Beatrice Kamugisha
JF-Expert Member
- May 18, 2019
- 762
- 6,980
Kesi ya Ugaidi inaypendelea Mahakama ya Uhujumu uchumi imeonysha namna Serikali ya chama cha Mapinduzi ilivyokuwa inaendeshwa na inavyoendeshwa. Yapo mambo ambayo Wala Jaji apaswi kusubiriwa kuyatolea hukumu maana yapo wazi kabisa. Mfano:
Mkuu wa upelelezi Arumeru Afande Jumanne anayetuhumiwa kuwatesa watuhumia huko Tazara alikamatwa Arusha akahojiwa na kusimamishwa kazi kwa Tuhuma za kumbambikia Profesa mmoja kesi Kisha kuchukua million mia Moja. Lakini pamoja na tuhuma hizo hakuwahi kufikishwa mahakamani Bali alilipwa na Serikali atoke Arusha kwenda DSM kutoa ushahidi Mahakamani na Jaji akiwa anayajua haya yote hakuonyesha kwa namna yoyote ile kutilia mashaka ushahidi wake wala kuomba taarifa za tabia zake kama taratibu zinavyotaka bali yeye Jaji alionekana dhahiri kuunga mkono kile mtuhumiwa huyu alichokuwa anakifanya Mahakamani. Huko Kenya mahakama imehukumu DCI aende jela baada ya kubaini anacheza na Mahakama. Huku kwetu Jaji hana initiative yoyote anayofanya kudhibiti wahuni mahakamani.
Pili , bila hata hukumu ya Jaji ni ukweli ulio wazi kwamba watuhumia wote awakuwahi kufikishwa central Polisi Dar es salaam Bali Kwa ushahidi na nyaraka zinavyoonyesha ni kwamba watuhumiwa walikuwa Tazara na Mbeni. Hivyo Kingai na genge lake wanaidanganya mahakama na Mahakama inajua inadanganywa. Mahakama inashindwa nini kuelekeza jeshi la Polisi kuwasilisha vitabu vya kuweka watu mahabusu? Inashindwa nini kuelekeza jeshi la polisi liwasilishe uthibitisho kwamba Msemwa alikuwa central na siyo osterbay kama utetezi unavyodai? Mahakama gani imefungwa mikono kwa kila kitu? Mahakama gani haitaki kufikiri na kuelekeza?
Tatu ni ukweli uliowazi kwamba makomandoo walioteswa n Polisi waliozibiwa riziki huko JWTZ kwa kufutwa kazi na baada ya kufutwa kazi viongozi wao waliamini wataenda uraiani kuteseka maisha yao yote. Waliposikia wamepata ajira wakaumia sana na kuamua kuzika ndoto zao kwa kuwabambikia kesi inaypendelea. Ni jambo la kawaida kabisa kwa waajiri au viongozi wa serikali kufukuza watu kazi na wanaposikia wamefanikiwa kupata kazi sehemu nyingine utafuta mbinu za kuwahaaribia. Roho mbaya ya kitanzania ina madhara makubwa sana.
Tumeshuhudia mawaziri kama Nape wakivuliwa Uwaziri lakini pia baada ya kuvuliwa uwazri na nyota zao kuonekana zinang'aa walinyamazishwa na kulazimishwa kwenda ikulu kisha wakaitiwa vyombo vya habari kudhalilishwa kwamba wameenda kupiga magoti. TU Membe alivyopitia mateso, hawa ndio waafrika ambao kazi kubwa waliyonayo nikuzima ndoto za waafrika wenzao na kuwasha ndoto za mabeberu na wageni.
Lakini tujiulize kile kinachotokea mahakamani kinawaumiza Askari wangapi? Tunaamini kwamba hawa Askari watazidi kuwa wamoja? Je wanaojua tabia za Makomandoo hawa akiwemo Urio ambaye kwa namna kesi inavyokwenda anaonekana alijua wameonewa na kufukuzwa kazi kimakosa akawataftia ajira wanajisikiaje? Kwamba akina Jumanne anayetajwa kuchukua milioni moja kesi ya sabaya ndiye anaonekana kuwatesa Makomandoo waliofukuzwa kazi?
Lakini pia tujiulize, viongozi waandamizi wa serikali waliopo nyuma ya kesi hii wanamaono gani kuhusu mpasuko wa Taifa LETU?
Nimesoma Kesi mbalimbali DUNIANI za kisiasa, hakuna kesi ya kijinga kama hii inayogonganisha maslahi ya siasa na vyombo vya dola. Kama yupo mwenye kesi kama hii kuwahi kutokea hata hapo Burundi ailete hapa.
Zamani tulizoea kutunishiana misuli Kati ya vijana wa JW na Polisi sijui tukiendelea na kesi hii itakuwaje. Tukumbuke Siro na Mabeyo wanaweza kuwa wamoja, General na viongozi wa juu wanaweza kuwa wamoja lakini nafsi za askari mmoja mmoja aliyejeruiwa na hii kesi haziwezi kuwa pamoja.
Huu ni mtizano wangu kwamba haya yanayokwenda live yanatia chumvi miyoyo ya wapiganaji WETU, wataanza kutunishiana misuli na kushirikiana kinafiki.
Stagomena Tax fanya analysis mshauri Mhe. Rais naamini atakusikiliza. Mahakama imetegwa na kesi ndogo ndani ya kesi kubwa kwa lengo lakuhakikisha kila kitu kinawekwa adharani na msidhani kwamba kina Kibatala wanatumia akili zao yawezekana wapo majaji, generals, watumishi waandamizi wanawapa mbinu hizi, this is not normal , mbinu hizi nikubwa sana ila kwa sababu naamini hakuna kiuongozi mwandamizi anayefuatilia kinachoendelea ndio maana hatujaona action kwa niaba ya nchi.
Mkuu wa upelelezi Arumeru Afande Jumanne anayetuhumiwa kuwatesa watuhumia huko Tazara alikamatwa Arusha akahojiwa na kusimamishwa kazi kwa Tuhuma za kumbambikia Profesa mmoja kesi Kisha kuchukua million mia Moja. Lakini pamoja na tuhuma hizo hakuwahi kufikishwa mahakamani Bali alilipwa na Serikali atoke Arusha kwenda DSM kutoa ushahidi Mahakamani na Jaji akiwa anayajua haya yote hakuonyesha kwa namna yoyote ile kutilia mashaka ushahidi wake wala kuomba taarifa za tabia zake kama taratibu zinavyotaka bali yeye Jaji alionekana dhahiri kuunga mkono kile mtuhumiwa huyu alichokuwa anakifanya Mahakamani. Huko Kenya mahakama imehukumu DCI aende jela baada ya kubaini anacheza na Mahakama. Huku kwetu Jaji hana initiative yoyote anayofanya kudhibiti wahuni mahakamani.
Pili , bila hata hukumu ya Jaji ni ukweli ulio wazi kwamba watuhumia wote awakuwahi kufikishwa central Polisi Dar es salaam Bali Kwa ushahidi na nyaraka zinavyoonyesha ni kwamba watuhumiwa walikuwa Tazara na Mbeni. Hivyo Kingai na genge lake wanaidanganya mahakama na Mahakama inajua inadanganywa. Mahakama inashindwa nini kuelekeza jeshi la Polisi kuwasilisha vitabu vya kuweka watu mahabusu? Inashindwa nini kuelekeza jeshi la polisi liwasilishe uthibitisho kwamba Msemwa alikuwa central na siyo osterbay kama utetezi unavyodai? Mahakama gani imefungwa mikono kwa kila kitu? Mahakama gani haitaki kufikiri na kuelekeza?
Tatu ni ukweli uliowazi kwamba makomandoo walioteswa n Polisi waliozibiwa riziki huko JWTZ kwa kufutwa kazi na baada ya kufutwa kazi viongozi wao waliamini wataenda uraiani kuteseka maisha yao yote. Waliposikia wamepata ajira wakaumia sana na kuamua kuzika ndoto zao kwa kuwabambikia kesi inaypendelea. Ni jambo la kawaida kabisa kwa waajiri au viongozi wa serikali kufukuza watu kazi na wanaposikia wamefanikiwa kupata kazi sehemu nyingine utafuta mbinu za kuwahaaribia. Roho mbaya ya kitanzania ina madhara makubwa sana.
Tumeshuhudia mawaziri kama Nape wakivuliwa Uwaziri lakini pia baada ya kuvuliwa uwazri na nyota zao kuonekana zinang'aa walinyamazishwa na kulazimishwa kwenda ikulu kisha wakaitiwa vyombo vya habari kudhalilishwa kwamba wameenda kupiga magoti. TU Membe alivyopitia mateso, hawa ndio waafrika ambao kazi kubwa waliyonayo nikuzima ndoto za waafrika wenzao na kuwasha ndoto za mabeberu na wageni.
Lakini tujiulize kile kinachotokea mahakamani kinawaumiza Askari wangapi? Tunaamini kwamba hawa Askari watazidi kuwa wamoja? Je wanaojua tabia za Makomandoo hawa akiwemo Urio ambaye kwa namna kesi inavyokwenda anaonekana alijua wameonewa na kufukuzwa kazi kimakosa akawataftia ajira wanajisikiaje? Kwamba akina Jumanne anayetajwa kuchukua milioni moja kesi ya sabaya ndiye anaonekana kuwatesa Makomandoo waliofukuzwa kazi?
Lakini pia tujiulize, viongozi waandamizi wa serikali waliopo nyuma ya kesi hii wanamaono gani kuhusu mpasuko wa Taifa LETU?
Nimesoma Kesi mbalimbali DUNIANI za kisiasa, hakuna kesi ya kijinga kama hii inayogonganisha maslahi ya siasa na vyombo vya dola. Kama yupo mwenye kesi kama hii kuwahi kutokea hata hapo Burundi ailete hapa.
Zamani tulizoea kutunishiana misuli Kati ya vijana wa JW na Polisi sijui tukiendelea na kesi hii itakuwaje. Tukumbuke Siro na Mabeyo wanaweza kuwa wamoja, General na viongozi wa juu wanaweza kuwa wamoja lakini nafsi za askari mmoja mmoja aliyejeruiwa na hii kesi haziwezi kuwa pamoja.
Huu ni mtizano wangu kwamba haya yanayokwenda live yanatia chumvi miyoyo ya wapiganaji WETU, wataanza kutunishiana misuli na kushirikiana kinafiki.
Stagomena Tax fanya analysis mshauri Mhe. Rais naamini atakusikiliza. Mahakama imetegwa na kesi ndogo ndani ya kesi kubwa kwa lengo lakuhakikisha kila kitu kinawekwa adharani na msidhani kwamba kina Kibatala wanatumia akili zao yawezekana wapo majaji, generals, watumishi waandamizi wanawapa mbinu hizi, this is not normal , mbinu hizi nikubwa sana ila kwa sababu naamini hakuna kiuongozi mwandamizi anayefuatilia kinachoendelea ndio maana hatujaona action kwa niaba ya nchi.