Tuhuma za Rais wetu kuhongwa suti: Marekani ituombe radhi!

Scrap!

Kama kahongwa kweli ni vibaya wao kusema? Ukisikia WANTED: ASSANGE - by USA unafanya mchezo? Hakuna kuombwa radhi, mtafuteni ASSANGE j.
 
naukifuata utaratibu wa hongo zinavyofanyika, mimi sioni sababu kabisa ya marekani kutuomba msamaha kwa sababu kisemwacho kipo. Kiini cha tuhuma na madai haya ni Al-Bawadry mwenyewe ndiye alozitoa fedha hizo na pengine ikichunguzwa safari zake London inaweza kugundulika walikuwa London wakati mmoja na JK.

Halafu JK mwenyewe naye hujitakia sana na hii mikutano ya nje kukutana na wafanya biashara ambayo kaifanya London na Marekani kwa hiyo upo uwezekano mkubwa wa hawa wafanya biashara kukutana naye faragha. Kwa mfano mwezi huu unakuja Canada na sii safari rasmi ya Kitaifa bali anakuja kwa mwaliko wa wafanya biashara ulioandaliwa na NGo moja ya wahuni tu. Sasa lije tokea jambo kesho, Ikulu wataanza kujitetea ilihali safari kama hizi sio official na ndizo chanzo cha tuhuma hizi..

As President, JK anatakiwa kusafiri nje ktk safari za Kitaifa tu, kukutana na viongozi wa nchi husika na kuweka mikataba ya kibiashara baina ya nchi. Haya mashirika yakitaka kuwekeza nchini yatapitia balozi kutazama fursa na mikataba ambayo serikali hizi mbili zimeafikiana, kinyume cha hapo tunafanya Umalaya wa kujiuza na hakika lazima kuna mahala tutaharibu tu. Akisha maliza uongozi wake anaweza kufanya ziara kama hizi labda aandike kitabu chake na hiyo Phd yake atakaribishwa majukwaani.
 
zawadi ngapi anapewa na mataifa ya kiarabu lakini hamulalamiki, ila kupewa na mmarekani ni zambi! acheni chuki kwa mataifa matajiri. semeni pia irani inatuhonga nini! Gadafi alikuwa nagawa mabenzi kwa raisi na baraza lake la mawaziri lakini hakuna hata siku moja mtanzania kalalamika, ila leo marekani ina lalamikiwa! jamani kueni!!
 
Wanabodi,

Kitendo aliyekuwa Balozi wa Marekani nchini, Michael Ritze cha kupitia mtandao wa Wiki Leaks, kumtuhumu Rais wetu, Jakaya Mrisho Kikwete, kuwa amehongwa pair 5 za Suti za Savile Row, sio tuu ni cha udhalilishaji wa hali ya juu kwa mkuu wetu wa nchi, bali ni matukano kwa Watanzania kwa ujumla wetu kwani Rais wetu ni kama baba wa familia kwenye nyumba yetu, hawezi baba yetu kudhalilishwa sisi watoto ambao tunaishi kwenye nyumba hii tukakaa kimya.

Kukanusha peke yake hakutoshi, tunataka Marekani imuombe radhi rais Kikwete na Watanzania kwa ujumla kwa kadhia hii ya Wikileaks.

Mara baada ya JF kutundika bandiko la kadhia hii, Ikulu ilikurupuka kutoa taarifa ya kukanusha. Nimesema Ikulu ilikurupuka kukanusha vipengele vya rushwa tuu kwa kukanusha yaliyonukuliwa na JF badala ya kuifuata ile link na kuyakanusha yote yanayohusiana na Tanzania. Kwa vile source mama ipo na tuhuma zinazidi kushuka, ilikuwa ni busara kwa Ikulu kukanusha yote in details once and for all vinvyo na tusubiri kuona ni mangapi Ikulu itakuwa inasafisha kila kukicha.

