala na wacheza vigodoro tu. Hii nafikiri ni kwasababu waimbaji wake wengi wametokea kwenye mazingira hayo. Hili ni swala la wadau wa muziki, maproducer na waandishi wa nyimbo wawasimamie hawa vijana watoe nyimbo za kueleweka
 
Muziki wa singeli ili uweze kupenya kimataifa inatakiwa kwanza ukubalike ushuani.
Lazima wakubali ku customize midundo yao ifanane atleast na muziki wa dunia.
 
SINGELI NI MZIKI WA ASILI YA TANZANIA NZIMA AU BAADHINYA SEHEMU???MAANA UKIZUNGUMZIA KWAITO NI SA NZIMA,BOLINGO NI CONGO NZIMA ILA HII SINGELI NI MZIKI WA ASILI TOKA KABILA FULANI TU,JE UNAWEZA KUWA NDO MUZIKI WETU WA TAIFA KAMA UTAMBULISHO WETU???
Swali fikirishi
 
Inawezekana kama Singeli ikiongezwa vionjo na maudhui ya nyimbo yabadilike kidogo kuendana na soko la kimataifa. Kwasasa nikisikiliza naburudika lakini naona ujumbe kwenye nyimbo za waimba Singeli wote unawalenga watu wa Mbagala na wacheza vigodoro tu. Hii nafikiri ni kwasababu waimbaji wake wengi wametokea kwenye mazingira hayo. Hili ni swala la wadau wa muziki, maproducer na waandishi wa nyimbo wawasimamie haya vijana watoe nyimbo za kueleweka
Well said mkuu
 
Muziki wa singeli ili uweze kupenya kimataifa inatakiwa kwanza ukubalike ushuani.
Lazima wakubali ku customize midundo yao ifanane atleast na muziki wa dunia.
Kwaio mkuu unataka watu wachane kwenye beats za techno au trap?
 
Kulikuwa na movement ya singeli to the worldmwaka jana, lakini ikaishia katikati.

Tatizo wabongo huwa tunapenda shortcut na hatukubali vya kwetu, mfano singeli kuna wabongo "wakishua" watakuambia hawasikilizi mziki wa uswazi lakini zikipigwa amapiano ambazo hizo hizo zinasikilizwa huko sauzi uswazi wanaruka nazo na mizuka yote.

Sasa msanii akiona hilo vibe akiingia studio atataka na yeye arekodi ngoma kama msauzi, tulishaiga wanaija pia kupiga ule mtindo wa afrobeats na ukija mtindo mwingine tutaruka nao hivyo hivyo, hakuna msanii mwenye moyo wa kutengeneza identity ya muziki wetu maana identity haiendi tu na trends, mwanzoni utakomaa na watu wanaweza wasikuelewe.
Umenena vyema sana mkuu
 
first
Mimi pia nipo hapo ulipo mkuu ukimuona mtu mnene kama kibanda cha mpesa, kavaa kanzu nyeupe. Nistue

Pili amapiano ni muziki wa hovyo kuwahi kutokea, muziki gani mpaka usikilize kwenye speaker kubwa tu?
 
first
Mimi pia nipo hapo ulipo mkuu ukimuona mtu mnene kama kibanda cha mpesa, kavaa kanzu nyeupe. Nistue

Pili amapiano ni muziki wa hovyo kuwahi kutokea, muziki gani mpaka usikilize kwenye speaker kubwa tu?
, ila kwenye spika kubwa hauondoki. Halafu ukute sasa siku hiyo ni weekend halafu watoto wa chuo wana boom
 
Hivi ule mtindo unaotumiwa na WAMWIDUKA BAND katika nyimbo zao kama Kilingeni na Ni Wewe unaitwaje na origin yake ni wapi? Uko poa sana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom