TUIMULIKE TBC KATIKA MATUMIZI YA TEKNOHAmA

Mtazamaji

JF-Expert Member
Feb 29, 2008
5,937
1,437
wanajamvi

Kabla sijasema memngi naomba tembelea

Home page ya TBC Tanzania Broadcasting Corporation - (TBC)
TBC Taifa wao page yao hii hapa TBC TAIFA
Alafu tembelea Home website ya KBC (kenya) Kenya Broadcasting Corporation:

Sitaki kwenda mbali kulinganisha hizi website na web kama za CNN na BBC.

Sasa kuna mapungufu mengi nimeyaona kwenye TBC moja ya tasisi inayotakiwa kuwa mfano kwenye mambo ya TEKNOHAMA.

  • Kwanza kabisa nilitegemea kwenye web ya TBc watanzania waweze kuona habari katika video. Japo taarifa ya habari ya jana au juzi. Ukichunguza vizuri Kbc wana viunganishi vyao official kwenda youtube ambako wameweka vipande ya taarifa za habari na vipindi vingine.TBC wansindwa nini kuweka picha za video.?????

  • Ukienda kwenye kiunganishi cha contact us ( http://www.tbc.go.tz/contact-us.html)cha TBC unakutana na kituko. Si tu wanawalazimsisha watu wawasiliane nao kwa njia moja ya simu pekeee bali nimejaribu kupiga baadhi simu zao naombiwa nakosea number . Anayeweza ajaribu hizo number za kwenye contac us one ( 0025522270032/62). Linganisha na contact us ya kbc (Kenya Broadcasting Corporation: - Contact Us) wameweka na email pia ambayo ndiyo njia rahisi na nafuu kwa mtu anayetumia website kuweza kutumia.
Hiki ni kituko sana kwangu.Najua wanaweza kuwa nayo email lakini hii web inaonyesha vitu haviko coordinated vizuri nyuma ya pazi . N a hata kama wanayo sijui kama kuna mtu serius anayekuwa anaicheki na kujibu au kufanyia kazi comments za watu

  • Taarifa haziko updated katika wakati TBC .Nafuu kidogo kwenye home page ya TBC kitu cha kwanza unaona ni picha ya Pinda lakini nina hakika hii picha inaweza kuwa ya mwaka 2009 au 2010. Sasa kituko ni kwenye TBC taifa picha inayoonekana ni mdada akiwa studio....... ..Hivi hata kama habari za picha zina umuhimu ndio waweke picha ya studio.!!!!!!!!!
Hakuna mtu anataka kuona xyz akiwa studio ,tunataka kuona wakisoma au kutangza taarifa
Sasa ukija kwenye hata habari zenyewe za maadishi pia haziwi updated na sio latest. Ilinishangaza website ya BBC swahili ilikuwa na updated news za uchaguzi wa tanzania kuliko TBC. BBC waliweza kutumia channel ya Ustream.tv kuwafikishia habari watu wengi zaidi.

Mfano TBC taifa habari yao ya kwanza inasomeka hivi "Last Updated ( Friday, 05 November 2010 03:45 ". Kiunganishi cha vacancies(http://www.tbc.go.tz/vacancies.html) kimekuwa "Last Updated Saturday, 24 October 2009 10:23" Je ni kweli TBC hawajaajiri toka kipindi hicho??!!!!​
Nimeongelea TBC sababu ni chombo cha umma lakini hoja yangu inaweza kuvilenga vyombo vingi vya habari ambavyo haviwi mfano mzuri katika Teknohama

Nawasilisha kwa mjadala
 
Nakubaliana na wewe, japokuwa nimeona kbc kuna banners and ads za google.

Labda wakushimoni wanatengenezea wavuti-uuaji (killer website)!
 
RedSilverDog said:
Nakubaliana na wewe, japokuwa nimeona kbc kuna banners and ads za google.

Labda wakushimoni wanatengenezea wavuti-uuaji (killer website)!

Yaani inasikitisha kuona watu wanakula mishahara lakini hawafanyi kazi inayotakiwa

Sasa kuna tofauti gani kati ya Tanzania Broadcasting Corporation - (TBC) na Gazeti la habari za kiswahili la kila siku Tanzania, linaongoza

Tofauti iliyo tunayojuani mwanahci inahusika na magazeti tu wakati TBC inahusika na broadcasting. Lakini ukitazama website hizo mbili ni kama TBC nayo ni web site ya gazeti.websiteya TBC haina ladha ya broadcasting kabisa.kuitofautisha na website ya mwananchi.

TBC wake upplease publish clip muhimu katika video au hata katika sauti tu. Mfano taarifa za habari, hotuba muhimu, mao au program za kuelimisha zinazopnedwa.

Je inawezekana bandwidth cost ikawa kikwazo hata kwa ?

Je wahusika wa TBC wanajua kuna site ya www.alexa.com inaweza kuwasaidiakujua position ya site yao . Hii site infanya analysis ya website kujua :-
- How good or bad website inapata trafiic
- Rank ya website kitaifa na kimataifa
-W adau wakubwa wanaoitembelea website ni wa nchi gani wa jinsia gani na wa age group gani ?

According to alexa.com analyisis tbc website ni poor kulinganisha na mwananchi.co.tz

Aibu kweli
 
Unampigia mbuzi gitaa?

hahahahaha
Sasa tufanyeje inabidi tupige tu inaweza kutokea mbuzi akacheza bit chache za hilo gitaa si unaona hata upande wa siasa kule wamenza kukubali mazungumzo yakatiba mpya sembuse huku kwenye teknolojia mbona kama ni professional sio kazi kubw mbuzi kucheza gitaakama ilivyo kwenye siasa.
 
... unaizungumzia televisheni ya chama tawala banyaaaa!!! Hawana lolote mbwa hawa, wala hawana knowledge ya professional journalism. teh, e.g Kipindi maalum kinachokusanya habari za upande mmoja ktk mgogoro wa pande mbili ni ukanjanja wa kichama huo banyaa!!
 
... unaizungumzia televisheni ya chama tawala banyaaaa!!! Hawana lolote mbwa hawa, wala hawana knowledge ya professional journalism. teh, e.g Kipindi maalum kinachokusanya habari za upande mmoja ktk mgogoro wa pande mbili ni ukanjanja wa kichama huo banyaa!!

Mkuu weli lakini hapa tunaongelea teknolojia sio siasa. Hata kama ni ukusanyaji wa habari za upande mmoja hoja ni kuwa tenolojia ya ICT waitumie ipasavyo. Hata kama ni kupotosha basi tuone clip za video hao CCM wakizungumza. I mean changamoto yangu ni kuwa mbona hatuoni video, mbona contact zao kwenye tovuti hazipatikani.

NB:
Nimeleta mada tujadili kiteknolojia sio kisiasa.
 
Firm yoyote ya ICT iliyofanikiwa ni lazima kuwe na vitu viwili,Ubunifu na Kuijua Technology. Vilevile kuna tofauti kati ya Manager na Leader. Wengi wa mamanager ni Leaders.

Nukta.

AfroIT Group
 
Back
Top Bottom