Mengi yaliyokanushwa na Ikulu, sio yale ya Wiki leaks, bali ya Wiki Leaks yaliyoandikwa JF. Kufuatia kanusho hilo, yule atoa taarifa kwa Balozi wa Marekani, Bi. Lisa Pile, naye ametumiwa sio taarifa ya Wiki Leaks, bali ametumiwa ile thread ya JF ambayo imeandikwa kwa lugha ya Kiswahili. Matokeo yake, Bi. Pile anakanusha kuwa yeye hajui Kiswahili na wala hakuwahi kukutana na JK hivyo wanamsingizia. Ilitakiwa huyu Bi Lisa atumiwe ile link ya WikiLeaks na sio hiyo ya JF waliomtumia. Alitakiwa akanushe kukutana na balozi wa Marekani au akanushe hakumwambia balozi Ritze kile balozi huyo alichoripoti nchini kwao na kunukuliwa na Wikileaks tujue Balozi ndie muongo hivyo kutupa haki Tanzania kuombwa radhi na JK kutendewa haki sio tuu kwa kuombwa radhi, bali pia kufidiwa kwa madhara aliyoyapata kwa kuchafuliwa reputation yake.

Badala ya kukanusha kilichoandikwa na Wiki Leaks yaani alichoongea na Balozi wa Marekani, hiyu bibie amekanusha hajui Kiswahili na hajawahi kukutana na rais Kikwete wala rais yoyote. Nani kamwambia bibi huyu kuwa kaongea Kiswahili au kakutana na JK?. Hebu soma hilo kanusho hapo chini lenye headline ya thread ya JF!.

Kufuatia kanusho hilo la Bi. Pile, Mmiliki wa Kilimanjaro hotel Albawadry naye ametoa statement ya kanusho akimtetea Bi. Pile kuwa kweli hajui Kiswahili hivyo yote ni uwongo!.

Kwa vile chanzo cha uwongo wote huu ni taarifa ya Balozi wa Marekani kipindi hicho, Bw. Michael Ritz, Serikali ya Tanzania, kupitia njia za kidplomasia,
1. Kwanza Lisa Pile apelekewa taarifa rasmi za Wikileaks na akanushe hayo aliyomweleza balozi wa Marekani maana Pile ndie chanzo kilichonukuliwa na balozi. Hiyo taarifa ya Pile kukanusha kilichoandikwa Jf ni nothing.
2. Waziri Membe kupitia njia za Kidiplomasia, kuulazimisha ubalozi wa Marekani nchini, Kukanusha taarifa hizo za aliyekuwa balozi wake nchini si za kweli bali ni uzushi wa aliyekuwa balozi wake hivyo kumuomba radhi JK na Watanzania kwa jumla.
3.Balozi Michael Ritz popote alipo, ama athibitishe alichoandoka ndicho alichoambiwa na Pile, au akiri kuwa kuwa yeye hakuzungumza hayo na Bi. Pile bali ndiye mzushi aliteutunga uwongo ule hivyo kumuomba rasmi radhi JK na kumpa JK fursa ya kudai fidia na Watanzania tutapoozwa kidogo japo kwa chochote kitu.
4. Wasaidizi wa Rais JK, kuanzia Ikulu mpaka chini, kunapotokea rais kuchafuliwa, muwe mstari wa mbele kumsafisha na kuilinda hadhi na heshima yake instantl na promptly mapema kadri iwezekanavyo, na sio kusubiri mpaka Mtandao wa JF uweke hadharani ndipo mkurupuke na kujibu tuhuma za JF ambazo ni nusu nusu, jibuni tuhuma za Wiki Leaks!.

Mbona ni mengi, mabaya, machafu, ya kudhalilisha na kutia aibu yamesemwa na Wiki Leaks nanyi mko kimya tuu bila kukanusha lolote, kitendo cha kuibuka na kukanusha hili la hongo kwa JK pekeyake, huku sio kukanusha proper, ni kujikomba komba kwa rais muonekane nanyi mko kazini!

JF ilipoziweka tuhuma zile, iliwawekea mpaka link ya Wiki Leaks, kilichowafanya msifungue hiyo link na kukanusha tuhuma zote moja baada ya nyingine ni nini, hadi kuwapelekea waarabu tuhuma za Kiswahili na Mtoa habari Bi. Pile kupelekewa taarifa ya JF ya kiswahili badala ya kumpa taartifa halisi ya Wiki Leaks?!.

