Tuambiane ukweli:Jee umezindika biashara yako?

Tuambiane ukweli:Jee umezindika biashara yako?

Kama ni aslimia 90 watu wamezindika biashara zao pia unabidi ukumbuke kuwa asilimia 95 ya wafanyabiashara wote wanalalamika kuhusu chuma ulete.
 
Kuna mjadala niliukuta mahali jana kuwa ni lazima kuzindika biashara na kwamba asilimia 90 ya biashara hapa bongo mfano wenye maduka huwa wanazindika biashara zao

Haya maneno sikuyaamini kwamba kila biashara au kila frem ninayoiona kila mmiliki keshatembea kidogo

Nikasema mbona ni asilimia kubwa sana?Maana kulingana na wanavyoongea ni kwamba ni jambo ambalo limekua kama la lazima hivi

Binafsi nikiri ukweli kuwa hata mimi nimefanya hivyo, japo maeneo niliyoweka frem hapana changamoto yoyote ila nilishauriwa na jamaa angu mmoja nifanye hivyo nikafanya lakini naona ni kawaida tu kwangu wala sioni maajabu yoyote ni miaka 2 sasa imepita

Swali kwa mnaomiliki biashara jee kuna ukweli?Jee umezindika biashara yako ili watu wasikuchezee au mambo ya chuma ulete?
Tawile mganga
 
Sijazindika na sitazindika ingawa nilipoanza biashara yangu watu walinifuata kunishauri nizindike kwasababu chuma ulete lile eneo ni wengi. Sikufanya hivyo na biashara yangu inaendelea kukua na haijatokea siku imepotea hela kimiujiza kwenye biashara yangu.
Nimeshuhudia wengi waliosifika kwa kuzindika biashara zao zikifilisika, vibuyu na tunguli havikuweza kuinusuru biashara zao.

Biashara ni umakini uki lose concentration tu kidogo umepata hasara ambayo utasema ni chuma ulete.
 
Kuna mjadala niliukuta mahali jana kuwa ni lazima kuzindika biashara na kwamba asilimia 90 ya biashara hapa bongo mfano wenye maduka huwa wanazindika biashara zao

Haya maneno sikuyaamini kwamba kila biashara au kila frem ninayoiona kila mmiliki keshatembea kidogo

Nikasema mbona ni asilimia kubwa sana?Maana kulingana na wanavyoongea ni kwamba ni jambo ambalo limekua kama la lazima hivi

Binafsi nikiri ukweli kuwa hata mimi nimefanya hivyo, japo maeneo niliyoweka frem hapana changamoto yoyote ila nilishauriwa na jamaa angu mmoja nifanye hivyo nikafanya lakini naona ni kawaida tu kwangu wala sioni maajabu yoyote ni miaka 2 sasa imepita

Swali kwa mnaomiliki biashara jee kuna ukweli?Jee umezindika biashara yako ili watu wasikuchezee au mambo ya chuma ulete?
mimi nimezindika kazi yangu!!
 
Umeulizwa je, umezindika biashara yako? Wewe unaanza Ni Imani potofu, hajauliza Kama Ni Imani potofu.
Hupendi kuambiwa ukweli kwa Kuwa ni mmoja wa mliozindika😂
 
Habari wadau, kwa wale wanahitaji kuweka mahesabu ya kampuni sawa
 

Attachments

  • 20230517_184110_0001.png
    20230517_184110_0001.png
    206.1 KB · Views: 20
Sisi waafrica utaratibu ni huo...sio biashara tu hadi nyumba hadi watoto wanafanyiwa zindiko ni mila na desturi za enzi na enzi..

(hakuna familia yyte ya kiafrica ambayo aijapitia huko ni hizi dini za wazungu na waarabu ndio wanatubadilisha sasa)

Ingawa haigurantee kuwa utafanikiwa kwenye biashara yako bado maarifa ya biashara yananafsi kubwa kama huna hayo ni swala la muda tu unafirisika na kusingizia wachawi.
Fact
 
Kuna wakati nilikabidhiwa sehemu yangu ya biashara baada ya mpangaji kufilisika

Nikaamua kufungua mwenyewe
Nilimtuma kijana afanye usafi kote, kumbe kulikuwa na mgogoro baina ya mke na mme na wakaamua kuondoa vitu kwa hasira

Kijana kanipigia simu anasema njoo uone haya mambo
Kulikuwa na vitu vya ajabu naona walikuwa sijui wanarogana wao kwa wao au ni mambo ya biashara

Dogo aliogopa kuvigusa nikampa ujasiri na kuvitoa vyote kwa mkono

Nikaviweka nje nikamwambia haya piga kiberiti yote
Nilifungua biashara yangu bila ushenzi huo na nikajaaliwa kuiendeleza

Kama ukiona watu wanapanda haraka haraka kwenye biashara wengi wao ni majizi wanaoshirikiana na wafanyakazi wa wholesalers
Aisee
 
Huo ni ushamba,na upungufu wa matumizi ya akili,mchawi wa biashara yako ni wewe mwenyewe,unamhudumia mteja wako kwa nyudo na jeuri,au ukiwa mlevi,au kwa lugha chafu,au kwa kuto mjali halafu unaenda kwa mganga biashara ngumu [emoji848].Utakuwa mwehu wewe [emoji23]
Nani kasema[emoji28]
 
Sijazindika na sitazindika ingawa nilipoanza biashara yangu watu walinifuata kunishauri nizindike kwasababu chuma ulete lile eneo ni wengi. Sikufanya hivyo na biashara yangu inaendelea kukua na haijatokea siku imepotea hela kimiujiza kwenye biashara yangu.
Safi
 
Kwenye jumuiya yetu ( FREEMASON ) huwa tunzindika kwa kutumia kichwa cha mbuzi na damu ya mbuzi lita 1. katika majengo au biashara unayo miliki.
 
Kuna mjadala niliukuta mahali jana kuwa ni lazima kuzindika biashara na kwamba asilimia 90 ya biashara hapa bongo mfano wenye maduka huwa wanazindika biashara zao

Haya maneno sikuyaamini kwamba kila biashara au kila frem ninayoiona kila mmiliki keshatembea kidogo

Nikasema mbona ni asilimia kubwa sana?Maana kulingana na wanavyoongea ni kwamba ni jambo ambalo limekua kama la lazima hivi

Binafsi nikiri ukweli kuwa hata mimi nimefanya hivyo, japo maeneo niliyoweka frem hapana changamoto yoyote ila nilishauriwa na jamaa angu mmoja nifanye hivyo nikafanya lakini naona ni kawaida tu kwangu wala sioni maajabu yoyote ni miaka 2 sasa imepita

Swali kwa mnaomiliki biashara jee kuna ukweli?Jee umezindika biashara yako ili watu wasikuchezee au mambo ya chuma ulete?
Hapo ulipozindika hapana changamoto ni kwa sababu wazee walishaona umepazindika, wanakuogopa.
 
Back
Top Bottom