Kwa vile kwenye ile link ya Wikileaks kuna tuhuma lukuki mle, kuanzia ile ya Hosea, itakuwa ni busara na kuwatendea haki Watanzania, sasa kama mtaingia kazini rasmi, na kuanza kupangua tuhuma moja baada ya nyingine kwa, vinginevyo usafishaji huu wa tuhuma za rais peke yake, utaishia kugeuka ni 'Funika Kombe, Mwanaharamu Haramu Apite!'...wenye akili zao watakuwa wameisha pepeta kujua pumba ni zipi na mchele ni upi, na badala ya kumsafisha rais wetu, mnajikuta ndio kwanza mnazidi kumpaka ....!.

Wito kwa Wana jf wenzangu kwenye issues kubwa kama hizi, zinazomhusu kiongozi wetu mkuu wa nchi, nawasihi sana, tuache mambo ya mizaha. Tuhuma hizi ni mzito na very serious, tunapozijadili, naombeni sana tuwe serious accordingly na kutumia lugha za Staha kwa Viongozi wetu.

Rias Jakaya Kikwete ni rais wa nchi yetu, yeye sio tuu ndiye mtu mwenye jina la JK, bali yeye ndie mkuu wa taasisi ya urais, ambayo ndio taasisi yenye hadhi na heshima kuliko taasisi zote hivyo inastahili heshima yake.

JK ndiye rais wetu, uwe ulimchagua, ua hukumchagua, uwe unamkubali au haumkubali, yeye ndiye rais wetu na ni rais wa wote hata hao alioshindana nao, this is not debateble fact ni hard fact. Naomba awe addressed kwa heshima stahiki.

Mode: For the sake of this thread, naomba muimoderate effectivel na kama mko busy sana naomba nipewe u-mode kwa muda only for the sake of this thread ili post zozote za kipuuzi puuzi zenye lugha isiyo na staha, nizifutilie mbali, ili zisichafue lengu, madhumuni na maudhui ya mjadala kwenye thread hii kwa maslahi ya taifa.

Wasalaam.

Pasco.

Nimesoma koote nilipofika hapo kwenye red nimechoka kabisa
 
Nimesoma koote nilipofika hapo kwenye red nimechoka kabisa

Usichoke ndugu yangu ndio matunda ya demokrasia hayo; kila mtu ana uhuru wa kuongea anachofikiri hata kama hakina mantiki yoyote. Cha muhimu hapa ni kuipinga kila hoja aliyoitoa kwa hoja yenye nguvu zaidi.
 
Nilitegemea email itakuwa ni ya kiofisi na si hotmail.com. Sound like 'hoax' material. Msemaji wa Ikulu alitakiwa kumjibu mmiliki asilia wa hiyo 'kebo' . Angalizo: Rweyemamu alijaribu kujustify kwa kusema jamaa mwenyewe kwanza aliondolewa bongo baada ya msuguano na waajili wake...naona alitaka kupindisha suala la msingi ambalo ni : Je JKM ALILISAFIRISHWA KWEND KUNUNULIWA SUTI na madudu mengine mengi...Kwanini MFA wanakimbia issue yao??
 
SOMA HAPA WEWE NA POST ZAKO ZA KIUSHABIKI, FATILIA ISSUES BROTHER!*DAR ES SALAAM — Surprising how some global events end up beating a path to your own front door. Just this morning I was reading a WikiLeaks U.S. cable written by the U.S. Embassy in Tanzania, which accuses Tanzania’s President, Jakaya Mrisho Kikwete, of accepting bribes to the tune of $1 million from the UAE-based owner of the Kempinski Hotel chain, Ali Albwardy.In addition to the bribe, Kikwete is accused of accepting a lavish shopping trip to London. Among other things, “Ali albwardy bought Kikwete five Saville Row suits”. President KikweteThe fact that a cash amount is mentioned, or that a ‘contribution’ was made to his CCM ruling party isn’t an issue at all; under Tanzanian law, donations to a political party are allowed. But having stayed at the Kempinski Kilimanjaro in Dar es Salaam on quite a few occasions, it did intrigue me enough to dig further.What is interesting however, according to the cable transcript, is the fact that Albwardy wanted to secure the rights to build a hotel on the edge of Ngorongoro Crater and “another on the Serengeti plain overlooking the main animal migration routes”.Stringent conservation rules currently ban the construction of permanent structures inside national parks, including in the crater and on the Serengeti Plain.It would appear that even back in 2006 – when the cable was written – the hotel publicity director, Lisa Pile, was already hinting that legislation would be changed in order to allow the construction.Convenient coincidence this probably is not, and corporate business affairs aside, when a democratic process is swept aside, this type of conduct is nothing more than corruption at the highest levels.Original CableC O N F I D E N T I A L DAR ES SALAAM 000277SIPDISDEPT FOR INR, R.EHRENREICHE.O. 12958: DECL: 02/13/2016TAGS: PGOV PREL TZSUBJECT: KIKWETE CORRUPTION TIDBITClassified By: Ambassador Michael Retzer, Reason 1.5 (d)¶1. (C) President Kikwete has accepted gifts (bribes) fromthe owner of the Kempinski Hotel chain,s Tanzanianproperties, a citizen of the United Arab Emirates.¶2. (C) In a conversation with the manager and the publicitydirector of Dar Es Salaam,s Kilimanjaro-Kempinski Hotelhours after accompanying A/S Frazer to her October 18, 2005meeting with then-Foreign Minister Kikwete, I commented onKikwete's flashy attire, asking "Who dresses him?" "We do,"they responded. Initially thinking this meant Kikwetefrequented a men,s shop in the hotel, I learned later inthe evening from hotel publicity director Lisa Pile (protect)that the hotel owner*UAE citizen Ali Albwardy*had recentlyflown Kikwete to London for a subsidized shoppingexpedition. Among other things, on that trip Ali Albwardybought Kikwete five Saville Row suits. He had also recentlymade a $1 million cash contribution to the CCM (which is alegal contribution under current Tanzanian law).¶3. (C) Pile told me the Kempinski Hotel chain is greatlyexpanding its presence in Tanzania. She said that inDecember it would open "the best hotel in Zanzibar." Herprediction was a little off; the new Kempinski hotel, locatedon the beach on Zanzibar,s east coast, opened January 5. Iattended the opening ceremony along with Zanzibari PresidentKarume, who was asked publicly by Ali Albwardy for a site inStone Town to build a new hotel. Later that day, Pilerevealed that the Zanzibar government had already earmarkedfor Ali Albwardy a hotel site in Stone Town.¶4. (C) Pile also said in the October 18 conversation that AliAbwardy was about to receive the rights to construct two newhotels on the mainland: one on the edge of Ngorongoro Craterand another on the Serengeti plain overlooking the mainanimal migration routes. Stringent conservation rulescurrently ban the construction of permanent structures insidenational parks*including in the crater and on the Serengetiplain*but Pile said that in November legislation would beintroduced to parliament to authorize the new hotels.(Comment: We have received no reports on new legislation,but the Dar Es Salaam Daily News on January 15 reported thatthe Tanzania National Parks Authority had approved constructionof a five star hotel on the Serengeti plain.)¶4. (C) Later on October 18, over dinner, an Indian/SouthAsian man described as a business associate of Ali Albwardybriefly took Pile from the table for a conversation inKiswahili. I am not sure what was said, but Kikwete's namecame up several times and he passed her an envelope. Piletold me the envelope was stuffed with 1 million shillings( $1,000) and was to pay for a Kikwete meeting at theKilmanjaro-Kempinski later that month. Apparently Kikwete isa regular customer, but no name ever appears on the hotelregistry when a government bigshot has an "event" in one ofthe guest rooms.¶5. (C) Bio Note: Lisa Pile, an Australian citizen, haslived in Dar working for Kempinski Hotels since early 2004.Before that she had served in a similar capacity with theKempinski chain in China. Her family in Australia is prominent inAustralia's Liberal Party (the center-right party of PrimeMinister John Howard).¶6. (C) Comment: What does it all mean? I don,t know, butmy guess is that the investor Ali Albwardy has access tooil money out of the UAE. I suspect giving free clothes andthe campaign donation is just the way these people do business.¶7. (C) For his part, Kikwete probably thinks having all thesefive star hotels around is a good idea for the country,and Iagree with him. His new minister of Natural Resources andTourism, Anthony Diallo, says he wants to double tourism,scontribution to the national economy in ten year,s time.Kikwete probably believes there is no harm in taking these&little gifts8 to do what he would have been inclined to doanyway. That said, they are what they are: bribes.
 
Wanabodi,

Mode: For the sake of this thread, naomba muimoderate effectivel na kama mko busy sana naomba nipewe u-mode kwa muda only for the sake of this thread ili post zozote za kipuuzi puuzi zenye lugha isiyo na staha, nizifutilie mbali, ili zisichafue lengu, madhumuni na maudhui ya mjadala kwenye thread hii kwa maslahi ya taifa.

Wasalaam.

Pasco.

Pasco.
Si ungeiweka tu kwenye jukwaa lako lile restricted "Hoja Kali" sijui "Hoja za Maana" or some crap like that. Uandike, ujijibu mwenyewe, ujihoji bila kuingiliwa na opinions za freewheeling brainstorming JF'ers.
 
Kwani mwashangaa nini? Hamjui kuwa viongozi wenu akiwemo Rais Kiwete ni ombaomba tangu enzi hizo akiwa Waziri na mpaka leo akiwa kwenye Urahisi bado ni ombaomba?

Tumesikia alinunuliwa suit, akapewa na pesa za kulipia gharama za Ukumbi wa Mikutano pale Movenpick wakti wa harakati zake za kuupata Urahisi. Sidhani kama Balozi Retzer wa USA ni mpuuzi kiasi hicho cha kuanza tu kumpakazia Kiwete maneno ya uongo.

Kumbuka kuwa wenzetu weupe wako very transparent hata kwenye mambo ambayo wewe unayaona hayana maana. Najua kuna viongozi wengi tu wa Serikali yetu wanaposafiri nje ya nchi wanapokutana na wenyeji wao LAZIMA HUOMBA RUSHWA AU HONGO ili kujinufaisha. Hawakosi kuomba NAFASI ZA MASOMO KWA AJILI YA WATOTO WAO,NDUGU ZAO,MARAFIKI n.k.Kwa hiyo kuomba suit au kununuliwa suit siyo jambo la ajabu hata kidogo. Haya mazingira wameyaumba wao wenyewe:MAZINGIRA YA OMBAOMBA.

Naamini kuna madudu mengi sana kama haya kwa Rais,Mawaziri,Makatibu wakuu na hata Wabunge HASA LINAPOKUJA SWALA LA UWEKEZAJI HAPA NCHINI. Kwa vile Wawekezaji/Wazungu walishajua UDHAIFU WETU WA OMBAOMBA wanajua kabisa nini cha kufanya wanapokutana na hawa VIONGOZI WETU UCHWARA.

Marekani haihitaji kuomba radhi yoyote wala Balozi wake. Haya LAZIMA YAMETENDEKA. Sana sana cha kukazania hapa ni kutafuta USHAHIDI KAMA KIWETE ALIHONGWA SUIT BASI AJIUZULU MAANA AMELIDHALILISHA TAIFA LETU.

Najua kabisa kila kiongozi anaposafiri kwenda nje ya nchi hupewa OUTFIT ALLOWANCE,posho inayomwezesha kununua suit yenye hadhi ya kimataifa. Lakini kwa vile viongozi wetu ni WAROHO NA WALOJAA TAMAA HATA AKIPEWA SUIT 100 ATAZIPOKEA TU!!!!!!
 
Sioni sababu ya USA kuomba radhi Tanzania. Huo ni ukweli dhahili. Kama ni uongo kaangalie location ilipojengwa Belila Kempinsky Lodge kule serengeti National Park. Rais wenu/wetu amejidhalilisha mwenyewe kwa kupata posho. Nakubaliana na wadau waliotangulia issue ni kwenda kumlekebisha Kikwete aache hujinga na kuiuza nchi. Na sio kwenda kumlalamikia jirani (USA) kua ndio chanzo. Acheni kuwapotosha hii issue, ili iwe fundisho kwa marais wajae.
 
kupotezea, yaishe! au mwenye uchungu rohoni mahakama ziko wazi!
 
Hamna haja ya kuomba radhi. Mwache aibike mwenyewe, kwani mimi mtz ndie niliyehongwa hizo suti. Hapo ameaibika JK mwenyewe na tamaa zake. Akome,.
 
Scrap!<br />
<br />
Kama kahongwa kweli ni vibaya wao kusema? Ukisikia WANTED: ASSANGE - by USA unafanya mchezo? Hakuna kuombwa radhi, mtafuteni ASSANGE j.
na hata wakimtafuta wajue hawampati..ASSANGE ana documents live, ndio maana anajiamini. Jk adhubutu aone kama hajaaibika.
 
Sweet dreams! Sweet dreams! Tuna hulka ya kudhani ukombozi wetu unaletwa na watu wa mataifa makubwa na hata mara nyingine kwa gharama kubwa kabisa ya kuuza uhuru wetu kama individuals au Taifa. Haya tunayoyaona ni mavuno ya yale tuliyopanda! Wamewajaza spies kibao kwa jina la kuleta na kusimamia misaada na mambo yanayoendana na hayo. Eti leo watuombe radhi...ndoto njema huanza asubuhi
 
Jk aliyataka mwenyewe..na akomeshwe. Hii ni aibu kubwa kwake. Na hana ubavu wa kuwashtaki wikileaks kwakuwa wana ushahidi wa documents. Sasa watampata wapi Assange? Good weakleaks, vujisheni mauchafu ya serikali yetu.
 
Ona na hii hapa ya hao unaowatetea......uongo mweupe umetumwa white house...

1. (SBU) Summary: From January 7-23, when Embassy Dar es
Salaam had the use of a Twin Otter airplane from Prescott
Aviation, mission personnel traveled to five of Tanzania's
26 regions: Mwanza, Shinyanga, Mtwara, Mbeya and Ruvuma.
These five regions form an arc through western and southern
Tanzania, which begins at Lake Victoria, then proceeds
along the shores of Lake Malawi and across the Mozambican
border. Our choice of itinerary was motivated partly by
our interest in seeing Tanzania's most remote areas while
we had a chance to do so. ……..


(C) Shinyanga is the hometown of Prime Minister
Frederick Sumaye, who is campaigning vigorously to be the
ruling party's nominee for president. The Regional
Commissioner for Shinyanga told emboff he had spent the
last two days touring the region in preparation for the
Prime Minister's upcoming visit. The Regional Commission
was expected to "pave the way" for the Prime Minister's
campaign. Paving the way often includes giving cash
presents to important local leaders to ensure their
support. The Regional Commissioner, who is a CCM appointee
from outside Shinyanga, was keenly interested to ensure the
visit went well.


Tunaomba Link ya topic hii,manake umeleta kitu ambacho kumbe hata sisi wenyewe watanzania wenyewe hatujuani nani katoka wapi kwa kuwa tumekalilishwa sana.

Naanza kama ukitoa link ya wikileaks hii,nikakuta taarifa hii uko hakika wamarekani watakuwa ni kiboko,manake nataka kuunganisha matukio na kujalibu kujenga logic na assumption juu ya mtajwa na mkoa huo,manake wakati wa uchaguzi wa mwaka 2005 Shinyanga hakika ilikuwa ndio kila kitu kwake,japo najua anatoka Arusha,ambayo inapakana na Shinyanga,inaonekana inaweza kuwa kijografia jamaa akawa na asili ya Shinyanga..Lakini huku wabongo wakakalishwa kuwa ni Arusha.
 
Linchi lenye laana. Yaani mtu akishakuwa kiongozi afanye atakavyo na asisemwe, halafu baada ya hapo mtegemee mkubwa fulani kwenye uwaziri au popote akiboronga ajiuzuru wakati kumbe haitakiwi hata kuweka madudu yake hadharani. Ndo maana huwa najiuliza inakuwaje kwa miaka kadhaa wabunge wengi siyo mmoja wengi wanahongwa na wizara mbalimbali na hakuna anayehoji! Siyo waandishi, takukuru wala nini sijui wote kimya. Hivi huko bongo mnakula nini? Maana ikiwa kiongozi anakosea na hatakiwi kuguswa, kusemwa wala kukosolewa...yaani ni balaa tupu.
 
Back
Top Bottom